TANZIA Zanzibar: Salim Turky, Mwanasiasa Mkongwe na Mgombea Jimbo la Mpendae Zanzibar, afariki dunia

TANZIA Zanzibar: Salim Turky, Mwanasiasa Mkongwe na Mgombea Jimbo la Mpendae Zanzibar, afariki dunia

Allah ailaze royo yake mahala pema

Turky alikua muungwana sana.

Katika Jimbo lake la Mpendae-Zanzibar, kiuhalisia ni jimbo la UPINZANI.

Mwakilishi kutoka Upinzani, Kura za Uraisi pia upinzani unaongoza kwenye Jimbo lake.

Lakini Nafasi ya Ubunge, Wananchi wanaweka siasa pembeni Turky anasimamishwa kwa Ushindi wa kishindo.

Turky alikua hana ubaguzi wa kisiasa, akitoa misaada anatoa kwa nyumba zotee bila kuangalia itikadi.

Akisaidia wajasiriamali hakuangalii itikadi yako ya Chama wala wapi Unatokea.

Hakika tukipata Viongozi mfano wa Turky tutakuwa mbali mnoo..
 
Kafariki leo usiku ghafla,juzi alikuwepo kwenye uzinduzi wa kampeni za Ccm Zanzibar.

Tulikuwa nae pamoja msibani Jumapili mwenye afya njema kabisa. I even joked with him, nikamwambia mavazi meupe kayapatia hasa kama kwenye msiba wa kihindi. Akacheka sanaa. Kwa wote wasiomjuwa, alikuwa the nicest guy ever, self depricated, hakujiweka kama muheshimiwa au tajiri. Alipenda kukaa pamoja na watu wa tabaka zote na kupiga nao stories za kijiweni.

The hole you have left with your sudden departure will never be filled up. Loved all and loved by all. Rest in eternal peace brother. Will be dearly missed but your presence will never leave us!
 
Lissu hana shukrani aliendelea kuponda CCM hata Kama walimsaidia. Mbowe mwongo hakutoa chochote Hadi turky akawasaidia ndege ya rafiki zake akawahishwa Nairobi kwa matibabu zaidi Hadi leo kapona kwa msaada wa Wana CCM. Turky alitoa ndege alikuwa mbunge wa CCM chadema mlikuwa wapi?
"Pengine msaada ume mletea tatizo maan ulimuoko mwiba"
 
Kumbe kwenye kundi la mashetani unaweza pata malaika japo mmja,rest in peace seems ulikuwa una ubinadamu sio Kama mwenyekiti na yule wa bungeni
 
Lissu hana shukrani aliendelea kuponda CCM hata Kama walimsaidia. Mbowe mwongo hakutoa chochote Hadi turky akawasaidia ndege ya rafiki zake akawahishwa Nairobi kwa matibabu zaidi Hadi leo kapona kwa msaada wa Wana CCM. Turky alitoa ndege alikuwa mbunge wa CCM chadema mlikuwa wapi?
Acha kunywesha watu sumu humu.
 
R.
Mwanasiasa mkongwe na mfanyabiashara maarufu Turk wa Zanzibar afariki dunia.

===

Mheshimiwa Salim Hassan Abdullah Turky, afariki dunia usiku huu akiwa hospitali ya Tasakhta global chanzo cha kifo chake inadaiwa kuwa aliugua ghafla. Swala ya maiti itafanyika leo Alasiri September 15 katika msikiti wa Othman Maalim na baada ya hapo atazikwa Fumba, Zanzibar.


Salim Turky alikuwa mfanyabiashara maarufu Zanzibar na mbunge wa jimbo la Mpendae tangu 2010, alizaliwa February 11, 1963. Mpaka anafariki alikuwa mwenyekiti wa makampuni ya Turky ambapo chini yake yalikuwa makampuni 12 yanayoendesha biashara zake Tanzania Bara, Zanzibar na visiwa vya Comoro.

Baadhi ya makampuni hayo yanajumuisha hoteli ya Golden Tulip, hospitali kubwa ya Tasakhtaa Zanzibar, pia ilijihusisha na biashara ya cement, Nitak communications, vyakula na mafuta.

Turks Group iliazishwa mwaka 1978 kama duka la nguo na ndugu wa familia moja ambao ni Salim, Murtadha na marehemu Yunus pamoja na baba yao, Hassan Turky na miaka 40 baadae wakalibadilisha kuwa moja ya makampuni yanayoongoza Tanzania.

Mwaka 2017 Lissu aliposhambuliwa kwa risasi, Turky alitafuta ndege iliyompeleka Lissu Nairobi na kuwa mdhamana wa deni la kukodi ndege iliyokuwa inamilikiwa na FlyghtLink ambao ni jamaa zake katika biashara.

Zaidi, soma:

= > Safari ya Lissu kuelekea Nairobi ilikuwa ni mateso na vilio, Spika Ndugai usitoneshe vidonda

= > Salim Hassan Turky: CHADEMA walilipia gharama za Ndege iliyomsafirisha Lissu

R.I.P Turky,Mwana CCM aliyekuwa mzalendo,muungwana na mwenye huruma kwa binadamu wenzake bila kujalisha itikadi.
 
By

Pascal Mwakyoma TZA


September 15, 2020


Mgombea Urais kupitia chama Cha CHADEMA Tundu Lissu akiongea na wananchi wa Njombe katika Viwanja vya National Housing ametoa pole kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Mpendae Salim Turk ambaye amefariki usiku wa kuamkia leo.

“Wakati nilipopata matatizo, Marehemu Salim Turky alimuendea Mwenyekiti Mbowe akamwambia Mwenyekiti mimi nitatoa dola za Marekani laki moja ili ndege ipatikane mimi nipelekwe Nairobi” Tundu Lissu
 
Huo ndio utu!! Utamaduni wa watz, toka enzi na enzi sio hao washamba ndio wamegeuza siasa kuwa ni uadui!!! Yaani kwa sasa mzungu/mwarabu anaweza kuwa na uchungu na mwana chadema apatapo majanga kuliko mwana ccm?!! Atakavyoguswa!!!
 
Turky alitenda wema mweupe kabisa kutoka moyoni, kukodi ndege kwa ajili ya mtoto wa Mungu aliyepigwa marisasi na wakala wa shetani ili afe. Turky kazi yake imekwisha...
 
Huo ndio utu!! Utamaduni wa watz, toka enzi na enzi sio hao washamba ndio wamegeuza siasa kuwa ni uadui!!! Yaani kwa sasa mzungu/mwarabu anaweza kuwa na uchungu na mwana chadema apatapo majanga kuliko mwana ccm?!! Atakavyoguswa!!!
Chadema wana utu? Tuambie ni jambo gani jema Chadema wameshawahi kulifanya katika nchi hii. Siyo wakati majanga wala chochote kile, salamu za pole tu mwiko kwao. Misiba hawahudhurii, hata misaada tu ya kibinadamu hawana.
 
Back
Top Bottom