Zama zetu kali. Unakijua hiko kidubwasha wewee!?

Zama zetu kali. Unakijua hiko kidubwasha wewee!?

Tulipenda mpira wa visoda, mimi niliipenda sana brazil enzi hizo za kina rivaldo, dunga na 8, ronaldo na 9, na wengine. Kila kisoda kilipewa namba yake.

Pia tulibandika picha za jojo za wachezaji kwenye madaftari. Tulishindana kujaza wachezaji bora hasa wale wa brazil
 
40+ ndio watu pekee kutokea wenye akili kubwa zote na michezo yote wamecheza. Kuna Butua,wengine wanaita kombolela,kuna “mwakabunguja”,hii ndude unachukua viazi vitamu,unaviweka kiasi kama viazi 10,15 hivi unachimba shimo kidogo unazungushia mabonge ya udonge,unawasha moto huko ndani,unaziba,baada moto kuwa unaanza kupiga. Hiyo hasa huko kwenye kuchunga ng'ombe.Kwa tuliokulia Bush countries

kuna kujenge ghetto lako barabarani kwa home. Ile kipipindi cha sikukuu mnachangiana labda vijana kama wa5 hivi. Mnachagua ghetto la mmojawenu,mnatengeneza mzunguko wa lisasa,funga mziki wa kutosha,vyakula,makuku kuku n.k. Sikukuu kwenu murua kabisa.

kuna timu za kitaa za viniengo,kabumbu zilikuwa zinaundwa kulingana na eneo,umbali. Siku za week-end kuna viwanja tulikuwa tunakutana hapo,unakuta tumekutana hapo kundi la timu hata mpaka 6. Ilikuwa ni mpira wa kibabe sana,unakuta katikati ya mpira ngumi zinaibuka. Basi kamji kote kanazizima. Ole wako upigwe. Unafika home nako unakutana na fimbo kwa nini uonewe. Basi ilikuwa ni kujengewa ujasiri sana.


Hivyo vishada tumeunda sana,japo vyetu vilikuwa vya makaratasi ya nailon. Tengeneza sana magari ya udongo. Tengeneza sana magari ya mabox,na mambo mengine mengi. 40+ ndio tumefaidi maisha. Tumepitia mengi hatari.

Nashukuru sana yale malezi,ndio yamenifanya niwe imara sana,mvumilivu,mpambanaji,na mtafutaji sana. Sio nyie wa 1995 na kuendelea,hasa 2000 hapo mmekulia ndani tu kuangalia TV tu.
Mimi siyo wa 95 ni wa 98
 
40+ ndio watu pekee kutokea wenye akili kubwa zote na michezo yote wamecheza. Kuna Butua,wengine wanaita kombolela,kuna “mwakabunguja”,hii ndude unachukua viazi vitamu,unaviweka kiasi kama viazi 10,15 hivi unachimba shimo kidogo unazungushia mabonge ya udonge,unawasha moto huko ndani,unaziba,baada moto kuwa unaanza kupiga. Hiyo hasa huko kwenye kuchunga ng'ombe.Kwa tuliokulia Bush countries

kuna kujenge ghetto lako barabarani kwa home. Ile kipipindi cha sikukuu mnachangiana labda vijana kama wa5 hivi. Mnachagua ghetto la mmojawenu,mnatengeneza mzunguko wa lisasa,funga mziki wa kutosha,vyakula,makuku kuku n.k. Sikukuu kwenu murua kabisa.

kuna timu za kitaa za viniengo,kabumbu zilikuwa zinaundwa kulingana na eneo,umbali. Siku za week-end kuna viwanja tulikuwa tunakutana hapo,unakuta tumekutana hapo kundi la timu hata mpaka 6. Ilikuwa ni mpira wa kibabe sana,unakuta katikati ya mpira ngumi zinaibuka. Basi kamji kote kanazizima. Ole wako upigwe. Unafika home nako unakutana na fimbo kwa nini uonewe. Basi ilikuwa ni kujengewa ujasiri sana.


Hivyo vishada tumeunda sana,japo vyetu vilikuwa vya makaratasi ya nailon. Tengeneza sana magari ya udongo. Tengeneza sana magari ya mabox,na mambo mengine mengi. 40+ ndio tumefaidi maisha. Tumepitia mengi hatari.

Nashukuru sana yale malezi,ndio yamenifanya niwe imara sana,mvumilivu,mpambanaji,na mtafutaji sana. Sio nyie wa 1995 na kuendelea,hasa 2000 hapo mmekulia ndani tu kuangalia TV tu.

Hii mwakabunguja ni kwa watu wa Mbeya nafikiri.
 
Yani nikiwa na hiki naweza kimbia km 25 bila kuchoka
 
Hapo unatakiwa ukimbie kuzidi motokaa ili mambo yawe mswano.Utoto raha sana![emoji13][emoji13][emoji13]
Ukirudi jioni yanaonekana meno na macho tu...halafu kuna jiwe,dodoki la kisalufeti na maji ya baridi yamo kwenye karai sasa kama kwenu ndo makambako utafurahi suala la kuoga lilifanana na kuchoma sindano
 
Tulipenda mpira wa visoda, mimi niliipenda sana brazil enzi hizo za kina rivaldo, dunga na 8, ronaldo na 9, na wengine. Kila kisoda kilipewa namba yake.

Pia tulibandika picha za jojo za wachezaji kwenye madaftari. Tulishindana kujaza wachezaji bora hasa wale wa brazil
Umenikumbusha njumu zangu za Romalio...ndo kilikuwa kiatu changu pendwa S/M Masebe
 
Hahaa umesahau kupiga baruti tulikua tunatumia spoko za baiskeli halafu kule kwenye tundu unajaza ule unga wa njiti ya kiberiti
Sisi tulitumia plugs zilizokufa na bolt. Tunaenda garage huko kusaka
 
Ukirudi jioni yanaonekana meno na macho tu...halafu kuna jiwe,dodoki la kisalufeti na maji ya baridi yamo kwenye karai sasa kama kwenu ndo makambako utafurahi suala la kuoga lilifanana na kuchoma sindano
Makambako kule Kitisi?😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom