Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

Huwezi kumpangia Mungu kazi yake, hivi mpaka leo ingekuwa kanisa 1 tu watu wangemjua Mungu kweli kama dar kanisa liwepo kule tu kwa Baba Pengo hivi tutakuwa na akili kweli ? Mitume wenyewe baada ya Yesu kufa kufufuka na kupaa na wao walisambaa kwakuhubili injili, Petro alifia Roma huko
Hilo Jamaa hata si mkristo bali ni Shetwani aliyejivisha ukristo ilimradi tu aupambanie udini wake.

Mkristo gani anasikitika Makanisa kuwa mengi?
 
Sinagogi ni nyumba ya ibada ya wayahudi tafuta historia au elimu ya dini utagundua kuwa uyahudi ni dini iliyokuapo zamani

Pia mahekalu yalikuwapo kipindi cha Kristo....



Soma,,,,,

—Yohana 18:20.

" Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na katika hekalu, ambapo Wayahudi wote hukusanyika.”
Kanisa lilizaliwa pale Yesu aliposulibiwa, ndiyo maana katika kitabu cha Matendo imeandikwa wakakusanyika na kanisa, na kanisa ni kusanyiko takatifu
 
Unasema kabla ya Yesu walikuwa na dini gani? Walikuwa wanamwabudu Mungu aliye hai pia wapo waliokuwa wanaabudu miungu
Mungu yupi sasa na Yesu ndy Mungu?
Au hapakuwa na Mungu?

Lazima ieleweke kwamba dini ilikuwapo kabla ya Yesu kuja.

Je ilikuwa dini gn?
Hilo lifanyiwe kazi.
 
Hilo Jamaa hata si mkristo bali ni Shetwani aliyejivisha ukristo ilimradi tu aupambanie udini wake.

Mkristo gani anasikitika Makanisa kuwa mengi?
Injili itahubiliwa tu mpaka upenuni mwa nyumba, na kila goti litapigwa na ulimi utakiri kuwa KRISTO ni BWANA na mwokozi. Hakuna wakuzuia maji kwa mikono.
 
Yesu alipokuja alikuwa ana abudu kwenye masinagogi ambayo ni misikiti ya wayahudu, nayeye Yesu akiwa ni myahudi, na kuitangua si kuibadilisha la bali kulitimiliza neno lake ambayo utalipata Yohana 1:1-5, na ndiyo maana manabii wakale waliandika habari zake kwamba atazaliwa Masihi, hivyo yeye ndiye njia ya kweli na uzima mtu haendi kwa Baba bila ya yeye, hivyo injili itahubiliwa tu hakuna wakuizuia kamwe.
Aliposema hakuja kutengua torati maana yake hakuja kutengua Yale yaliyokuwapo kabla yake.

Je hao akina Moses(mussa) walikuwa dini gn?

Hyo ndy dini ya kweli..
 
Mungu yupi sasa na Yesu ndy Mungu?
Au hapakuwa na Mungu?

Lazima ieleweke kwamba dini ilikuwapo kabla ya Yesu kuja.

Je ilikuwa dini gn?
Hilo lifanyiwe kazi.
Kaanze kusoma kitabu cha mwanzo angalau anzia Mwanzo 12: utaona Mungu alivyokuwa anasema na watu,
 
Aliposema hakuja kutengua torati maana yake hakuja kutengua Yale yaliyokuwapo kabla yake.

Je hao akina Moses(mussa) walikuwa dini gn?

Hyo ndy dini ya kweli..
Halafu nawewe wapi Agano la kale wameandika dini? Wale walikuwa wanapewa maagizo moja kwa moja ukikosea Mungu anakulamba kichwa sahizi fanya dhambi Mungu anakusubilia tu.
 
Halafu nawewe wapi Agano la kale wameandika dini? Wale walikuwa wanapewa maagizo moja kwa moja ukikosea Mungu anakulamba kichwa sahizi fanya dhambi Mungu anakusubilia tu.
Kwahyo hawakuwa na dini?
 
Niliiona jana hii habari, sema Wahusika wametulia kwa sababu wanajua walichokuwa wakifanya sio sahihi

Huwezi ukaejenga makanisa na kwenye makazi ya watu na kuwapigia kelele usiku kucha kwa miujiza ya kitapeli

Zanzibar hawapendi ujinga
Yapo makanisa kama Katoliki ambayo tunaheshimu na kuishi nao kwa amani, ila haya makanisa ya kijasiriamali yaliyojaa utapeli hayawezi kuvumilika.

Hakuna uhuru wa kuabudu usio na miaka, ndio maana hata serikali ilimfungia Nabii Tito pia imefungia Zumaridi
Ila nyie huku bara mnajenga kila sehemu na asubuh mnatupigia kelele zenu na kutukera lakini tunavumila tu. Wakristo mfike mahala mbomoe hizo nyumba za hao wanaoamini kwenye majini wazuri na wabaya.
 
Niliiona jana hii habari, sema Wahusika wametulia kwa sababu wanajua walichokuwa wakifanya sio sahihi

Huwezi ukaejenga makanisa na kwenye makazi ya watu na kuwapigia kelele usiku kucha kwa miujiza ya kitapeli

Zanzibar hawapendi ujinga
Yapo makanisa kama Katoliki ambayo tunaheshimu na kuishi nao kwa amani, ila haya makanisa ya kijasiriamali yaliyojaa utapeli hayawezi kuvumilika.

Hakuna uhuru wa kuabudu usio na miaka, ndio maana hata serikali ilimfungia Nabii Tito pia imefungia Zumaridi
Mpumbavu wewe nyie mnavotupigishia kelele na ving'ora vyenu asubuhi mnahubiria mtaa mzima
Watu wengine hovyo kweli. Na usikute eneo hilo hilo watu wanafungulia mziki mkubwa mpaka kero, unakuta eneo hilo hilo kuna disco na maclub ya ujinga. TAG ni kanisa la kiroho sio manabii matapeli
 
Mpumbavu wewe nyie mnavotupigishia kelele na ving'ora vyenu asubuhi mnahubiria mtaa mzima
Watu wengine hovyo kweli. Na usikute eneo hilo hilo watu wanafungulia mziki mkubwa mpaka kero, unakuta eneo hilo hilo kuna disco na maclub ya ujinga. TAG ni kanisa la kiroho sio manabii matapeli
Hapo hapo mtu akiweka kiringe chake utasikia tunaenda kwa mtaalamu ambaye hata kusoma hajui, ila kanisa kelele, ila wakipiga muziki mtu anakoroma mpaka mwisho ila injili kelele duu
 
Kaanze kusoma kitabu cha mwanzo angalau anzia Mwanzo 12: utaona Mungu alivyokuwa anasema na watu,
Nataka ufahamu kwamba dini ya Mungu ilikuwapo kabla ya Yesu.

Je walikuwa wanaabudu Mungu kwa dini ipi?
 
TAG taifa tunategemea askofu atoe tamko la kulaani hata la mdomo tu. pamoja na kwamba, hadi hapo wameshapata ujumbe, kungúteni tu mavumbi ya viatu vyenu mkajenge sehemu nyingine. siku hizi injili inafikiwa kwa nman ambalimbali hadi china wanapata kwa mtandao, hivyo wasifikiri watakwepa kumsikia Yesu Mtenda miujiza. watamsikia sana na siku ya mwisho hawatakuwa na cha kujitetea. hayo magreda yalivyovunja jengo yatawashuhudia.
 
Wewe kiongozi.

Mimi nimekaa nao Saudia.
Wakristo wapo.

Wacha kushupaza shingo..

Hivi unajuwa kama wamarekani wapo Saud Arabia maelfu?
.umewahi kujiuliza wanasali wapi?

Nilichokigunduwa Mimi kutokana na experience yng ya kukaa Saudia.

Sisi waafrika tulioisikia dini tunajifanya tunajuwa dini ya kiislam na uchungu nayo .
Kuliko wale wenyeww wenye asili nayo.

Ukiwaona hata hao waarabu wasaudia wanavyo swali.

Nina uhakika swala za waafrica wote ni peponi moja kwa moja.

Usiongee vitu huvijuwi.
Ni mpaka miaka mitatu iliyopita, Prince Mohamad Bin Salman alipojiamulia kuwe na kanisa lijengwe huko Saudi, uhuru uko wapu hapa mpaka huyo prince aamue.
 
Saudia Arabia wakristo wapo.
Ila ni ngumu kuwakuta miji hii mikubwa MAKA NA MADINA
 
Niliiona jana hii habari, sema Wahusika wametulia kwa sababu wanajua walichokuwa wakifanya sio sahihi

Huwezi ukaejenga makanisa na kwenye makazi ya watu na kuwapigia kelele usiku kucha kwa miujiza ya kitapeli

Zanzibar hawapendi ujinga
Yapo makanisa kama Katoliki ambayo tunaheshimu na kuishi nao kwa amani, ila haya makanisa ya kijasiriamali yaliyojaa utapeli hayawezi kuvumilika.

Hakuna uhuru wa kuabudu usio na miaka, ndio maana hata serikali ilimfungia Nabii Tito pia imefungia Zumaridi
Yule padri mliemmwagia tindikali alikua mpentekoste?
Mbona unahalalisha haramu Kua halali?
 
Mm Ni mkiristo sioni sababu huyo mtumishi kwenda kufanya ujenzi ktk maeneo ya wanao ishi waislmu yaani unakwenda uarabuni kufungua kanisa hapan aise. usijaribu Imani za watu haondoke Hapo kbsa Tena ashukuru ajapigwa kipigo kikali mnk hvyo yey ndie mchokozi ..watu wasitafute usaw wa kidini hapa
Kenya umewahi sikia muslami kaw rais au hata kiongoz mkuu hkn hvyo vitu sas na huku iwe Hvyo uwez kwenda kufanya ibada Zanzibar Tena siku hz wamestarabika zamani waliwamwagia tindikali .....
Unatushauri na Sisi tuanze kuchoma misikiti iliyopo kwenye makazi Yetu?
 
Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo wakishinikiza kuwa hawataki Kanisa katika eneo lao.

Hii ni kunyume kabisa na sheria za nchi zinazoruhusu Uhuru wa Kuabudu. Kama jambo halitafanyika basi ni wazi kuna kiongozi mbaguzi wa dini anaewalinda wabomoaji na pia hii itachochea sehemu nyingine makanisa na makazi ya wachungaji kubomolewa.

Pia miezi michache ijayo kipindi cha mfungo kikianza huwa ni marufuku kwa wakristo kula sehemu za wazi, ukikutwa unafungwa mpaka mfungo uishe, wengine huwa wanapigwa sana, sasa hapa ni kwamba mtu kama umeamua kufunga kwa imani yako iwaje hutaki kuona wenzako hawali, ni kwamba imani yako no nyepesi sana kuisimamia, kama ni hivyo kuna haja gani ya kufunga.

View attachment 2146530

View attachment 2146523

============================================

Taarifa uhakika juu ya tukio hilo ni kuwa Mchungaji David Victor Suna ni mzaliwa wa Sumbawanga, lakini kwa miaka mingi amekuwa akiishi Zanzibar baada ya familia yake kuhamia huko. Kaka yake naye ni mtu wa kanisani lakini anafanya shughuli zake Dar es Salaam.

Alipoanza harakati za kutafuta eneo kwa ajili ya kanisa alipata wakati mgumu kwa kuwa walikuwa wanamkatalia, baadaye akabadili gia na kutafuta eneo la kununua la kwake binafsi na siyo kwa ajili ya kanisa.

Baada ya kutafuta eneo lake binafsi ndipo akapata eneo hilo lililopo Sebleni, Unguja. Akanunua kwa Sh 16,000,000 (milioni 16) akalipa fedha taslimu, akasaini mkataba rasmi wa mauziano (tazama picha), japokuwa katika eneo hilo alikuta mmiliki tayari amejenga banda ambalo nalo lilikuwa sehemu ya mkataba wa manunuzi.

Baada ya kununua akajenga ukuta kuzungushia eneo husika kisha akaanza shughuli zake za ibada, baada ya majirani kubaini kuwa mnunuzi ameanzisha kanisa eneo hilo ndipo mgogoro ulipoanzia.

Wakamwabia hatakiwi kuwa na kanisa eneo husika lakini David Victor Suna akashikilia msimamo wake kuwa ataendelea na shughuli zake za kanisa.

Mhusika ambaye aliuza eneo hilo naye akamvaa David Victor Suna na kumtaka arejeshe eneo hilo kwa kuwa hakuuza kwa ajili ya kanisa bali kwa ajili ya kujenga makazi, bado David Victor Suna akagoma kubadilisha matumizi wala kurudisha eneo.

David Victor Suna akawa asisistiza kuwa yeyote mwenye malalamiko aende Mahakamani ambapo haki itatendeka, hata waliposhirikisha Serikali za mtaa nao wakawa wanamshawishi ama kubadili matumizi au kurejesha eneo, msimamo ukawa ni uleule.

Ndipo siku ya tukio, lilikuka bulldoza likaanza kuvunja eneo husika wakati wahusika wakiwepo wachache wakiendelea na ibada kama kawaida, kanisa likavunjwa na baadhi ya vitu vikiwemo viti vikaharibiwa na gari hilo.

Mamlaka za Serikali za mtaa hazijawa tayari kuzungumzia tukio hilo, naye David Victor Suna amekuwa mgumu kuzungumzia kinachoendelea kwa kile kinachodaiwa hajatulia hadi sasa.

SERIKALI YAINGILIA
Taarifa zinaelezwa kuwa Mkuu wa Wilaya wa eneo husika anatarajiwa kutolea ufafanuzi suala hilo mchana wa leo Machi 11, 2022.

Nitarudi kuwapa kilichoendelea kuhusu tamko la Serikali.

ITAENDELEA...
View attachment 2146667
View attachment 2146668
View attachment 2146670
View attachment 2146671 View attachment 2146672
Minaamin Zanzibar iwe nchi ni mzigo kwa Tanganyika sijui kwanin inanganganiwa iwe nchi wapemba wote wa kariakoo warudishwe kwa lazima
 
Back
Top Bottom