Zamani viwanja vilikuwa unaamka asubuhi unaenda kuwahi, ila unakuta mzazi hana ardhi anayomiliki hadi sasa

Zamani viwanja vilikuwa unaamka asubuhi unaenda kuwahi, ila unakuta mzazi hana ardhi anayomiliki hadi sasa

Kama wazazi wako wangekuwa wazembe ungekuwa hai leo?

Fikiria walivyokutunza ukiwa kichanga. Wangezembea hata sisimizi wangekuua. Wanekusomesha Hadi unaweza kuandika ulichooandika.

Unavyodhani hawajafanya yafanye wewe. Sasa wamezeeka INAWEZEKANA wewe ni sababu ya wazazi wako kutonunua ardhi kibwa. Wakitimiza pesa zao kukulisha , kukuvisha , kukusomesha, kukutibisha NK. Pesa Yao ikaishia hapo.

Zaa Watoto wako uone ni rahisi kiasi gani kuwafanyia yote unavyodhani wazazi wako hawajakufanyia.

Shukuru MUNGU wamekufikisha hapo? WEWE unayedhania u smart zaidi ya wazazi wako nunua ardhi ambayo wazazi wako hawakununua.
Usiwaze Mali ya kurithi.

Najisikia aibu kubwa Sana kuwa na mtu Kama wewe Duniani.

Jifunze kufikiri vizuri. Fanya Kazi KWA bidii na Maarifa.

WEWE unaanzia walipokufikisha wazazi wako.

Nakushauri ukawaombe radhi wazazi hako hata kama hawajadoma ulichoondika.
Acha ujinga wewe wazazi wangapi wamezaa watoto kibao na wanamaeneo mengi acha kutetea ujinga hivi nyie wazee mbona hamtaki kuambiwa ukweli kwamba mlikua wajinga
 
Kama wazazi wako wangekuwa wazembe ungekuwa hai leo?

Fikiria walivyokutunza ukiwa kichanga. Wangezembea hata sisimizi wangekuua. Wanekusomesha Hadi unaweza kuandika ulichooandika.

Unavyodhani hawajafanya yafanye wewe. Sasa wamezeeka INAWEZEKANA wewe ni sababu ya wazazi wako kutonunua ardhi kibwa. Wakitimiza pesa zao kukulisha , kukuvisha , kukusomesha, kukutibisha NK. Pesa Yao ikaishia hapo.

Zaa Watoto wako uone ni rahisi kiasi gani kuwafanyia yote unavyodhani wazazi wako hawajakufanyia.

Shukuru MUNGU wamekufikisha hapo? WEWE unayedhania u smart zaidi ya wazazi wako nunua ardhi ambayo wazazi wako hawakununua.
Usiwaze Mali ya kurithi.

Najisikia aibu kubwa Sana kuwa na mtu Kama wewe Duniani.

Jifunze kufikiri vizuri. Fanya Kazi KWA bidii na Maarifa.

WEWE unaanzia walipokufikisha wazazi wako.

Nakushauri ukawaombe radhi wazazi hako hata kama hawajadoma ulichoondika.
Naona kama unataka kuchepusha mada, kwa kutoa maoni yanayoonyesha unataka kukwepa wajibu wako.
Suala la Malezi ya Mtoto ni wajibu wa Msingi kabisa kwa kila mzazi. Aidha, mtoto ana haki zote kabisa za kulelewa na wazazi wake. Endapo kama hautaki kuwajibika katika kulea mtoto basi acha kuwa na mpango wa kukileta kiumbe chochote kile hapa duniani.

Vile vile, suala la kujitafutia Mali ni wajibu na haki kwa kila mtu hapa duniani,
 
Ila kuna kaukweli fulani. Ukiwa na nguvu pambana uitafute kesho yako.
Kumsomesha mtoto ni wajibu kama mzazi anayejitambua.
Ila huu utaratibu kijana kamaliza shule, kupata kazi ya teller NMB, halafu wazazi wanataka dogo abebe majukumu yote ya familia, siyo fair. And then unakuta mzazi anayeanzisha familia umri umeenda (likely kwa mafao ya kustaafu), anafikisha miaka 75 ana watoto wa miaka kumi. Then anasukuma mzigo kwa “watoto wakubwa” ambao nao wanajitafuta bado. It’s neither fair nor right.

Tusaidiane. Lakini tusibebeshane mizigo pasipostahili.

Fanya unayoyafanya, tambua mda utafika utahitaji kulipa bills zako, wakati hakuna active employment, kama bima ya afya, nk. Yote haya lazima uyafanyie maandalizi ukiwa na nguvu.
 
Umezaliwa ukalelewa ukasomeshwa sasa unakuja kutukana hapa! Hivi hujui kuwa hii ni sawa na laana?
Kikubwa ameshayajua yote hayo kwa "upeo wake" huo alio nao. Yeye mpaka sasa amefanya nini kuhakikisha anayoyaona "makosa" ya wazazi wake hayatajirudia kwenye kizazi chake?

Hamna mtoto aliyechagua mzazi wa kumleta duniani. Itoshe kusema tu, tatizo halitatuliwi na lawama.
 
Ama umeamua kutusema, maana tumo wengi tu humu wa 1950s na 60s.

Mtoa mada nakukaribisha kwetu Dondwe ujipatie ardhi. Ekari nzima haifiki tsh20m. Isije kuwa na wewe ukasutwa kwa kukosa ardhi utakapokuwa mzee.
 
Kikubwa ameshayajua yote hayo kwa "upeo wake" huo alio nao. Yeye mpaka sasa amefanya nini kuhakikisha anayoyaona "makosa" ya wazazi wake hayatajirudia kwenye kizazi chake?

Hamna mtoto aliyechagua mzazi wa kumleta duniani. Itoshe kusema tu, tatizo halitatuliwi na lawama.
We mzee huna akili unasema hamna mzazi alieamua kumleta mtoto duniani inamaana mtoto anashushwa kutoka mbinguni anatua ardhini too halafu unaenda kumuokota
 
Kizazi cha miaka ya 1950 -1970 amabao ndo wazazi wetu walikuwa ni kizazi cha watu wazembe.

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho kimekufa na ukimwi kwa kupenda Sana ngono.

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho kinatoa vitisho vya laana .

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho hakina maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiakili.

Kizazi hiki ndo kilishikilia dini na kusahau mila za babu zetu.

Kizazi hiki ndo kizazi cha laana starehe zote kilikuwa kinaendekeza wao.

Zamani ardhi kupata ni sawa na bure Ila unakuta mzazi hana ardhi anayomiliki.
Madhara ya kuvimbiwa ndio haya. Nenda katubu , Bwana Yesu anakupenda
 
Acha kutudanganya boss. Wasemee wazazi wako, kama kizazi kizima hakikushika ardhi inamaana bado ipo, kaishike wewe. Kama haipo ujue ilishashikwa, na si watoto wa 2000 ndo wameishika.
 
Umeongea point sana Mkuu, wengi wanakimbilia Kusema wamekusomesha, wamekulea n.k kama lugha ya kutetea uzembe walioufanya kwa kuendekeza starehe na maisha ya kutaka sifa.
Kulea, kulisha, kusomesha n.k. Ni majukumu ya msingi na ya lazima kwa mzazi kwa uzao wake, haiwezekani mimi leo nibweteke nisijiwekeze kwa maisha yangu ya baadaye ili nije kuwa mzigo kwa watoto wangu eti nilitumia muda wangu kuwalea na kuwasomesha.
Ndiyo maana umasikini hauishi kwenye familia nyingi unakuta kijana ameanza kazi badala aanze kujiwekeza kwa maendeleo yake binafsi unakuta kuna lundo la ndugu na mzigo wa wazazi waliouchezea ujana wao wanataka wagawane kamshahara hako kiduchu kwa mtu anayeanza maisha.
Kijana pambana kujijenga na punguza starehe zisizo na msingi ili usiwe mzigo kwa uzao wako na kuwaongezea majukumu ambayo ulitakiwa uyafanye ukiwa na nguvu badala yake uje kuwatishia watoto kuwa utawapa laana kwa ulofa wako.
Uzi ufungwe umemaliza kila kitu,,,,,

watu kutoka bara giza wanashindwa kuelewa maswala ya malezi, kuzaa na kusomesha sio HISANI ni MAJUKUMU ikiwa umeamua kuleta kiumbe hapa duniani yamkini kama huwezi hayo majukumu ni bora mtu abaki bila watoto maana saiv kuna maskini wengi wanatuletea vibaka na majambazi vile wanazaa hovyo kwa imani zao potofu ya kuijaza dunia. Hivi makapuku na maskini wakiijaza dunia hii wanazani hii dunia itakalika😂😂😂😂
 
Kizazi cha miaka ya 1950 -1970 amabao ndo wazazi wetu walikuwa ni kizazi cha watu wazembe.

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho kimekufa na ukimwi kwa kupenda Sana ngono.

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho kinatoa vitisho vya laana .

Kizazi hiki ndo kizazi ambacho hakina maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiakili.

Kizazi hiki ndo kilishikilia dini na kusahau mila za babu zetu.

Kizazi hiki ndo kizazi cha laana starehe zote kilikuwa kinaendekeza wao.

Zamani ardhi kupata ni sawa na bure Ila unakuta mzazi hana ardhi anayomiliki.

Kwanini wewe usiende Handeni na wilaya nyingine za kusini huko kushika mashamba? kule ni bure kabisa au pengine unaweza kupata hekari kwa shs 50,000; tofauti na hapo na wewe miaka 30 ijayo utalaumiwa kama unavyo laumu wazee wako!
Kwa taarifa yako miaka hiyo kulikuwa na umasikini wa kupindukia hata hizo starehe unazosema; sijui masikini wa kupindukia ambaye hana Elimu kama wewe, kula na kuvaa kwake kwa taabu atazifanyaje???
 
Kizazi kilicho pita (unacho kisema) na hiki hakuna utofauti wowote, nasisi tusubilie kuja kutwikwa lawama za namna hii.
Mimi sasa hivi niko kwenye 20's nikija kufika 40's sina mashamba, viwanja na nyumba kadhaa. Watoto wakojolee kaburi langu

Kizazi hiki changu na chenu kukosa mali ni uzembe wa hali ya juu
 
Umeongea point sana Mkuu, wengi wanakimbilia Kusema wamekusomesha, wamekulea n.k kama lugha ya kutetea uzembe walioufanya kwa kuendekeza starehe na maisha ya kutaka sifa.
Kulea, kulisha, kusomesha n.k. Ni majukumu ya msingi na ya lazima kwa mzazi kwa uzao wake, haiwezekani mimi leo nibweteke nisijiwekeze kwa maisha yangu ya baadaye ili nije kuwa mzigo kwa watoto wangu eti nilitumia muda wangu kuwalea na kuwasomesha.
Ndiyo maana umasikini hauishi kwenye familia nyingi unakuta kijana ameanza kazi badala aanze kujiwekeza kwa maendeleo yake binafsi unakuta kuna lundo la ndugu na mzigo wa wazazi waliouchezea ujana wao wanataka wagawane kamshahara hako kiduchu kwa mtu anayeanza maisha.
Kijana pambana kujijenga na punguza starehe zisizo na msingi ili usiwe mzigo kwa uzao wako na kuwaongezea majukumu ambayo ulitakiwa uyafanye ukiwa na nguvu badala yake uje kuwatishia watoto kuwa utawapa laana kwa ulofa wako.
Sasa kama mtu hataki kuwa na ardhi je
 
Uzembe wa mzazi wako usimtwishe mzazi wangu, uzembe wa babu yako usimtwishe babu yangu. Sema baba yako na babu yako walikuwa wazembe wapenda ngono na anasa alah! Kila mtu anapambana kulingana na upeo wake.
Na ww hapo unaweza kuona unafanya mengi mazuri ili kuandaa kesho nzuri kwa familia ako lakini itakapofika muda huo wanao wakakuona mzembe na hukuwa na mipango.
 
Back
Top Bottom