Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Mchezo huu hauhitaji hasira, mtu ni kwao, karibu sana Sultan Jamshid.

TOKA MAKTABA:
AIISHUKURU SERIKALI YA TANGANYIKA KWA KUMPA NJIA YA KUPITA KUELEKEA UGAIBUNI

Karibu sana nyumbani.

Hapa clip fupi akitoa shukrani kwa serikali ya Uingereza kumpatia hifadhi na pia serikali ya Tanganyika kwa kumpa ruhusa kupita Dar es Salaam baada ya mapinduzi ili afanye taratibu za kwenda Uhamishoni


View: https://m.youtube.com/watch?v=TKE2C5svBLo

Maafisa nchini Kenya walifikiri kwamba kuingia kwa Sultan Mombasa kunaweza kusababisha hali tete ya usalama na misukosuko ya Waarabu wanaoishi Mombasa; hivyo, iliamuliwa kutompa kimbilio, wala kwa wasaidizi wake; badala yake, iliamuliwa waelekee Dar es-salaam.

Jijini Dar es-Salaam, Sultani na msafara wake waliwekwa katika kizuizi cha nyumbani katika nyumba mbili za serikali zinazolindwa na polisi na ziko katika eneo la kifahari la Oyster Bay.

Nyumba moja ilitengwa kwa HM. Sultani na familia yake huku wa pili akikalisha wasaidizi wake. Walikaa Dar es Salaam kuanzia tarehe 13 hadi 18 Januari 1964, siku ambayo walisafiri kwa ndege kuelekea Uingereza
 
View attachment 3186808

Mnamo Januari 9, 2025, Zanzibar itashuhudia tukio la kihistoria itakapompokea Sultan Jamshid bin Abdullah kurejea kwenye pwani zake. Hili ni tukio muhimu sana kihistoria, kwani mtawala wa zamani wa Zanzibar anarudi baada ya miongo sita ya uhamisho nchini Uingereza na Oman, kufuatia kuondolewa kwake madarakani wakati wa mapinduzi ya 1964.

Cc Pascal Mayalla

Maelezo kuhusu jinsi ziara hii ilivyopangwa bado hayajafahamika, lakini umuhimu wake hauwezi kupuuzwa. Kurudi kwa Sultan Jamshid kunawakilisha ishara ya upatanisho wa kipekee kutoka kwa serikali ya Zanzibar. Ziara yake inaweza kuwa daraja kati ya enzi za kabla na baada ya mapinduzi, ikichochea mshikamano na uponyaji wa kitaifa.

Zanzibar inaweza kuchukua nafasi hii kumwalika Sultan kuishi katika mojawapo ya majumba yake ya zamani kama raia wa kawaida. Hatua kama hiyo haitaimarisha tu taswira ya Zanzibar kimataifa bali pia inaweza kuinua sekta yake ya utalii, kwani uwepo wake utavutia shauku kubwa. Zaidi ya hayo, inaweza kuashiria sura mpya ya upatanisho kati ya Sultan na serikali ya mapinduzi, ikitoa mfano wa maendeleo na mshikamano.

Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.
Dah. Hatimaye watu wazima wamepata ujasiri wa kukabiliana na nuru (light) baada ya kujificha gizani miaka 60.

We can easily forgive a child for being afraid of the dark but the real tragedy of life is when men become afraid of the light - Plato

Ukweli hupanda ngazi na, hakika, utafika.
 
Picha Sultani alipofika na kuteremka bandarini Dar es Salaam kukimbia Mapinduzi ya 1964 Zanzibar

1735388839931.jpeg
 
Sasa mapinduzi yatakaaje waungwana, je atatmbulishwa kama Sultani Jamshid au kama Bw. Jamshid?

Wataalamu muongozo wenu muhimu hapa.
Hawakawii kusema wakoloni walikuwa wazungu sio waarabu😂😂😂🤣🤣 maana hao wazenji wametekwa na waarabu hao,mpaka sasa huwa wanasema waarabu ni ndugu zao🤣🤣🤣
 
sultan sio mwanasiasa ujio wake hauna uhusiano na mambo yenu ya kisiasa akifika ataenda msikitini kuswali badae anaenda nyumbani kwake
Kwa hiyo huyu Sultan Freeman ni sultan uchwara!
 
Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.
Waingereza siyo wajinga wa muhifadhi huyu ndugu miaka yote hiyo bure! Tena nchini mwao. Kikubwa tujue Waingereza wametuandalia nini ili tuwe tayari kulipokea hicho kilichoandalawi!

Karibu sana "Sultan" Jamshid bin Abdullah!!
 
View attachment 3186808

Mnamo Januari 9, 2025, Zanzibar itashuhudia tukio la kihistoria itakapompokea Sultan Jamshid bin Abdullah kurejea kwenye pwani zake. Hili ni tukio muhimu sana kihistoria, kwani mtawala wa zamani wa Zanzibar anarudi baada ya miongo sita ya uhamisho nchini Uingereza na Oman, kufuatia kuondolewa kwake madarakani wakati wa mapinduzi ya 1964.

Cc Pascal Mayalla

Maelezo kuhusu jinsi ziara hii ilivyopangwa bado hayajafahamika, lakini umuhimu wake hauwezi kupuuzwa. Kurudi kwa Sultan Jamshid kunawakilisha ishara ya upatanisho wa kipekee kutoka kwa serikali ya Zanzibar. Ziara yake inaweza kuwa daraja kati ya enzi za kabla na baada ya mapinduzi, ikichochea mshikamano na uponyaji wa kitaifa.

Zanzibar inaweza kuchukua nafasi hii kumwalika Sultan kuishi katika mojawapo ya majumba yake ya zamani kama raia wa kawaida. Hatua kama hiyo haitaimarisha tu taswira ya Zanzibar kimataifa bali pia inaweza kuinua sekta yake ya utalii, kwani uwepo wake utavutia shauku kubwa. Zaidi ya hayo, inaweza kuashiria sura mpya ya upatanisho kati ya Sultan na serikali ya mapinduzi, ikitoa mfano wa maendeleo na mshikamano.

Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.
taarifa hii ya kurejea Sultan isije kuwa ni fake story,kwasababu nime cross check na Msemaji wa SMZ, Charles Hillary, wao hawana taarifa za ugeni huu, labda kama anakuja Zanzibar on a private visit kama mtalii tuu, then hahitaji kutoa taarifa popote bali kugongewa tuu visa na kuingia Zanzibar。

P
 
Yaani ulivyandika kwa Shauku na kujikweza😀😀😀😀

Hakika MTUMWA NI MTUMWA tu, babu zako wamatumbi na wamwera huko waliko wanakunja mafuvu yao na kujipigiza kwenye kuta za makaburi kwa gadhabu baada ya kuona huu uzi wako.

Hivi wazanzibari wnajua historia yao vizuri yaani wanajisahaulisha wao ni kizazi cha kitumwa tena watumwa sio kutoka OMAN ila kutoka Tanganyika ila wanaona Waoman waliotesa babu zao ni watu wa maana sana na wao wanajiona waomani🤣🤣🤣🤣

Ukienda Uarabuni mwafrica ni katika kiumbe daraja la chini sana tena ambaye unaruhusiwa kumiliki kama mali. Lakini waarabu hawa wa kubabatiza huku africa wanavyowahusudu waarabu orijinal sasa🤗🤗🤗

Anyway, kupanga ni kuchagua!!!
Unaweza mtoa nyani porini lakini huwezi litoa pori kwenye kichwa Cha nyani
 
Tunamtaka Richard Turnbull Tanganyika ili tusameheane naye pia😒
Nilitarajia utawauliza CCM enzi za Maalim Seif CUF, hoja yao kubwa ya kampeni ilikuwa kudai hatari ya hao Hizbu (CUF) kurejesha utawala wa sultani na waarabu Zanzibar.

Kelele zao zilikuwa dhidi ya “machotara wa Hizbu” (CUF) kumrejesha sultani huko Zanzibar!

Leo wanataka maridhiano na Sultani? Good. Inasemwa ukweli hupanda ngazi. Nasubiri ukweli utakapofika kauli ya mwisho itakuwaje.

Hii nchi tumeishi kwa uongo miaka yote. Mengi yatawekwa sawa muda muafaka ukifika.
 
Hii mifumo ya kimaisha na shule zenu inalemaza sana watu akili.
Just imagine, Okello ametoka huko Kijijini kwao, tena miaka hiyo, akaenda Kampala, akajifunza mambo kadhaa, akaamua kwenda Zanzibar akiwa na miaka 22 akaenda kuwasaidia kupambana na Sultan hadi kumuondoa. Akakabidhi madaraka kwa raia wa pale, then akafukuzwa.
Leo kijana gani katika umri huo anaweza akafanya hayo.

Ila Iddi Amin alikuwa mtu mzuri sema makosa yake yalikuwa ni 'deadly/grave'. Okello alitengwa na akateseka sana nchini Uganda kiasi cha kukosa hata hela ya kula, akalazimika kurudi kijijini. Iddi Amin alipoingia alimfuata Okello na kumuahidi uwaziri ili waiongoze Uganda, lakini Okello akachomoa, Iddi Amin hakukata tamaa, akamuahidi umakamo wa rais, lakini Okelleo akachomoa, akabembelezwa sana, akakubali kwa masharti apewe urais, Iddi Ammin ndiye awe Makamo...hapo ndiyo story ilipoanzia na kuishia
Leta source ya story yako kati ya Iddi Amin na Okello
 
Back
Top Bottom