Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Yes jeshi as jeshi ni moja, wale ni migambo
Hivyo rais wa Zanzibar ni amir jeshi wa migambo ya Zanzibar ya KMKM, JKU na vikosi vya SMZ.
P
Naomba kufahamishwa,
Km Rais wa Zanzibar ndie Kamanda Mkuu wa vikosi vya Zanzibar km KMKM,JKU,SMZ;
1.Je kuitwa vikosi sio kwamba ni majina tu kama kuitwa majeshi,pia vipi kuhusu mafunzo yaoyanatofauti ganina majeshi yetu,
2.Je huyo Kamanda Mkuu si ni sawa na amri jeshi katika vikosi vyake?
pia anauwezo wa kutoa oda yeyote na vikatekeleza ?
3.Je Rais wa JMT ambae ndie amri jeshi ana uwezo wa kutoa ida kwa vikosi vya Zanzibar na wakat huo vina Kamanda Mkuu ambae ni Rais wa Zanzibar
 
Naomba kufahamishwa,
Km Rais wa Zanzibar ndie Kamanda Mkuu wa vikosi vya Zanzibar km KMKM,JKU,SMZ;
1.Je kuitwa vikosi sio kwamba ni majina tu kama kuitwa majeshi,pia vipi kuhusu mafunzo yaoyanatofauti ganina majeshi yetu,
Ni majina tuu, lakini mafunzo ya kijeshi ni sawa kabisa!, tofauti ni utambuzi na mamlaka tuu, kama ilivyo kwa Rais Samia na rais Mwinyi wote ni marais sawa kabisa, ila wana utambuzi tofauti na mamlaka tofauti, mmoja ni rais wa nchi mwingine ni rais wa eneo, hata wewe mandomc nyumbani kwako, unaweza kupaita jamhuri ya mandomc, ndani kwako ukapandisha bendera, wiombo, ukajiita rais wa mandomc, ukabandika picha yako ukutani, utakuwa ni rais kweli wa mandomc, mlizi wako ukamuita ni jeshi la mandomc na wewe ni amiri jeshi mkuu wake, vyote hivi vitakuwa ni kweli ila tofauti ni utambuzi na mamlaka.
2.Je huyo Kamanda Mkuu si ni sawa na amri jeshi katika vikosi vyake?
pia anauwezo wa kutoa oda yeyote na vikatekeleza ?
yes ni amori jeshi mkuu wa vikosi hivyo viko chini yake, akitoa amri vinatekeleza.
3.Je Rais wa JMT ambae ndie amri jeshi ana uwezo wa kutoa oder kwa vikosi vya Zanzibar na wakat huo vina Kamanda Mkuu ambae ni Rais wa Zanzibar
Rais wa JMT ni amiri jeshi wa jeshi la JMT, hawezi kutoa order kwa hao migambo wa Zanzibar, kwasababu jeshi la JMT liko kote!.
P
 
Unaambiwa na Pengo , uulinde Muungano uliowekwa na mungu wenu



Kardinali Pengo: Muungano si bahati nasibu​



- May 02, 2016

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waamini na wananchi kwa ujumla kutambua kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar si jambo la bahati nasibu.

Kardinali Pengo ameyasema hayo ofisini kwake hivi karibuni alipoitisha vyombo vya habari vya Kanisa Katoliki kuzungumzia pamoja na mambo mengine ongezeko la Parokia mpya jimboni kwake pamoja na mabadiliko kwa Maparoko na Maparoko Wasaidizi katika baadhi ya Parokia jimboni humo.

Asemema suala la Muungano linapaswa kuchukuliwa kwa uzito wa pekee kwa kila Mtanzania hasa waamini Wakatoliki na kwamba kila mwamini anapaswa kutambua kuwa amepewa jukumu na Mwenyezi Mungu kulinda na kuombea Muungano huo.
Unaona sasa ulivyo punguani propaganda za ccm kutugawa(kidini)zilivyoathiri moyo na akili yako.
 
Yaani gavana ndiye Pengo ? Kweli wewe una akili nyingi
Pengo anahusikaje kwenye hili yani wewe tangu Cuf ife hasira zako umeziamishia kwenye Muungano na hivi mmejiunga na tawi la ccm linaloongozwa na Zitto Kazi mnayo najua mpasuko lazima utokee japo utazimwa na dola maana waliohama Cuf hawapendi huu muungano na Ccm na Zitto hawatakubali issue ya muungano iwe agenda maana Zitto anahofia kungolewa kwenye cheo chake cha Mkuu wa chama na ccm-dola kwa sababu Zitto ana makubaliano ya kufifisha upinzani na atalindwa kwenye hicho cheo chake endapo Act Cuf wataanzisha harakati za kumng'oa maana wanajua kikwazo namba moja ni Zitto na ili wayafikie
malengo yao ya kudai Muungano uvunjwe ni lazima wamngoe Zitto ila kwa sasa wanajipanga, na Act ili kiwe chama cha upinzani kweli ni lazima Zitto aondoke kitu ambacho ccm hawatakubali kuona mtu wao akingolewa kwa kuwa wanajua Zitto akiondolewa Act Cuf itarudi kwa mlango wa Act na harakati zao za kudai Muungano zitaanza na kikwazo ni Zitto kwa hiyo kuna Kazi kubwa kumng'oa Zitto iwe kwenye chama au cheo cha Mkuu wa chama alichojificha ila itategemea namna atakavyoathiri maslahi ya ccm-dola kwenye makubaliano yao kwa hiyo waliohamia Act kutoka Cuf mjipange kwelikweli.
 
Ukisimama upande wa Zanzibar ukatazama Tanzania Bara, Zanzibar ni nchi huru

Lkn ukisimama Tanzania Bara ukaangalia Zanzibar, Zanzibar ni sehemu ya Tanzania ma sio nchi huru. Hili utaliangalia kupitia katiba za nchi hizi mbili

Lkn pia Kwa upande mwingine Zanzibar ni huru kwasbb imeamua kuungana na Tanzania Bara katika baadhi tu ya mambo, na ndio Maana tuna mambo ya Muungano yanayotuhusu wote na Tuna mambo yasiyo ya muuungano .Haya ambayo yasiyo ya Muungano yana sheria zake Kwa upande wa Zanzibar lkn Kwa upande wa Bara (Tanganyika)kuna Sheria Ya Muungano Kwa Maana zinazotuhusi wote. Hapa ndipo unapoweza kugundua kuwa Bara (Tanganyika)imevishwa koti la Tanzania lkn Zanzibar imebaki yenyewe kama Zanzibar

Infact no Common Answer kutokana na namna nchi hizi zilivyoungana,ila inategemea tu unataka kuelezea jambo lipi
 
Pengo anahusikaje kwenye hili yani wewe tangu Cuf ife hasira zako umeziamishia kwenye Muungano na hivi mmejiunga na tawi la ccm linaloongozwa na Zitto Kazi mnayo najua mpasuko lazima utokee japo utazimwa na dola maana waliohama Cuf hawapendi huu muungano na Ccm na Zitto hawatakubali issue ya muungano iwe agenda maana Zitto anahofia kungolewa kwenye cheo chake cha Mkuu wa chama na ccm-dola kwa sababu Zitto ana makubaliano ya kufifisha upinzani na atalindwa kwenye hicho cheo chake endapo Act Cuf wataanzisha harakati za kumng'oa maana wanajua kikwazo namba moja ni Zitto na ili wayafikie
malengo yao ya kudai Muungano uvunjwe ni lazima wamngoe Zitto ila kwa sasa wanajipanga, na Act ili kiwe chama cha upinzani kweli ni lazima Zitto aondoke kitu ambacho ccm hawatakubali kuona mtu wao akingolewa kwa kuwa wanajua Zitto akiondolewa Act Cuf itarudi kwa mlango wa Act na harakati zao za kudai Muungano zitaanza na kikwazo ni Zitto kwa hiyo kuna Kazi kubwa kumng'oa Zitto iwe kwenye chama au cheo cha Mkuu wa chama alichojificha ila itategemea namna atakavyoathiri maslahi ya ccm-dola kwenye makubaliano yao kwa hiyo waliohamia Act kutoka Cuf mjipange kwelikweli.
Yaani gavana ndiye Pengo ? Kweli wewe una akili nyingi
 
Mkuu sijui mm nilikuwa wapi sijaona bandiko lako huwa nikiona koment yako mahali popote Happ jf nafurahi mno na Kisha natulia kukufatiliza wew unasemaje au unamuelekeo gani hvyo nakuaminigi Sana chochote usemacho ,wee Ni member mmoja wapo nakukubali Sana Sana na sijui kwanin ??nitatatafuta siku moja nikione live live mnk navutiwa Sana na wew. Hapa ktk jamvi


Embu ona elimu uliyoshusha Happ jamvini kwa koment yako mmoja tu na nzito na kumfunika Hadi mleta mada


We w nadhani ccm ccm wakutumie vzr kwenye ishu hi ya muungano Kuna kitu ,vitu unavijuwa kwa uelewa mpana Sana

Happ awali nilidhani muungano ni muhimu kwetu cc kumbee unatunyonya cc watanganyika Ni kheri kubakia na jina bovu la tanganyika kuliko upuuzi huu wa Sasa HV

Ubarikiwe Sana mkuu kwa elimu ya bure uliyo nipa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mkuu nashukuru sana, tuendelee kufanya kazi kwa bidii.
 
Siyo msimamo wangu. Ni msimamo wa Sheria za Tanzania na zile za Kimataifa. Rejea pia case ya Machano Hamis Machano iliyoamuliwa na Mahakama ya Rufaa ya Tanzania
Kwahiyo leo tusipokuwa na kiti kule UN basi hatuwi taifa au dola ?
 
Zanzibar ni nchi Kwa mujibu wa Katiba ya zanzibar
Screenshot_20221230-170221_1.jpg

Screenshot_20221230-170211_1.jpg
 
Ni kweli Zanzinzibar ni nchi kwa Katiba ya huko huko ila kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Zanzinzibar sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hiyo sheria inayoitambua Zanzinzibar ni nchi kwa Katiba ya Jamhuri ni batili.
 
ZANZIBAR SIO NCHI. NI MOJA YA MIKOA YA TANZANIA AMBAO UMEPEWA JINA LA NCHI.
 
Kutoka kitabu, kwaheri ukoloni kwaheri uhuru




Mzee Faraji

Nilipata kusikia kutoka kwa mmoja wa Marais wa zamani wa Zanzibar, kuwa manunguniko na madai ya Wazanzibari yaliyoanza katika miaka ya 70; kuhusu kuvunjwa mkataba wa 1964, kwa manufaa ya Tanganyika; madai hayo yalikuwa yakiwaudhi sana viongozi wa Tanganyika.

Hivyo siku moja Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, akamwambia Raisi wa Muungano (wakati huo) Mwalimu Nyerere, kwamba kwanini hawavunji mbali muungano ili wapumzike na “kelele” za Wazanzibari? Inasemekana Mwalimu Nyerere alimjibu kwa kumkatalia kwa kusema mengi pamoja na “…tukiwaachia tu, utaona jinsi mapesa ya Waislamu na Waarabu yatakavyo miminika Zanzibar…hapana, hatuwaachii.”

Laiti shida ya Mwalimu Nyerere ingelikuwa nae anazitaka pesa hizo kwa ajili ya Tanganyika, kisa kifuatacho kisingelitokea. Kwa mujibu wa kisa hiki kama kilivyosimuliwa na Rais huyo wa zamani [wa Zanzibar], Mwalimu Nyerere, wakati huo akiwa ameshastaafu, alipita akiwa safarini, katika uwanja wa ndege Jeddah, Saudi Arabia. Balozi wa Tanzania aliyekuwepo Saudi Arabia ilimlazimu ki-protokoli, kwenda uwanja wa ndege kuzungumza nae katika muda wa transit.

Pamoja na mambo mengine, Balozi huyo alimwambia Mwalimu Nyerere “…katika nchi hizi kuna mapesa mengi, na jamaa yaelekea wapo tayari kutusaidia mipango yetu mingi ya maendeleo, ilimradi tu, tuwaombe.” Nasikia Mwalimu alimjibu kwa mkato na kwa kiasi cha kuonekana kakasirishwa: “Hapana. Acha kabisa!”1

Ni dhahiri, mpishi wa mapinduzi na muungano, Mwalimu Nyerere, alikuwa ameacha “grand design” [mpango mkubwa] katika kuipata Zanzibar, bila shaka si kwa manufaa ya nchi (Tanganyika na Zanzibar), bali kwa manufaa ya wale wasiowatakia mema Waislam (pamoja na Waarabu ambao wengi wao ni Waislam).

Niliwahi kumuuliza mmoja wa Maraisi waliopita wa Zanzibar kama aliwahi kuuona waraka asilia [wa Muungano baina ya Zanzibar na Tanganyika] uliotiwa saini tarehe 26 April 1964, akaniambia hapana, hajawahi kuuona. Nikamuuliza tena, je, yule uliyemuachia nafasi yako unaweza kumuuliza kama kawahi kuuona? Akanijibu: “hapana haja ya kumuuliza, kwa sababu nafahamu kuwa nae pia hajauona.”

Kwa kawaida nchi inapotaka kujiunga na Umoja wa Mataifa (UN), hutowa taarifa ya mwezi mmoja na kisha kuwasilisha maelezo/vielelezo na vithibitisho kuwa ni nchi (yenye sifa ya kuwa na Utaifa), inayostahili heshma ya uwanachama huo. Nchi zilizokuwa zinapata uhuru wake toka ukoloni zilitoa taarifa ambayo tarehe yake ya mwisho ilisadifia na tarehe ya kupandisha bendera mpya.

Hivyo nchi iliyojisajili UN na kupewa kiti, bila shaka ilipobadili nafasi iliyoiondosha uwananchi wake, haikuondoka katika umoja huo bila ya taarifa yoyote. Bila shaka patakuwepo maelezo na vielelezo vilivyokubalika kiti chake kurudishwa, bendera yake kushushwa katika mlingoti wa UN, na majukumu yake kame vile michango n.k., kufutwa.

Vipi leo nchi kama hiyo isiwe na hati halisi ya makubaliano ya muungano ambayo wananchi waliona Sheikh Karume na Mwalimu Nyerere wakisaini na kupeana April 26, 1964? Na vipi nchi isiwe hata na zile nakala halisi za vielelezo japo vile vilivyopelekwa UN kuhusu suala zito la utaifa wake? Au hata ushahidi wa kisheria kuwa hakuna nchi inayoitwa “Tanganyika” au yakuwapi maelezo/vielelezo kuhusu kuongezeka kwa mambo ya muungano na nani alotia saini kwa niaba ya Zanzibar? Ni saini yake au ni ya nani na kwa ushahidi gani wa kisheria?

Wenye kuumizwa na yote hayo khasa ni Wazanzibari na si Watanganyika. Mapinduzi ndo yalioipinduwa nusu ya jamii ya Zanzibar ilioshinda uchaguzi [wa Julai 1963]. Mapinduzi ndo yaloleta muungano na kuyapinduwa makubaliano ya mwanzo ya muungano. Mapinduzi ndo yaliokifuta kiti cha Zanzibar UN kwa nia ambazo Wazanzibari bado hawajazitambuwa.

Mapinduzi ndio yaliomuondowa Al Hajj Aboud Jumbe madarakani, na kilichomponza khasa Mzee Jumbe ni pale alipolianzisha Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA); yakamtia ndani Maalim Seif Sharif Hamad; na ndiyo yaliyopelekea Dk. Salmin Amour akataliwe kuiingiza Zanzibar/Tanzania katika OIC na kuiakhirishia Zanzibar kutojiunga na taasisi hiyo. Ndiyo yaliyoifanya Katiba ya nchi itamke kuwa Raisi wa Zanzibar siyo tena Makamo wa Kwanza wa Rais wa muungano, kama ilivotamkwa 1964. Na ndiyo yaliyo “thibitisha” kuwa nchi ya Zanzibar sasa ni Mkoa kama mkoa wowote Tanzania. Na kubwa zaidi, hayo ndiyo yaliyofanywa kuwaonesha rasmi Wazanzibari kuwa hata ndani ya chama kilichoundwa kwa kuunganisha ASP na TANU, TANU, CCM Bara, ndiyo itakayoamua nani atagombea Uraisi Zanzibar.

Hivi sasa hakuna udhibiti kwa watu kutoka bara kuingia na kuishi Zanzibar. Lengo ni kubadilisha “demographic situation in favor” [hali ya wingi wa watu] ya bara katika miaka michache ijayo. Na hiyo population [idadi ya watu] mpya inaandaliwa kuwa “superior” katika uchumi, ilimu na ushawishi wa kisiasa. Wapemba kuunga mkono chama kinachoongozwa na Maalim Seif Sharifu, Mpemba, university graduate [mhitimu wa Chuo Kikuu] na mzoefu katika serikali na siasa; mtu ambae alikhitalifiana na Mwalimu Nyerere inakaa vizuri katika “grand design” [mkakati mkubwa] ya Mwalimu ya kuwatenga Waunguja. Nyerere alipoenda Zanzibar kueleza kwa nini CCM iliwafukuza Seif na wenzake, alimtaja Seif kama watu “…tuliokuwa tukiwapokea katika chama pasipo kuwachunguza kwa undani ili kujua asili yao na huko watokako…” Mbali ya maneno hayo, Nyerere pia alianzisha propaganda za kwamba watu wenye rangi ya kuchovya kama ya Seif, japo si Waarabu, alitaka watazamwe kama Waarabu. Siasa zao zitakuwa za kutaka kumrudisha Mwarabu Zanzibar.

Nyerere pia alianzisha lugha ya kampeni ya “kuwanasihi” watu wa bara (Tanganyika), kama moja ya propaganda zake za kujenga hoja ya kujitetea pale itakapoonekana kuwa bara inatumia nguvu kulazimisha muungano. Ikawa akisema mara kwa mara kuwa “…hawa wanataka kuuvunja muungano, mkiwaachia, watauana ovyo…sasa wameshaanza kugawanyika na kubaguana, kati ya Wazanzibari na Wazanzibara…Wapemba na Waunguja…” Ingawa hoja hiyo inakusudiwa kuwaomba Watanganyika “kuwanusuru” Wazanzibari ili wasi-jeuana, haikumpitikia Mwalimu wala wengineo kuhoji; kama Wazanzibari wamegawika kiasi hicho, msimamo wa uhalali wa muungano ukoje hivi sasa? Tanganyika hivi sasa imeungana na nani; Wapemba, Waunguja, Wazanzibari au Wazanzibara? Siri ya mapinduzi ya wazee inatowa jawabu lililo safi; Tanganyika iliungana na Waafrika kutoka bara kuwapinduwa Wapemba na Waunguja—Wazanzibari.

Katika mambo ya kudhulumiana nchi, wajanja hufanya kila njia kuepuka masuala ya mfumo. Watakupelekeni kwenye utendaji kazi. Huko mtazungumza na wale waliopewa kazi ya ku “run” government [kuendesha serikali]. Hamtokutana tena na wale wanao “rule” [wanaotawala]. Sioni sahihi kuutegemea Muwafaka badala ya Mkataba wa Muungano na Katiba na sheria za nchi, kutupa muelekeo wa kule tunakostahili kwenda. Hivyo hivyo, siamini kuwa mtu atayewekwa na madhalim katika madaraka ya nchi, ana uwezo wa kujua na kuipeleka nchi hiyo pahali pasipokuwa pale panapo takiwa na madhalim hao.

Kwa vyoyote vile, endapo tutatanabahi, tukatambua kuwa nguvu za wananchi ni muhimu kuliko chochote, na kwamba nguvu hizo hazipatikani ila kwa kuwatoa katika umasikini wa kiza cha ujinga wa ilimu duni; tunakoelekea si kubaya. Kuwatowa wananchi kunako giza la tunakotoka na Zanzibar kujiwakilisha nchi za nje, kuujenga na kuulinda uchumi wake, pamoja na kulindwa na Wazanzibari, ni kuzuri, na huko ndiko kwa kuanzia.
Hio hapo ,iliitwa United Republic of tanganyika and zanzibar, tujiulize kwa nini tunafichwa historia,
 

Attachments

  • main-qimg-dabc033474ff9b6225c1805d60d0b953.png
    main-qimg-dabc033474ff9b6225c1805d60d0b953.png
    4.3 KB · Views: 2
Back
Top Bottom