Zebra cake

farkhina

Platinum Member
Joined
Mar 14, 2012
Posts
14,568
Reaction score
16,917
Mahitaji
1)sukari (granulated sugar) 1cup
2) mayai 4
3)maziwa kikombe 1
4)mafuta ya kupikia(vegetable,corn au canola) kikombe 1
5)unga wa ngano 2 cups
6)1/3 vanilla ya unga au arki ya vanilla
7)dark cocoa powder 2 tablespoon
8)baking powder 1 tablespoon.


Namna ya kutaarisha

1)changanya sukari na mayai..tumia electric hand mixer au whisk beat kuchanganyia..hadi mchanganyiko uwe laini
2)weka maziwa na mafuta na endelea kuchanganya hadi vichanganyike vizuri
3)katika bakuli jengine changanya baking powder,vanilla powder na unga pamoja
4)weka huo unga kwenye mchanganyiko wako wa mayai na sukari...changanya
5)gawa mchanganyiko sehemu 2 sawa
6)sehemu moja iweke pembeni na nyengine weka cocoa yako na uichanganye vizuri..
7)mimina kwenye trey viwiko 3 vya mchanganyiko plain then weka vijiko 3 vya mchanganyiko wa cocoa...fanya hivo hadi imalizike...(usisubirie mchanganyiko usambae).
8)weka moto 300-350° hadi iwive vizuri

Zebra cake tayari kwa kuliwa...
 

Attachments

  • 1385483812789.jpg
    27.1 KB · Views: 1,726
  • 1385483825804.jpg
    33.8 KB · Views: 1,551
  • 1385483838245.jpg
    35.1 KB · Views: 1,713



Dada farkhina kwa mara ya kwanza nimekuweza leo hii na haunitishi ng'oo.....lazima nikupiku mapishi tu.
 
Last edited by a moderator:




Tafadhali lete maelekezo ya pilau.....natanguliza shukrani.
 

mashaallah,wajua kupika weye ila kuonjesha tu ndo hutaki...
 
Hii Keki ya Zebra itabidi mimi nitafute keki ya Simba maana hii keki ya Zebra itatupiga mateke sisi binadamu kasheshe kweli hongera keki ya Zebra.
 
Vipi red velvet? Ushawahi kuila hiyo? Wawekee recipe wadau waijaribu.

By far, my most favorite cake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…