Mi nilikuwa na akili mulize TID nilikuwa nawashikia namba class
Kama ni kweli inaelekea sasa hivi ndo umekua mjinga..
maana husema,"mwenye hekima huona haya na kujificha bali mpumbavu huenda mbele na kuvimba kichwa"
Kama ni kweli inaelekea sasa hivi ndo umekua mjinga..
Mie nilikua najua watoto wanaenda kuchukuliwa hospital.......
Miaka hiyo ya 1978 kuendelea hadi 1985 nilikuwa najua wanaovaa miwani wote ni wasomi sana tena sana, na pia mwalimu yoyote nikikutana nae amebeba mzigo lazima nimkimbilie nimsaidie na hata kwenye yale mabasi yetu ya mjini (town bus) "Shimawino" tulikuwa haturuhusiwi kukaa kwenye siti hata kama zipo wazi tunajua ni za wakubwa tuu, kweli tulikuwa gizani.
mm mpaka jana nilikuwa najua rais ni tajiri kuliko wananchi wote.
mimi nilikuwa nadhani zile picha za ukutani sebuleni wazazi walikuwa wakiniona hivyo nilikuwa naogopa kudokoa chochote kilichopo sebuleni:becky:
Nilipanda vifuatavyo nikidhani vingeota. Thumni Keki Pipi na Dagaa