Ziara ya Rais wa Tanzania nchini China kuleta fursa mpya kwa maendeleo ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili

Ziara ya Rais wa Tanzania nchini China kuleta fursa mpya kwa maendeleo ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
微信图片_20221101103024.jpg
Mkuu wa Taasisi ya Confucius katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Aldin Mutembei, amesema, ziara ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan nchini China itaendeleza uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Profesa Mutembei amesema, ziara hiyo ya siku tatu kuanzia tarehe 2 hadi 4 itatoa fursa zaidi kwa maendeleo ya uhusiano wa nchi hizo mbili, na kupanua ushirikiano wa kibiashara kati ya China na Tanzania.

Profesa Mutembei amesema, China ni rafiki mkubwa wa Tanzania, na nchi hizo mbili zina fursa isiyo na mwisho katika kukuza ushirikiano wa utamaduni, uchumi na diplomasia.

Amesema maingiliano ya elimu yamekuwa na nafasi muhimu katika ushirikiano kati ya Tanzania na China, na hivi sasa, Kiswahili kinatumika katika taasisi za kitaaluma za China, hali ambayo imehimiza ushirikiano wa kina wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili na uwekezaji wa China nchini Tanzania.

Ameongeza kuwa nchini Tanzania, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na Taasisi ya Confucius, pia vimekuza ipasavyo ushirikiano wa Tanzania na China katika nyanja za uchumi, utamaduni na kilimo.
 
Huko hamna kingine Zaid ya bandari , tangu lini ngozi by yeusi ikawa na upeo kuzid ngozi nyeupe , huko ni za uso tuu Tanzagiza inaenda kupigwa , Kwa Gharama ya 10 % ya watu fulani.
 
Mutembei alijitahidi sana kufurukuta, lakini Magu hakumuona.

Ngoja tuone kama mama naye 'atamfungia vioo' kwenye teuzi zake.
 
Chawa Mwingine huyu anakuja kwa speed ya light! Natamani kuwajua, true identity!
 
Back
Top Bottom