Zamani ilikua hatuwezi kutengeneza hii....sasa sijui kama wakati huu wa viwanda tunaweza tengeneza hii kitu.

Zamani ilikua hatuwezi kutengeneza hii....sasa sijui kama wakati huu wa viwanda tunaweza tengeneza hii kitu.

Swahiba wewe najua mboga saba mtoto wa mjini haya mambo ya vibegi vya kichina ulikua unabadili unavyotaka mwenyewe.

Sie lazima uvizie suruali chakavu ukate miguu ndio ushone mfuko wa madaftari, kiwanda kingine cha kushona hicho...
Hapana mimi enzi zangu hivyo vibegi vya kichina vilikuwa havijazaliwa...
 
Sie ndio ilikua zetu mkubwa. Tena home wakikaa vibaya unawachenjua unapiga makopo kadhaa ya mahindi unachanganya na yako unaingia black market unauza unasunda mpunga kibindoni...I miss those days
Ila maisha ni safari ndefu sana mkuu yani mm maisha ya bata yalinishindaga utanikuta nachunga mbuzi za watu, naenda gombania ukoko wa ugali na viporo Kwa majirani wakati home mfanyakazi kashaanda chakula ila nikiziweka now day natamani bata sema ndo majukumu yashaniandama
 
Daah! Umenikumbusha mbali,

Nakumbuka vilikuwa vinauzwa mia tano, ila nikawa naogopa kumwambia Bi mkubwa aninunulie na mimi nikatambe,

Kwa kuwa mwenyewe ninaubunifu nikanunua mfuko wa Nailoni ile migumu yenye mistari myekundu na myeupe, nikakata juu kuondoa ile sehemu ya kushikia kisha nikachukua sindano na uzi nikapiga Pindo,

Baada ya hapo nikafumua kiroba nikachukua zile kamba zake kisha nikasokota,

Nikapitisha kwenye lile pindo kisha nikatoboa kwa chini then nikafunga,kwa hiyo ikawa ukivuta zile kamba palle juu panafunga kama ile ya kichina

Sasa na mimi nikawa na Sport Made by mi mwenyewe kufika shule nikafunika vibaya sana, yaani shule nzima nikawa na Sport ya kipekee,

Mvua ikinyesha sasa, mi sina wasi wasi na madaftari kuloa napuyanga kama kawa, wao wenye Visport vyao vya kununua ikawa wanasubiri mvua ikatike,

Bi mkubwa mwenyewe alinipigia saluti,
Akaniambia tu, huo ukiisha ntakununulia Bag, mi sikuwa na mpango wa Bag, ukiisha natengeneza mwingine

Daah! Yaani nilikuwa mbunifu kweli kweli
bila shaka unatakiwa upatiwe milioni 100 [emoji23][emoji23]
 
Ila maisha ni safari ndefu sana mkuu yani mm maisha ya bata yalinishindaga utanikuta nachunga mbuzi za watu, naenda gombania ukoko wa ugali na viporo Kwa majirani wakati home mfanyakazi kashaanda chakula ila nikiziweka now day natamani bata sema ndo majukumu yashaniandama

Dah. Sisi hayo ndio yalikua maisha ya kawaida kabisa. Siku likipikwa beche hauchezi mbali. Lilikua linaitwa cheka na watoto. Kama kwenu kidogo mambo safi unalibahatisha krismas
 
Watoto wa geti kali utawajua tu. Yaani enzi hizo sie bazoka ikitemwa unaiokota unapangusa mchanga unaendeleza ku show game. Nyie tayari mlikua mnamiliki vitu vya anasa kiasi hicho?

Kwanza kijijini ndani ndani huko ukiokoteza mahindibaada ya watu kuvuna ndio unaenda kununua kandambili za bora, unazivaa jumapili tu, ukirudi unazisuuza unazisunda uvunguniiii zisije kuibiwa hapo ni hadi okesheni nyingine.
[emoji23][emoji23][emoji23] watu mmetoka mbali kweli kweli. Mimi nakumbuka nilikua narafiki yangu anapita upande wa kushoto wa barabara mimi napita kulia tunaokota vifungashio vya biskuti tunakula zile chenga za biskuti zinazobaki
 
Hivi hii mipira ya kiume inatengenezwa hapa kwetu kweli ama tunaagiza kwa kontena? Nawaza tu just in case maana sikuwahi kuisoma made in wapi..
 
Back
Top Bottom