Zanzibar: Yaliyojiri kwenye ziara ya Rais Magufuli kisiwani Pemba - Sept 2016: Ampongeza Jecha kusimamia uchaguzi vizuri

Zanzibar: Yaliyojiri kwenye ziara ya Rais Magufuli kisiwani Pemba - Sept 2016: Ampongeza Jecha kusimamia uchaguzi vizuri

Katiba,katiba,katiba.Nina hakika kama huyu mtawala wa sasa angekuwa rais miaka 10 iliyopita hata hule mchakato wa Katiba usingekuwepo,hii style yake si ya kiongozi ni style ya watawala.
 
"Tanzania tumechezewa mno na kama kuibiwa tumeibiwa mno... Mimi nipo serikalini najua. Kila mahali ni dili! Kila mahali ni dili... Ukigeuka hivi unakuta kuna mahali palikuwa panapigwa dili... Ukigeuka hivi unakuta kuna mahali palikuwa panapigwa dili... Yaani ni dili ni dili tu... Ila naomba niseme kutoka moyoni Tanzania kugeuzwa shamba la bibi sasa basi... Ni lazima iwe mwisho na nasema imetosha!" Mhe Rais Dkt Magufuli.

Hii vita si nyepesi. Tunakuombea na kukuunga mkono Mhe Rais.

[HASHTAG]#ImetoshaKuibiwa[/HASHTAG]
 
Kwa bahati mbaya, jana sikupata fursa ya kufuatilia ziara ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano huko kisiwani Pemba!! Kutokana na hilo, leo nikaamua kuperuzi peruzi hapa JF. Kitu ambacho kimenishitua sana kama sio kunitisha ni kauli ya Mheshimwa Rais JPM aliyomwambia Mheshimiwa Dk. Shein. Hii ndio kauli ya JPM ambayo imenishitua kwa kweli:

Binafsi nashindwa kuamini ikiwa Rais aliyechaguliwa kupitia sanduku la kura, bado anaweza kuwa na kauli kali na ya vitisho namna hiyo!! Sasa ikiwa ni kweli mtu ameshindikana na Mheshimiwa Shein; yeye Mheshimiwa JPM atamfanya nini huyo mtu ndani ya hizo dakika 5?! Hapa lazima niwe na hofu kwavile JPM ni Commanding In Chief na majeshi yote yapo chini yake! Ni wapi tunaelekea kwenye hili taifa?! Mbona ikiwa mambo yenyewe kama ndo haya mbona hayo magereza yenu hayatatosha kufunga "wachochezi"?

Nafahamu wapo wanaofurahia na kushadadia kauli kama hizi huku wakidhani haziwahusu!! Pamoja na yote hayo, mnapaswa kufahamu fika kwamba; wote nyinyi hata kama mna kadi za CCM bado ni vidampa tu mbele ya yule Kingunge Ngombale Mwiru wa CCM!! Hata kama mna kadi tangia enzi za TANU, wote nyinyi ni vidampa tu mbele ya mtu kama Lowassa au Fredrick Sumaye wa enzi za CCM! Na si ajabu, ni vidampa hata mbele ya mtu kama Lawrence Masha aliyepata kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nchi hii!!

Hii maana yake nini? Usidhani vitisho kama hivi wewe havikuhusu kwa sababu tu wewe ni kada wa CCM! Kama ndivyo unavyodhani, basi uelewa wako ni mdogo kupitiliza! Nimewataja hapo akina Kingunge ambao miezi 30 tu iliyopita nao wangedhani kauli za vitisho kama hizo haziwahusu! Je, mtu kama Lowassa ambae hapo kabla angedhani kauli kama hiyo haimuhusu leo anaweza kudiriki kusema hivyo? Who are you ndani ya CCM compared to Kingunge Ngombale Mwiru? Ingawaje Kingunge ametoka CCM; hivi unaamini vigogo kama Mzee Mwinyi au Pius Msekwa anaweza kukuamini kada wewe kuliko Mzee Kingunge?!

Endeleeni kufurahia kauli za vitisho kama hizi lakini kaa mkifahamu hili si la mmoja! Wakati inapitishwa Sheria y Mitandao niliamini kwamba hainihusu kwa kile nilichoamini nikiwa na akili yangu timamu siwezi kuingia online na kuanza kutukana watu, kuanza ku-post picha za utupu n.k! I swear to God, niliamini hainihusu kabisa na hata hapa niliwahi kuandika kwamba "A black cat may be a bad lucky only if you're mouse!" Lakini leo hii hakuna sheria ninayoiogopa kwenye hii nchi kama sheria ya mitandao ambayo, practically imebadilika kutoka kuwa Sheria ya Mitandao to Sheria Ya Kubana Maoni!

Ajabu ni kwamba, utakuta wengi wanaoshabikia kauli kama hizi hapa JF ni vijana wadogo wengine wakiwa below 30. Don't be stupid, you've a very long way to go!! Hilo hilo unaloshabikia leo wakati hata direction ya maisha yako haija-settle ndio hilo hilo litakalokutafuna kesho kwenye harakati zako za kimaisha!

Ikiwa kupinga kauli ya Rais ni UCHOCHEZI, am ready to face consequences lakini kauli hiyo ya Rais haileti picha nzuri kutoka mdomoni mwa Rais aliyechaguliwa kwa sanduku la kura. Haipendezi kutoka mdomoni mwa Commanding In Chief ambae Majeshi ya Ulinzi na Usalama yapo chini yake!

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Duuuuh hii nchi imeshakuwa ya kujaribiwa
 
.

"Kuna watu wanasema mzunguko wa pesa umepungua na hali imekuwa ngumu, hizo pesa zilizokuwa zinachezewa huko mtaani zilikuwa pesa za serikali. Mimi nataka pesa ziende kwenye miradi ya maendeleo na ndiyo maana bajeti ya maendeleo tumeiongeza kutoka 26% hadi 40% ".

-Mh Rais John Pombe Magufuli , 1st September 2016
 
Najua mmeshachoshwa na vtisho na ahadi hewa kwa watoto maskini,so nini kifanyike ili tuwe na uhuru kwa nchi yetu,coz hii ni nchi ya watu wote na s mmoja,hayo ni madaraka tu ya muda but watu wanashindwa kutumia utu,busara na hekima .hilo ndo tzo kubwa kwa africa,but kwa tz awamu hii imepitiliza bora juzi na hata jana lkn leo imekuwa too much
 
Acha uongo kila mtu anajuaje CUF walishinda wakati kura hazikuhesabiwa zote na tume haikutangaza matokeo? Mtu kujitangazia kuwa ameshinda ndiyo unataka kuaminisha watu kiupotofu kuwa CUF ilishinda? Endelea kuota ndoto bandia ambazo hazitakuja kutimia.
Acha uongo!!

Kura zote zilihesabiwa ila sema ZEC haikuverify kura zote kabla ya kufuta uchaguzi. Kura zinahesabiwa vituoni. Sasa kuna kituo kinahesabu kura zaidi ya siku tatu!?
 
Ndugu watanzania CCM, wapenda maendeleo na TBC kwa ujumla inakukaribisha/kukutaarifu kuwa leo jioni katika kipindi muddaartt kabisa cha "Tunatekeleza" atakuwepo Mh Harrison Mwakyembe waziri wa sheria na katiba kuelezea maendeleo na mipango/mikakati ya wizara yake katika kulipeleka taifa mbele kimaendeleo, kisheria na kuzongatia haki kwa wote.

Itakusaidia sana. Itakungua akili zaidi, hivyo usikose!!!
 
Rais wa JMT Mh Magufuli ametoa kongole zito kwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ZEC kuwa alifanya kazi kwa uadilifu na kwakweli anastahili sifa na tuzo ya heshima kwa kuiweka historia vyema na daima atakumbukwa.

Salim Jecha pokea pongezi kutoka kwa rais na kutoka kwa CCM Tanzania.
[HASHTAG]#hiindiccm[/HASHTAG]
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Magufuli amempa ujumbe mzito kwa Dr Shein kuwa aache upole na awe mkali kuwashughulikia kikamilifu wale wanaoleta mchezo kwa serikali.

Waonyeshe kuwa dola unaiongoza wewe, sio wanaleta chokochoko na waachwe hivyohivyo. Waonyeshe kazi.

[HASHTAG]#hiindioccmyahapakazi[/HASHTAG]
 
TBC hata Mkulu haangaliagi, kipindi hicho wangepeleka clouds
 
Serikali inayoongozwa na CCM chini ya Mh rais magufuli inetoa onyo kali kwa wale wanaodhania wataivuruga amani ya taifa. Jana rais alipokuza ziarani pemba alitoa dhamira nzito kuwa hatowavumilia vibyangarika watakao vuruga amani ya nchi
 
Katiba,katiba,katiba.Nina hakika kama huyu mtawala wa sasa angekuwa rais miaka 10 iliyopita hata hule mchakato wa Katiba usingekuwepo,hii style yake si ya kiongozi ni style ya watawala.
Pasingekuwa na mchakato wa katiba bali pangetokea ubadilishaji wa katiba hususani ibara inayoweka ukomo wa kuwa madarakani! Hata hivyo si kwamba hilo halitafanyika tena, it's a matter of time! Katu sitarajii kuuona ule ukali wa Mkapa pale baadhi ya watu kwa kujipendekeza tu; wakaanza kunong'ona nong'ona kwamba eti katiba ibadilishwe ili Mkapa aendelee! Mkapa akawajia juu mchana kweupe!
 
Ubabe haujawahi saidia chochote katika kuleta umoja, amani na maendeleo kwa wananchi. Hekima na Busara kwenye uongozi vinahitajika zaidi katika dhama hizi. Msije mkapandikiza vitu ambavyo mkizeeka mtakuja juta.
 
Ndugu Wanachadema Mkoa wa Arusha, sisi ni vijana wenye uchungu na chama chetu ndio maana tuko tayari kuipigania hata kuifia ili tupate ukombozi. Ni sisi tulikesha nje ya mahabusu alipowekwa ndani Kamanda Godbless Lema. Alivyoshinda siku tatu bila kula na sisi tulishinda naye bila kula.

Ndugu wanaChadema chama hiki kimejengwa kwa nguvu za umma yani sisi ndio maana CCM imefutika hapa Arusha. Hakipo.
Tuna uchungu sana. Hapa Arusha tumeshapigwa sana na Policcm tukitetea ukombozi. Wenzetu wameshatangulia mbele za haki. Mungu awarehemu. Yote ni kupigania ukombozi.

Ndugu zetu wanaChadema na Watanzania, hivi karibuni Kamati Kuu chini ya Kamanda Mbowe iliazimia tuandamane nchi nzima na mikutano kupinga Udikteta wa Serikali ya maCCM isiyotaka demolrasia, UKUTA ya Sept Mosi.

Vijana wa Arusha tulijiandaa vilivyo kupambana na Policcm endapo wangetuzuia hadi tone la mwisho la damu yetu. Tuko tayari kuifia haki na demokrasia. Dunia nzima ilijua ni siku ya ukombozi Tanzania.

Ndugu wanaChadema tumesikitishwa sana, tumeumizwa sana, tumefedheheshwa sana na kitendo cha Mbowe kwa hiari yake kusitisha maandamano hayo kwa madai eti ameombwa na viongozi wa dini na Lowassa naye ameombwa na familia ya Nyerere tuache kuandamana.

Ndugu wanaChadema, popote mlipo hata nje ya nchi tumechunguza hata kuongea na baadhi ya viongozi wa dini aliowataja Mbowe wamekataa hawakuongea naye hivyo Mbowe ni mwongo. Hata familia ya baba wa Taifa wamekataa hawakuongea chochote kuhusu Ukuta.

Tunatambua heshima ya Lowassa kwa chama. Lakini ni dhahiri Mbowe anamwogopa Lowassa. Lowassa bado ana maslahi binafsi na CCM ndio maana hapendi uharakati ambayo ndiyo asili ya Chadema na chama chochote cha upinzani. Tazameni Garbon.
Lowassa anatuletea siasa za Ccm. Anataka tufanane nao mafisadi. Arudi alikotoka.

Maandalizi ya UKUTA Sept 1 imegharimu chama mamilioni ya shilingi ilhali wilaya kibao hatuna ofisi, tumepanga na tunadaiwa kodi. Nani atarusisha fedha hizi?

Mbowe amelewa madaraka ya Uenyekiti wa Chadema. Sisi vijana kwa umoja wetu tunamtaka Mbowe na Lowassa wakae pembeni ili kamanda Lissu atuongoze. Hatuwezi kubembeleza haki yetu.
Tunamtaka aondoke na Lowassa wake atuachie chama. Kinyume cha hapo tumeamua kujichangisha fedha tutaenda kwa Msajili Dar es salaam atusajili kama CHADEMA-ASILI.

Akiondoka hata leo hatutafikia huko. Tulianza na Mungu tutamaliza na Mungu. Vijana wengine wa mikoa mingine mtuunge mkono kama Singida na Kagera ambao nao Wako mbioni kutoa matamko.

Ahsanteni
John Ole Kaparo
Mwenyekiti wa Muda
Kamati ya Kudai Chadema Asili (KAKUCHA)
 
Ujumbe murua kabisa huo!. Na hizi ndizo busara zilizotukuka za mkuu wetu wa nchi, Mhe. rais, Dr. John Pombe Joseph Magufuli!.
Mwenye masikio na asikie! .
Pasco
 
Back
Top Bottom