Zamani viwanja vilikuwa unaamka asubuhi unaenda kuwahi, ila unakuta mzazi hana ardhi anayomiliki hadi sasa

Umemaliza?
Mkaa laana mkubwa wewe.
 
Acha lawama na dhihaka kwa wazee wako kijana.
 
wewe unamiliki nini, kwani kizazi hiki kimefungiwa? kufanya hayo hapo juu
 
Sasa kama mtu hataki kuwa na ardhi je
azizae maana huyo hana cha kurithisha,,,,ukizaa mtoto atarithi mpaka akili. Sasa kuliko kutuletea majobless na watu wasio faida kama huyo mzazi asiyependa kumilki mali ya uzalishaji na asiye na akili ya kufikiri kwa mapana kuwa aridhi ni dhana ya msingi ya uzalishaji ni bora uzao huo usiwepo kabisa!!!
 
Kwangu Mimi kuwalaumu wazazi wangu ni halali kabisa,maana sikuwaomba wanizae,hata Mimi natoa ruhusa ya wanangu kunilaumu pale watakapoona nilishindwa kutimiza majukumu yangu.


Pongezi zimfikie babu kizaa baba,huko aliko apate rehema,alionao mbali sana
 
Hakika u kizazi cha laana!
Umefikia hatua ya kutukan wazazi walokuzaa na kukulea.
ULAANIWE!
 
HAKIKA UMEPOTOKA!
JIFUNZE KUONA MAZURI KWENYE KILA JAMBO, HATA KWA TOCHI ITAKUSAIDIA SANA
 
kwani mzazi wako kutomiliki ardhi wewe inakuhusu nini chief ? Kwanini usitafute ya kwako? Mambo gani kuanza kupangiana? Unajua miaka kadhaa mbele mtoto wako atakuja kuandika kwamba kizazi chako ni cha hovyo kwa sababu hauna rolls royce?

N.b
Pole sana kama bado una mentality ya kungojea mirathi utakuwa umefeli pakubwa mno.
 
Shukuru kama wewe umejaliwa hivyo, hata enzi za manabii na mitume wapo ambao hawakuwa na ardhi. Wapo waliotamani vya masikini, na kutwaa kwa nguvu na hila. Hakikisha hata wewe uliejaliwa usidhulumu!
 
Uzi huu unaonyesha ni kwa jinsi gani bado watu hawakotayari na bado wnaufahamu mdogo wa kuongelea kweli na kuikubali kweli hiyo😂😂😂😂😂watu wanatokwa na mapovu yamkini hawa ndo wanaosemwa na mtoa uzi. Kuzaa sio lazima na hakuna mtoto alikuomba umzae ni aidha ashki zako au ulimbukeni wako wanadunia wakakuingiza kingi ati kuzaa ni baraka na unazaa ili watoto waje wakulee😂😂😂 ukifata hii dhana lazima ubaki kutisha LAANA uchwara( dhana/imani potofu ya watu wa kale waliokuwa hawapendi kuambiwa ukweli na wale wadogo kwao).
 
nimesikitika sana,...kwa hizi nondo ulizoshusha umeshindwa hata kumalizia neno ,.(PUMBAVU ZAO)..🙄
 
Kiukweli wazee wa karba hiyo inatakiwa kupigwa viboko kabisa ni Hawa wanajua kuhoji mishahara ya watoto wao ili wajue wanaanza kukupigaje .
😂🤣🤣 nina uhakika hawa wazee wanaokufa kwa mshtuko wa moyo,.. sababu ni majibu ya watoto wao,...mzee anakutana na jibu ambalo hakuwai tegemea kusikia kutoka mtoto wake,...
 
Sasa hivi wewe ndio mzazi, type mafanikio, au ndio unakesha kwa Mwamposa, au unakesha baa wakati kisarawe kuna maelfu ya hekari hayajalimwa, unaoga maji kwa sabani ambayo umeitumia kumsafisha kinyesi katika mikono yako
 
hata sasa hivi kuna sehemu ukiwa na elfu 30 unapata acre moja, kuna siku siku wajukuu zako watashangaa kwanini babu hakununua acres 100
Mkoa gani huo mkuu?? Maana hata kwetu Iringa nimeenda hivi karibuni bila 300000 hupati hata eka wakati enzi zangu najitafuta eka ilikuwa 50,000 to 100000
 
kutetea uzembe
Sio wote walikuwa wazembe. Mfano mikoa mingi ilikuwa haina miundombinu ya kusafirisha bidhaa hivyo hata ulime vipi utakula mwenyewe. Watu hawakuwa wengi sana kama sasa chochote unaweza kuuuza.
Chama tawala ccm kiliwadumaza.
Kumbuka hata sasa chama tawala kinadumaza mambo mengi ambayo yatakuwa lawama kwa wote huko mbeleni.
Wazee wetu walidanganywa sana na kundi la wasomi, hawakuwa wakipima maendeleo yao binafsi hivyo walikiamini chama na viongizi hata kama hawaleti maendeleo.
Wazee wetu walijengwa ktk falsafa ya ujamaa. Hawakuamini ktk kumiliki mali nyingi, hivyo kumiliki ardhi haikuwa ishu.
Wazee wetu hawakuwa na hamasa kama sasa.
Hata sasa kuna ardhi ila sio kila mtu anaweza kuimiliki au kuinunua. Kuna watu wanamiliki ardhi ila mitaji hawana.
 
Hadi sasa ardhi iko nyingi nchi hii, Anza wewe kutafuta ardhi uokoe kizazi chako, acha lawama, generation yao imeshapita
 
wewe una ardhi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…