Ziara yangu ofisi za JamiiForums

Ziara yangu ofisi za JamiiForums

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
966
Reaction score
6,019
Waziri Doroth Gwajima.jpg

Waziri Doroth Gwajima_Maxence Melo.jpg


Wasalaam Wanajukwaa wenzangu.

Mapema tarehe 12 Julai, 2024 nimetembelea Ofisi za Jamii Forums kama mojawapo ya taasisi inayojihusisha na habari za kijamii. Lengo la ziara ni kuweza kufahamu shughuli za taasisi hii na kuona namna ya kushirikiana Ili kupanua wigo wa kuifikia jamii kidigitali.

Kama Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, tumejadiliana kuhusu umuhimu wa kushirikiana kwenye mada za kuifikia jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo na ustawi wa jamii kwa ujumla na hususan, kupambana kutokomeza ukatili wa kijinsia na kwa watoto.

Kama mwanachama hai wa JF na aliyethibitishwa, niko tayari kuendelea kupokea mawazo na changamoto kutoka kwa wananchi kupitia mitandao ya kidigitali ambayo kimsingi inarahisisha sana mawasiliano na wananchi.

Hivyo, nawakaribisha nyote kunitumia mawazo mbalimbali na changamoto kwani, ushirikiano wa jamii ni muhimu kwa maendeleo.

Ahsante sana Mkurugenzi wa JamiiForums Maxence Melo (ninayesalimiana naye) na timu yako yote🤝

Mungu awabariki 🤝🇹🇿 na awabariki wanajukwaa wote🤝

JamiiForums_Doroth Gwajima.jpg

Waziri Gwajima_JamiiForums.jpg

Waziri Gwajima_JamiiForums.png

Maxence Melo_Doroth Gwajima.jpg

Doroth Gwajima_Jamiiforums Staff.jpg
 
Sisi kama Taifa, tunachangamoto kubwa sana kimaadili. Sisemei masuala ya ukatili au ushoga maana yanaongelewa sana. Ila nasemea maadili ya mtu mmoja mmoja kwa Taifa lake.

1. Watu wengi si waaminifu.
2. Watu wengi ni waongo waongo wamejaa uswahili uswahili sana.
3. Watu wengi wababaishaji sana
4. Vijana wanawaza kupiga madeal tu, hawataki kufanya kazi na kupata vipato halali
5. Watumishi wengi wa Serikali maadili yao ya kazi yapo ICU.

Najua tumechelewa ila bado tuna nafasi ya kusahihisha. Mwambie Rais afanye maadili ya nchi hii kuanzia ngazi ya familia iwe agenda ya Kitaifa. Kila Viongozi wanapoenda waifanye agenda hii kuwa agenda muhimu zaidi.

Ili tufanikiwe katika hili, viongozi wakubwa wawe vinara wa maadili mema. Endapo wao hawatabadilika na kuonesha njia tutatwanga maji kwenye kinu.

Narudia tena, maadili, maadili, maadili ya watu wa Taifa letu yapo ICU.

Fanyia kazi jambo hili mkuu. Wizara yako inayo nafasi. Tusiwaachie viongozi wa dini peke yao maana watu wa Taifa hili hawana muda na mambo ya Mungu kiviiile. Wao wambie miujiza tu. Bora kidogo mkisema nyie Viongozi wa Serikali mnaweza leta mabadiliko.

Pole kwa kusoma comment ndefu. Nimemaliza.
 
Back
Top Bottom