Zamani nilivyokuwa Mjinga!

me nazani now ndo mjinga kuliko zamani, me nilikua natisha enzi za utoto
 
ule ulikua utoto na si ujinga.ila ulichoandika hapa ndo ujinga.,teh teh tehee!
 
Mie zamani nilipokuwa katoto nilikuwa nikisikia kuwa yule binti ni bikira nilidhani yule binti huwa na kabirika kazuri ka kuwanawisha watu wanapotaka kula ugali. Sasa naelewa kidogo ingawa hadi sasa sijaona hizo bikira, jee wewe?
 
Eti mama alikua ananiambia watoto wananunulia,kumbe dahhh
 
Ule mchezo wa kukaa barabarani then kila gari linalopita mnashindana kwa kusema hili langu nyie hamjaupitia? Mimi nilikuwa naibuka kidedea kila siku! Amakweli utoto mzigo!

Mwisho Wa huu mchezo nilijikuta nimechagua magari yenye plate number SU na mwenzangu akachagua SM. baadae nikajikuta SM zilikua nyingi kwa wakati ule basi nikawa bored saaana!
 
Mi nilifuata upinde wa mvua(rainbow) na wenzangu tukitaka kujua umetua wapi, ukiwa mbali unaona umeishia sehemu fulani,lakini ukuifika wapi. Tuligonga km kadhaa mazee,tulipochoka tukarudi home.
 
mii nilikua nikipita pale posta si kuna makatuni wamevalishwa suti wanapouza nguo kule basi nilikua nawashangaa halafu nawamkia
 
Mwisho Wa huu mchezo nilijikuta nimechagua magari yenye plate number SU na mwenzangu akachagua SM. baadae nikajikuta SM zilikua nyingi kwa wakati ule basi nikawa bored saaana!

Mm nilikuwa nachagua magari yote yenye matairi meusi! So nikajikuta magari karibu yote ni yangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…