Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Suala si ninyi kuwa ndugu, bali ni inferiority complex yenu kwa waarabu.
Waarabu wamewadominate kwenye kila angle ya maisha.
  • Hapa mnatamani warudi kuwatawala hapo Zanzibar, lakini wao hawawezi kuwaruhusu mkawatawala na wanawabagua weusi wote, uwe muislamu au la.
  • Mnaitwa majina yao, mnafuata imani na matendo yao, meanwhile, hamna chenu wanachofuata.
Kiufupi, waarabu ni superior race kwa waislamu wote wa Zanzibar na Tanganyika, na ninyi wabantu mmesalia kwenye nafasi ya utumwa.
Mkuu suala la dini usiliunderlate ukweli utabaki kuwa wakiristo watazidi kuwaona wazungu kama ndugu zao kwa kuwaletea dini ya kikiristo bila wao leo hii tusingekuwa na akina john na peter hapa kwetu tz

Vilevile waislam watazidi kuwaona waarabu ndugu zao na watu waliowaletea dini ya kiislaam bila wao tusingekuwa na akina Abdallah na Mohammed hapa kwetu tz

Huu ukweli huwezi kuukwepa balance tu minzani usijipe shida
 
Kumbe bado anaishi!!! Ana miaka mingapi kwa sasa? Alipokuwa akiitawala zanzibar alikuwa na miaka mingapi?
Waliomtoa yeye madarakani vijana wa Umma Party wengi wa viongozi wake walishatangulia mbele za haki.

Karume ana bahati sana. Mapinduzi wafanye wengine uraisi akapewa yeye. Wakati hakushiriki kwenye mapinduzi hata kidogo.
Ana miaka 95. Anataka tu kumalizia uhai wake mahali alipozaliwa. Hizi ndiyo 4Rs za Samia
 
View attachment 3186808

Mnamo Januari 9, 2025, Zanzibar itashuhudia tukio la kihistoria itakapompokea Sultan Jamshid bin Abdullah kurejea kwenye pwani zake. Hili ni tukio muhimu sana kihistoria, kwani mtawala wa zamani wa Zanzibar anarudi baada ya miongo sita ya uhamisho nchini Uingereza na Oman, kufuatia kuondolewa kwake madarakani wakati wa mapinduzi ya 1964.

Cc Pascal Mayalla

Maelezo kuhusu jinsi ziara hii ilivyopangwa bado hayajafahamika, lakini umuhimu wake hauwezi kupuuzwa. Kurudi kwa Sultan Jamshid kunawakilisha ishara ya upatanisho wa kipekee kutoka kwa serikali ya Zanzibar. Ziara yake inaweza kuwa daraja kati ya enzi za kabla na baada ya mapinduzi, ikichochea mshikamano na uponyaji wa kitaifa.

Zanzibar inaweza kuchukua nafasi hii kumwalika Sultan kuishi katika mojawapo ya majumba yake ya zamani kama raia wa kawaida. Hatua kama hiyo haitaimarisha tu taswira ya Zanzibar kimataifa bali pia inaweza kuinua sekta yake ya utalii, kwani uwepo wake utavutia shauku kubwa. Zaidi ya hayo, inaweza kuashiria sura mpya ya upatanisho kati ya Sultan na serikali ya mapinduzi, ikitoa mfano wa maendeleo na mshikamano.

Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.


Ile ni roho ,itawatafuna wazanzibari na watangayika muda sio mrefu.

Mungu alimtimua shetani kwenye utawala wake na kukiondoa kabisa kiti chake na nafasi yake kule mbinguni .

Roho ya utumwa imerejea rasmi na itapata nguvu kupitia dini.
 
Unapopenda ufisadi uwe tayari kuishi na madhara yake.

Wewe sio mtu wa kulalamika (hasa) kwa kutumia ID hiyo ambayo ni mtetezi wa ‘bi-tozo’ bora ata ungekuja na ID nyingine.

Kwani we unadhani raisi Samia akienda Zanzibar ‘Othman Masoud’ anamlisha propaganda gani.

Na huku bara mshafundisha atafute watu wanaoiweza CCM na kuendesha nchi.

Yote kwa sababu ya kupewa maslahi yenu.

Yaani wewe ni mtu wa mwisho kulalamikia mustakabali wa nchi hii.

Ni mtu wa hovyo kweli
Umemlenga nani kwa ujumbe huo?
 
View attachment 3186808

Mnamo Januari 9, 2025, Zanzibar itashuhudia tukio la kihistoria itakapompokea Sultan Jamshid bin Abdullah kurejea kwenye pwani zake. Hili ni tukio muhimu sana kihistoria, kwani mtawala wa zamani wa Zanzibar anarudi baada ya miongo sita ya uhamisho nchini Uingereza na Oman, kufuatia kuondolewa kwake madarakani wakati wa mapinduzi ya 1964.

Cc Pascal Mayalla

Maelezo kuhusu jinsi ziara hii ilivyopangwa bado hayajafahamika, lakini umuhimu wake hauwezi kupuuzwa. Kurudi kwa Sultan Jamshid kunawakilisha ishara ya upatanisho wa kipekee kutoka kwa serikali ya Zanzibar. Ziara yake inaweza kuwa daraja kati ya enzi za kabla na baada ya mapinduzi, ikichochea mshikamano na uponyaji wa kitaifa.

Zanzibar inaweza kuchukua nafasi hii kumwalika Sultan kuishi katika mojawapo ya majumba yake ya zamani kama raia wa kawaida. Hatua kama hiyo haitaimarisha tu taswira ya Zanzibar kimataifa bali pia inaweza kuinua sekta yake ya utalii, kwani uwepo wake utavutia shauku kubwa. Zaidi ya hayo, inaweza kuashiria sura mpya ya upatanisho kati ya Sultan na serikali ya mapinduzi, ikitoa mfano wa maendeleo na mshikamano.

Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.
Mkuu Situ, Stuxnet ,hii ni habari njema sana,na najisikia faraja sana kwa jambo uliloshauri litekelezwe,nilianzia hapa Dear Mama, Can you Offer An Unconditional Amnesty to All Zanzibaris Waliokimbia After Revolution, Incl Sultan, Be Free to Return & Start Afresh? nikaja Voices From Within: Sultan Jamshid bin Abdullah Al Said atafurahi zaidi kama atarudi Zanzibar. Rais Samia, Rais Mwinyi, sameheni, utabarikiwa sana! halafu likatekelezwa Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni hata kama utekelezaji huo hauhusiani na ushauri wako,lakini ulishauri Sultani ajengewe mazingira ya kurejea Zanzibar, sasa anarejea Zanzibar, mtu unafarijika。

Kuhusu kurejea Sultani Zanzibar, Ushauri wangu ni huu。
  1. Serikali ya Zanzibar igharimie kila kitu kwenye ziara hiyo, apokelewe na kutembezwa na ving'ora as a healing process ya machungu aliyopitia。
  2. Aandaliwe an ad hoc protocal ya Sultan mpinduliwa,kwa jinsi ile ile katiba ya JMT,haitambui katiba ya Zanzibar lakini protocal inawatambua na wana ving'ora。
  3. Akabidhiwe part ya lile kasri lake la Beit Al Ajab, sehemu ibaki open kwa public,watalii waendelee kutembelea, sehemu iwe ni private ya makazi yake, watakao taka kupita na kumuona tuu akiwa amekaa kwenye kiti chake cha enzi cha Sultani, malipo yawe $100, kumsalimia $500 na kuzungumza na Sultan kwa dakika 5 ni $1000, matajiri wote wa kiarabu toka dunia kote watakuja Zanzibar, Sultan ndie atageuka kivutio kikubwa cha utalii Zanzibar!。
  4. Sehemu ya mapato hayo yatumike kumtegemeza na ziada iingie serikalini kama mapato ya utalii。
  5. Katika kuzungumza nae kwa dakika 5,inawekwa caveat,sio kuzungumzia machungu ya Mapinduzi,kuzungumzia mema na mazuri tuu ya Zanzibar。
  6. Media turuhusiwe kufanya mahojiano for healing process,tusimuulize maswali ya maudhi kuepuka kutonesha makovu ya Mapinduzi。Mfano mimi sitamuuliza kitu kuhusu hoja hii Kumbe Sultan Jamshid Alifurahia Kuuawa kwa Karume!. Alitaraji Kurejea Kama Sultani, Kumbe...
  7. Zanzibar ianzishe truth and reconciliation commission watu waruhusiwe to vent,hivyo to heal machungu ya mapinduzi。
  8. Decemba 10 iwe ni siku ya mapumziko ya uhuru wa Zanzibar,sio lazima iadhimishwe kwa shamra shamra,inaweza kubadili jina ikaitwa Sultan Day。
  9. Neno Matukufu kwenye Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,lisiendelee kutumika,yaitwe tuu Mapinduzi ya Zanzibar na vibwagizo Mapinduzi Daima, na Tutayalinda kwa gharama yoyote, tuachane nayo ili kuponya wapinga mapinduzi
  10. Falsafa ya 4R za Samia,itumike hadi Zanzibar,mshindi wa kweli wa uchaguzi wa Zanzibar atangazwe,mfano mzuri ni huu Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda na ili kumuondolea posibility ya aibu ya kushindwa,nimetoa ushauri hapa kwenye HII
P
 
Mkuu Situ, Stuxnet ,hii ni habari njema sana,na najisikia faraja sana kwa jambo uliloshauri litekelezwe,likatekelezwa,hata kama utekelezaji huo hauhusiani na ushauri wako,lakini ulishauri Sultani ajengewe mazingira ya kurejea Zanzibar, sasa anarejea Zanzibar, mtu unafarijika。

Kuhusu kurejea Sultani Zanzibar, Ushauri wangu ni huu。
  1. Serikali ya Zanzibar igharimie kila kitu kwenye ziara hiyo, apokelewe na kutembezwa na ving'ora as a healing process ya machungu aliyopitia。
  2. Aandaliwe an ad hoc protocal ya Sultan mpinduliwa,kwa jinsi ile ile katiba ya JMT,haitambui katiba ya Zanzibar lakini protocal inawatambua na wana ving'ora。
  3. Akabidhiwe part ya lile kasri lake la Beit Al Ajab, sehemu ibaki open kwa public,watalii waendelee kutembelea, sehemu iwe ni private ya makazi yake, watakao taka kupita na kumuona tuu akiwa amekaa kwenye kiti chake cha enzi cha Sultani, malipo yawe $100, kumsalimia $500 na kuzungumza na Sultan kwa dakika 5 ni $1000, matajiri wote wa kiarabu toka dunia kote watakuja Zanzibar, Sultan ndie atageuka kivutio kikubwa cha utalii Zanzibar!。
  4. Sehemu ya mapato hayo yatumike kumtegemeza na ziada iingie serikalini kama mapato ya utalii。
  5. Katika kuzungumza nae kwa dakika 5,inawekwa caveat,sio kuzungumzia machungu ya Mapinduzi,kuzungumzia mema na mazuri tuu ya Zanzibar。
  6. Media turuhusiwe kufanya mahojiano for healing process,tusimuulize maswali ya maudhi kuepuka kutonesha makovu ya Mapinduzi。Mfano mimi sitamuuliza kitu kuhusu hoja hii
  7. Zanzibar ianzishe truth and reconciliation commission watu waruhusiwe to vent,hivyo to heal machungu ya mapinduzi。
  8. Decemba 10 iwe ni siku ya mapumziko ya uhuru wa Zanzibar,sio lazima iadhimishwe kwa shamra shamra,inaweza kubadili jina ikaitwa Sultan Day。
  9. Neno Matukufu kwenye Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,lisiendelee kutumika,yaitwe tuu Mapinduzi ya Zanzibar na vibwagizo Mapinduzi Daima, na Tutayalinda kwa gharama yoyote, tuachane nayo ili kuponya wapinga mapinduzi
  10. Falsafa ya 4R za Samia,itumike hadi Zanzibar,mshindi wa kweli wa uchaguzi wa Zanzibar atangazwe, na ili kumuondolea posibility ya aibu ya kushindwa,nimetoa ushauri hapa kwenye HII
P
Ccm Yako huijui bado vizuri wewe.....hapo namba 10 utasubiri Sana.
 
View attachment 3186808

Mnamo Januari 9, 2025, Zanzibar itashuhudia tukio la kihistoria itakapompokea Sultan Jamshid bin Abdullah kurejea kwenye pwani zake. Hili ni tukio muhimu sana kihistoria, kwani mtawala wa zamani wa Zanzibar anarudi baada ya miongo sita ya uhamisho nchini Uingereza na Oman, kufuatia kuondolewa kwake madarakani wakati wa mapinduzi ya 1964.

Cc Pascal Mayalla

Maelezo kuhusu jinsi ziara hii ilivyopangwa bado hayajafahamika, lakini umuhimu wake hauwezi kupuuzwa. Kurudi kwa Sultan Jamshid kunawakilisha ishara ya upatanisho wa kipekee kutoka kwa serikali ya Zanzibar. Ziara yake inaweza kuwa daraja kati ya enzi za kabla na baada ya mapinduzi, ikichochea mshikamano na uponyaji wa kitaifa.

Zanzibar inaweza kuchukua nafasi hii kumwalika Sultan kuishi katika mojawapo ya majumba yake ya zamani kama raia wa kawaida. Hatua kama hiyo haitaimarisha tu taswira ya Zanzibar kimataifa bali pia inaweza kuinua sekta yake ya utalii, kwani uwepo wake utavutia shauku kubwa. Zaidi ya hayo, inaweza kuashiria sura mpya ya upatanisho kati ya Sultan na serikali ya mapinduzi, ikitoa mfano wa maendeleo na mshikamano.

Dunia inaposhuhudia tukio hili la kihistoria, Zanzibar inasimama katika nafasi ya kubadilisha urithi wake kuwa simulizi ya mshikamano na heshima ya pande zote.
Issa AlHarthy.
X anarudi nyumbani kwa mkewe kikongwe
 
Umemlenga nani kwa ujumbe huo?
Wewe si ndio shabiki wa huyu mama, sasa unadhani nimemwandikia nani mwingine.

Katika move ambayo huyu mama kaitibua CCM ni hii hasa upande wa Zanzibar.

Yaani ni kiazi, hamna kitu kichwani kwake.

Subiri utaelewa baadae namna gani kawakera CCM.

Mambo mengine mpaka uone matokeo yake ndio utaelewa.

Ugomvi wake utakuwa na CCM Zanzibar kwenda, mbele; yaani hana akili hata chembe.

Watch it
 
Ndio view ya Wazanzibari hio? Ama nyie wa Bara? Wazanzibari wengi ukiwaambia wachague utawala wa Sultan na huu wa sasa hawataki wa sasa, uchaguzi kila mwaka unaonesha.

Pia masultan wa Znz wengi wa miaka 100 iliopita ni weusi kushinda hata wewe.
Wazanzibar wako tayari kurudishwa utumwani chini ya mwarabu sultan wa Oman
 
Tatizo wazanzibar wanafikra za utumwa vichwani mwanao hata Mombasa Kuna jamii ya kiarabu lakini huwezi kusikia watu wa Mombasa wakiwalilia waOman waje wawatawale
Sababu Znz ni mix ya Waoman na wabantu, hilo ni jambo ambalo huwezi ukalifuta.

Oman ni Nchi ya kiarabu ila viongozi wao wote wana Asili ya Africa, na hutasikia Waoman wakilalamika kwanini tunatawaliwa na Wa Africa.

Masultan walileta maendeleo thats a fact, Wazanzibari waliheshimika, Znz waliingia mkataba na mataifa kama Marekani wasinunue kitu chochote toka kwa yoyote Africa bila kupitia wao, nani leo ana ubavu kama huu?
 
Vipi kuhusu wahindi na waarabu 5,000 waliookufa wakati wa mapinduzi ? Ni nani atafidia familia zao?
Watafidiwa na makwao walipotoka.....kikubwa hili bara ni la mu Afrika watajua wao walipotoka huko na kuja kufanya ufedhuli wao.......mtu mweusi alijibu mapigo maana walianza wao
 
Back
Top Bottom