Zengwe lagubika ziara ya Rais na wasanii; waratibu wadaiwa kufanya mchezo mchafu

Zengwe lagubika ziara ya Rais na wasanii; waratibu wadaiwa kufanya mchezo mchafu

Nifah

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2014
Posts
34,020
Reaction score
79,098
IMG_5450.jpeg

Mkono mtupu haulambwi!

Naam, ndivyo ninavyoweza kulielezea hili.

Wikiendi iliyopita Rais alijumuika kwenye uzinduzi wa albam ya msanii wa kizazi kipya Harmonize akiwa kama mgeni rasmi pamoja na wageni waalikwa wengine ambao ni viongozi na wadau wa tasnia ya burudani.

Katika uzinduzi huo Rais alitangaza rasmi ushiriki wa wasanii katika ziara zake ikiwemo ziara inayotarajiwa hivi karibuni nchini Korea ya Kusini, kisha kufuatiwa na ile ya Marekani.

Japo tangazo lake hilo lilikuja ikiwa tayari wasanii (waigizaji) walishaanza kufunga safari kuelekea nchini huko kabla ya Rais kuungana nao hapo baadaye.

Zengwe katika wasanii watakaosafiri na Rais
Kuna mchezo mchafu umefanyika katika nafasi za wasanii watakaoungana na Rais ziarani hapo. Safari hii ya Korea ya Kusini Rais ataambatana na waigizaji filamu.

Mkurugenzi wa bodi ya filamu nchini Dr. Kiagho Kilonzo anatajwa kufanya upendeleo kwa kupoka nafasi ya muigizaji mmoja mwanamama (jina linahifadhiwa kwa sasa) kisha kumuweka mwanadada mwingine anayedaiwa kuwa mpenzi wake.

Upendeleo huo wa waziwazi umewaumiza na kuwasononesha wengi, lakini Mkurugenzi hakujali hilo zaidi ya kuweka maslahi ya mpenzi wake mbele!
IMG_5509.jpeg



Kupitia chanzo changu nyeti,

Nifah.
 
Wingi wasanii ndio unafanya wengine wapate wengine wakose, raisi hawezi kwenda nao wote. Inawezekana hata huyu angeenda tu hata kama hana mahusiano na huyo mtu, sometimes ni bahati tu. Ni kama unavyoona kocha wa taifa stars anavyofanya selection ya kikosi cha timu Kuna ambao wataachwa tu

Kwa mantiki hiyo basi hii habari yako haina umuhimu wowote, sababu hakuna cha ajabu hapo
 
We Nifah vaa viatu vya mkurugenzi kama ingekuwa ni wewe ziara yenyewe matembezi tu ya hisani
Ningemchukulia usafiri binafsi, hoteli binafsi tule raha zetu wenyewe huko Korea sio kudhulumu nafasi ya mwingine.

Tukiwa huko sasa ndio ningetumia nafasi yangu ‘kumchomeka’ naye anufaike watakayojifunza waigizaji wenzie.
 
Wingi wasanii ndio unafanya wengine wapate wengine wakose, raisi hawezi kwenda nao wote. Inawezekana hata huyu angeenda tu hata kama hana mahusiano na huyo mtu, sometimes ni bahati tu. Ni kama unavyoona kocha wa taifa stars anavyofanya selection ya kikosi cha timu Kuna ambao wataachwa tu

Kwa mantiki hiyo basi hii habari yako haina umuhimu wowote, sababu hakuna cha ajabu hapo
Yani safari ilishapangwa na washiriki wakapangwa wakajiandaa kwa safari kisha baadae ghafla mshiriki anaondolewa anawekwa mwingine halafu unasema hakuna cha ajabu?
 
View attachment 3002202
Mkono mtupu haulambwi!

Naam, ndivyo ninavyoweza kulielezea hili.

Wikiendi iliyopita Rais alijumuika kwenye uzinduzi wa albam ya msanii wa kizazi kipya Harmonize akiwa kama mgeni rasmi pamoja na wageni waalikwa wengine ambao ni viongozi na wadau wa tasnia ya burudani.

Katika uzinduzi huo Rais alitangaza rasmi ushiriki wa wasanii katika ziara zake ikiwemo ziara inayotarajiwa hivi karibuni nchini Korea ya Kusini, kisha kufuatiwa na ile ya Marekani.

Japo tangazo lake hilo lilikuja ikiwa tayari wasanii (waigizaji) walishaanza kufunga safari kuelekea nchini huko kabla ya Rais kuungana nao hapo baadaye.

Zengwe katika wasanii watakaosafiri na Rais
Kuna mchezo mchafu umefanyika katika nafasi za wasanii watakaoungana na Rais ziarani hapo. Safari hii ya Korea ya Kusini Rais ataambatana na waigizaji filamu.

Mkurugenzi wa bodi ya filamu nchini Dr. Kiago Kilonzo anatajwa kufanya upendeleo kwa kupoka nafasi ya muigizaji mmoja mwanamama (jina linahifadhiwa kwa sasa) kisha kumuweka mwanadada mwingine anayedaiwa kuwa mpenzi wake.

Upendeleo huo wa waziwazi umewaumiza na kuwasononesha wengi, lakini Mkurugenzi hakujali hilo zaidi ya kuweka maslahi ya mpenzi wake mbele!

Kupitia chanzo changu nyeti,

Nifah.
Daaaa huyu jamaa mpare ni malaya balaaa Tangu namfahamu akifundisha pale Ilala
 
Back
Top Bottom