Zari amlipua Diamond kwamba hatoi hela ya matunzo ya watoto wake baada ya kutangaza kulipa kodi za kaya 500

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Mwanamama mrembo na mjasiliamali Zari the Bosslady aliyezaa watoto 2 na Diamond Platnumz amemlipua mzazi huyo mwenzie baada ya kutangaza kulipia makazi kata 500 wakati hajua watoto wake wamekula Nini wala wamelala vipi.

Zari anamwambia Diamond huwezi furahisha dunia wakati wakwako hawana furaha na wewe wala kuwajali.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeye kataka kushindana na mwanaume wake,haiwezekani ukambadilisha uraia mtoto bila kumshirikisha mwanaume,kisa una hela alafi mwanaume akuchekee

Mbona Hamisa sasa hivi halalamiki na mtoto huwaga anampeleka kwa baba yake siku moja moja,yy mtoto kambadilisha uraia kilazima na kwa baba yao hutaki kuwa peleka.Mbona hajaumia mwaka jana alivyo kabizi pikipiki kwa bodaboda wa Tandale,kutoa matank kwa baadhi ya shule za tandale pamoja na Insurance.

Yeye tatizo anajiona ana hela,yeye kiburi kakutana na jeuri na ndio maana baadhi ya wanaume tunaogopa kuoa wanawake wenye hela.

Mwisho wa siku anawavuruga watoto wanakuwa kama digidigi manake baba Mtanzania,Mama Mganda,Watoto wana uraia wa Afrika kusini,wakati yy hajaukana uraia wa Uganda ila kwa makusudi kawapa watoto uraia wa SA.

Hiyo haitoshi unawapeleka watoto Kanisani,wakati baba yao muislam.
 
Ametaka tu mjue kuwa mnalipiwa kodi na mtu ambaye hawajibiki kwenye malezi ya watoto wake.
 
Ooohh kumbe shida ni urahia wa watoto....nimeanza kupata picha sasa.
Ndo maana nashangaa baba gani hajali watoto wake hata kidogo...sasa nimeelewa kilicho nyuma ya pazia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…