Zama za Mayele Yanga zimekwisha, wachambuzi fungeni huo ukurasa wake

Zama za Mayele Yanga zimekwisha, wachambuzi fungeni huo ukurasa wake

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Wachambuzi wetu ni low profile, tuwasaidie kuwaandalia ajenda. Mayelle aliletwa Yanga na viongozi wa Yanga, kabla ya kuletwa Yanga alikuwa hatambuliki na wachambuzi wetu. Mayelle alikuwa na kipaji kilichonolewa na Nabi sawa na Fei Toto na wachezaji wengine pale Yanga ambao kabla ya kuja Yanga na kukutana na Nabi walikuwa na vipaji ambavyo havikuendelezwa.

Wachambuzi wetu wanajenga hoja kwamba Mayelle hakutakiwa kuondoka Yanga milele, Yanga bila Mayelle imekwisha na pengo la Mayelle haliwezi kuzibwa na waliopo sasa na waliosajiliwa. Kuwaza kwa namna hii kunaturudisha nyuma; yaani ligi yetu na mpira wetu unazidi kukua lakini waandishi na wachambuzi wa mpira ama wako vilevile au wanarudi nyuma.

Mayelle ni mchezaji bora kabisa kutokea tangu tanzania hii kuumbwa; na ubora wake ukom pale alipoweza kuwa mfungaji bora wa mashindano ya CAF rekodi ambayo haijafikiwa na mchezaji yeyoyote yule Tanzania. Hata hivyo unapomsifu mkiambiaji lazima umsifu zaidi yule anaemkimbiza. Mayelle alikuja Yanga akitokea ligi ya DR Congo lakini hakuwika kama alivyowika Yanga, hii inaonyesha kuwa sifa ya kwanza lazima iende kwa Eng. Hersi na uongozi wake, GSM, benchi la ufundi, wachezaji wezake na mashabiki wa yanga waliokuwa wako nyuma yake.

Kama Eng. Hersi na wenzake, bench la ufundi, wachezaji na mashabiki bado wako yanga, nina imani kuwa pengo la mayelle litazibwa na hata mayelle anaweza kuomba kurudi tena yanga bila kupata nafasi kwakuwa nafasi imejaa.

Wakati ligi yetu inaongezeka thamani hata wachambuzi wetu wasibaki palepale na vilevile.
 
Kama Eng. Hersi na wenzake, bench la ufundi, wachezaji na mashabiki bado wako yanga, nina imani kuwa pengo la mayelle litazibwa
Benchi la ufundi halipo, kwa hiyo kwa maelezo yako, wachambuzi wapo sahihi kuwa pengo halitazibika
 
Benchi la ufundi halipo au limebadilika?
Kwa maana hiyo hata Eng. Hersi asipokuwapo akaja rais mwingine, mfano Haji Manara, mambo yatakwenda tu. Basi haukutakiwa kumpa credit Hersi kwa kumtaja kwa jina lake, bali ungemtaja kwa cheo chake
 
Inabidi tuvumilie ndio aina ya wachambuzi tulionao kwasasa, Mambo hubadilika taratibu kwa sasa wachambuzi wetu wengi wapo kwenye zama za Volkswagen mgongo wa Chura wakati dunia ipo kwenye Lamborghini.
Mchambuzi anatumia kiredio cha mtu kudai eti timu "imepigwa" kumsajili mchezaji fulani, ukimuuliza taarifa kama hiyo kwa umma ina faida au lengo gani nae hajui, amejisemea tu. Wewe ni nani, una ujuzi gani na umechangia nini hata useme timu imepigwa. Yaani mtangazaji nae anavaa koti la ushabiki kwenye chombo cha habari ambacho sio cha timu. Maana kama taarifa ukiikuta kwenye App, insta, tv au gazeti la Yanga, Simba, Azam au timu nyingine unaweza kusamehe maana hiyo ndiyo kazi yake.
 
Benchi la ufundi halipo au limebadilika?
mtu mwenye weledi unawezaje kusema pengo la mayelle, chama, dube,...... haliwezi kuzibwa? yamezibwa mapengo ya akina Messi na Ronaldo sembuse la mayelle? wakati ligi yetu ikichanja mbuga Afrika na tanzania ikihangaika kutafuta nafasi ya kuendesha mashindano ya CAF mwaka 2027 TFF kwenye kanuni zake itupie jicho upuuzi kama huu unaokinzana na maendeleo haya ya soka. Timu zetu zinasajili na kutunza wachezaji kwa bei kubwa sana, mtu anatoka kujisaidia haja kubwa yenye harufu ya dagaa halafu anasema umemsajili Ngoma mmepigwa, amejaa majeraha, sijui njini? kumbukeni mchezaji pia ni binadamu, anastahili kuheshimiwa.
 
Kila kipindi kinachohusu michezo lazma uskie story za mayele.
 
Kiufupi tu wachmbuzi wetu wengi wa bongo n wavivu wa kutafuta habari wanasubiri tu issue za umbea ndio wanajiona tyr wachambuz in short hatuna wachambuz tuna mashabiki
 
Kiufupi tu wachmbuzi wetu wengi wa bongo n wavivu wa kutafuta habari wanasubiri tu issue za umbea ndio wanajiona tyr wachambuz in short hatuna wachambuz tuna mashabiki
Ligi yetu Ina wageni wengi na timu zetu 4 zinashiriki mashindano ya kimataifa, hivyo zitakuja timu nyingi, wachezaji na makocha wengi wa kigeni pia, hivyo Wachambuzi na wanahabari wetu wajifunze kugja za kigeni na kujifunza namna ya kuhoji na kuuliza maswali wageni ili kuepuka aibu.
 
Tanzania hakuna wachambuzi wa mpira bali kuna washabiki wa timu wanaotoa maoni na mpenzi ya timu zao kwa mwavuli wa uchambuzi. Majuzi nilisikiliza radio tano tofauti wanazungumzia juu ya jezi namba 20 ya Simba wanatumia zaidi ya saa nzima kuijadili jezi hiyo.
 
Wachambuzi wa makolo ni vichwa maji ukianzia na msemaji wao!
....
Badala ya kuhangaika na kukosa kipa wa uhakika mpaka Simba Day inafika,wao wanahangaika na issues za timu nyingine!
Hivi zile Goli Mbili Bila za Inonga na Kibu de.

Golikipa wa Simba alikuwa nani ?

Acheni dharau kwa Wazawa.

Ally Salimu.
Huko uliko jifue sana
Hakuna aliyezaliwa Golikipa ni Bidii ya Mazoezi tu
 
Hivi zile Goli Mbili Bila za Inonga na Kibu de.

Golikipa wa Simba alikuwa nani ?

Acheni dharau kwa Wazawa.

Ally Salimu.
Huko uliko jifue sana
Hakuna aliyezaliwa Golikipa ni Bidii ya Mazoezi tu
Ally Salum anazo cleansheet ngapi kwenye ligi kuu?
 
Back
Top Bottom