sungusungu
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 3,057
- 719
Habari zenu wandugu?? Leo embu tukumbushane mambo ya zamani ambayo ulikua unatumia akili za kitoto ktk kufikiri. Basi bhana mimi zamani nilivyokua mjinga nlikua najua ukizima RADIO kama ilikua ni taarifa ya habari au matangazo ya vifo, ukija kuwasha baadae kitaendelea kilichokua kinatangazwa kabla hujaizima radio. Nlikua mjinga eh? Embu na wewe tupe kaujinga kako kazamani...
Mimi nilivyokuwa mdogo niliaminishwa kuwa wanaokula filigisi ni wakubwa peke yao tena wanaume, watoto wakila watakufa,mwanangu wa kike alikula mwaka juzi hadi leo hajafa.