Zamaradi acha kumfananisha Billgate na Mtoto wa Kajala, Unampotosha

Nilisoma aliyoandika nikapita kimya kimya nilijisemea kama washauri ndio wanaandika hivi.. bila hata kujifikiria.. kisa kusaka kiki mitandaoni.. basi nchi yetu ina mengi bado ya kusaidia wananchi kama huyo mwandishi..

Atakuambia yeye alisoma hadi chuo na ndio ameandika hayo..
 
Robo tatu ya Watanzania ni Wachawi.
 
Kina zamaradi ni jamii ya wale watu watakwambia Bakhressa alikuwa shoe shiner. Wanatakiwa wamueleze ukweli kuwa Bill gate Ali drop out kwa sababu alikuwa anajua zaidi ya walimu wake ,akaamua atumie uwezo aliokuwa nao kutengeneza pesa haku drop out kwa sababu alifeli .
 
Bill Gate hakuwahi kufeli. Tangu utoto wake alikuwa Na kipaji cha juu katika kudadisi masuala ya computer, tena sio jinsi ya kuitumia, bali ni jinsi inavyofanya kazi.
Mtihani wa kumaliza shule, SAT, alipata alama 1590 kati ya 1600.
Na kuchukuliwa katika chuo kikuu maarufu cha Harvard kutokana na kufanya vizuri madarasa ya chini.
Ila aliamua kuacha na kuendelea kipaji chake cha mambo ya computer, sio kwamba alifeli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inasikitisha sana...

Binti kafeli kwa ujinga na mambo yake mwenyewe leo mje kumpa false hopes...

Alafu Billgates haku drop off form 4, ali drop off Harvard University kuna utofauti mkubwa sana...


Cc: mahondaw
 
Tatizo wabongo wengi tunadanganyana upuuzi. Billgate hakuwai kufeli sehemu yoyote katika elimu yake in short he was the best mpaka akafika havard. He is a dropout and not a failure same to mark and many more. Hawa watu elimu haikuwai kuwashinda bali wao walikuwa na akili nyingi na hawakuona umuhimu wa kuendelea kusoma kwa kipind hiko.
Tupeane moyo lakini tusitoe mifano ya uongo ili kuwapa moyo. Kufeli shule sio kufeli maisha coz elimu ya darasani ni njia moja tu ya kufikia mafanikio bado ana nafasi kibao tu za kutoboa.

Lakini kunfananisha genious billgates na mark na hao ngumbaru wa mtaani wanaopata div zero ni kuwashushia heshima hawa magenious

Nawasilisha


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Waambie walahi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bill Gates alikuwa na akili za darasani pia, ila kilichokuwa kinafundishwa sio kilichomvutia. Na ndio hapo inapoaelezwa huyo binti asifananishwe na huyo tajiri. Katika huo umri alio nao huyu binti, tayari Bill alishajipambanua na kutambuliwa uwezo wake usio wa kawaida katika mambo ya computer. Binti ana nini mpaka sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zamaradi kushney walahi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanachanganya sana matukio, Bill Gates alikuwa genius aliandika program za computer ambazo hata professor wake hakuwa na idea nazo kwa kipindi hiko, hata Albert Einstein ambaye naye alikuwa kilaza darasani na alikuwa slow kuelewa masomo anayofundishwa naye alikuwa genius, so kutofanikiwa kwa hawa jamaa kwenye madarasa yao ya awali hakufanani na matukio ya wanafunzi wetu, wa kwetu wanafeli kwa kuwa ni pure vilaza, hawataki kusoma, hawana ambition wala ubunifu, akina gates walikuwa wanaacha masomo wakafanye project zao wakazifanikishe, sasa muulize mtoto huyo aliyefeli alikuwa anatumia muda wake kwenye project gani zilizokuwa zinammalizia muda hamna, ni pure kilaza, tuache kuwapa matumaini ya kijinga, wasome waache ufala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pili zamaradi uache kuandika magazeti ambayo hayana kichwa wala mguu, Billget hakufeli kizembe zembe, alifika hadi chuo kikuu bora zaidi duniani, pia uwakanye hawa mabinti wa skuizi

Acheni kuwalisha watu matango pori; kama hamna uhakika wa habari kaeni kimya. Bill Gates hakufeli alipokuwa Havard University bali aliamua kuacha na kwenda kufanya mambo aliyodhani yalikuwa ya faida kwake wakati ule badala ya kuendelea na chuo kwani aliona angepoteza muda wake bila manufaa!

Sasa nyie watoto wenu wanafeli mnawadanganya kuwa hata tajiri mkuu duniani pia aliferi tena form four exams kwahiyo wajipe moyo!!
 
Leo nimesoma mara moja na kukuelewa!!

umeandika mwenyewe,umeandikiwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…