Zifuatazo ni Tabia 11 zitakazokupatia heshima kama utaishi nazo

Zifuatazo ni Tabia 11 zitakazokupatia heshima kama utaishi nazo

Nimemuelewa vizuri Sana ..

Hizo zote zinazungumzia Ustaarabu na huruma huruma...ili uheshimiwe..
Wengine ni nature yao... Kuwa na huruma, ustaarabu na kujiheshimu/kuheshimu pamoja na kuheshimiana na wengine.

Ficha ujinga wako. Inaonesha wazi ni mtu usiye na busara.

Kubwa jinga!
 
umenikwaza 🐒

hiyo no.7

mpira ni miongoni mwa mada za kipuuzi?🐒

awali ilikua ni kipindi cha lisaa1 tu, wadau wakapendekeza muda uongezwe kidogo, hivi sasa ni masaa3 tunajadiliana masuala ya mpira, na tunachombeza na tumichezo tudogotudogo, huu ni upuuzi kweli?🐒
Nchi zilizoendelea hukuti vigenge vilivyojaa nguvu kazi wakijadili mpira badala ya tathmini za kina za kujikwamua kimaisha na kupigisha hatua maradufu maendeleo ya nchi.

Mwingine ni ubishani wa Kipumbavu!
 
Mtu aishi kwa kadiri ya kiwango chake cha akili ..

Heshima haitafutwi , heshima inakuja automatically..
Na ikija automatically ujue hakuna heshima hapo... Ni wanafiki tu! Wanakuigizia na kukunyenyekea kwa sababu una kitu/vitu fulani
 
Na mwisho wa yote tafuta hela maana swaga bila impact maishani mwa watu ni porojo.
Sio kwamba iyo niliisahau ila sikuiweka tu kwasababu swala la kutafu pesa si la kuimizwa ni automatically utatafuta tu pesa😀
 
1. Siku zote simamia kwenye ukweli na uhalisia, usikubali kubali tu.

2. Ongea kwa ujasiri na uwazi, tena ongea kwa speed ndogo sio unaongea haraka haraka kama chiriku.

3. Unapo ongea na mtu rafiki au mpenzi Onyesha nia ya dhati usiongee tu kwa kumfurahisha, kuwa mkweli.

4. Unapokuwa sehemu yeyote ile hasa ugenini kuwa mpole "just calm down" ila jitahidi kwa na confidence.

5. Chukulia mambo kwa wepesi, furahia wakati ulio nao.

6. Sehemu yeyote ile utakayoenda jaribu kujitawala kwa kuonesha ujasili ulionao acha woga na aibu za kishamba.

7. Usipendelee sana kujadili mada za kipuuzi kama mademu, mpira, wasanii nk. Jadili mada ngumu zenye mashiko.

8. Usipendelee kumkatiza mtu anapo kuelezea au kusimulia jambo we kuwa tu makini kum sikiliza bila kumkatisha katisha.

9. Sikuzote chukulia mambo kwa wepesi, epuka kufikiri kupita kiasi.

10. Acha ubishi na kukosoa kosoa mambo jitahidi kudhibiti hisia zako.

11. Sikuzote usitake mafanikio ya haraka believe in process watu watakueshimu kama walishuhudia njia ulizotumia kupa uo utajiri.
Hata ufanye hayo yoote kwa 💯 kama hela huna wewe ni lofa tu! Cc: Mkapa CHADEMA
 
Ukiwa mpole sana napo tabu,kuna muha mmoja shamba boy katoka huko kwao michikichini hivi karibu, alikuwa akiwa na madem anapenda sifa, siku moja natoka zangu job nimebeba viazi vya chipsi kwenye ile mifuko laini transparent, nikamkuta dogo yupo kakaa na wake za wapangaji wenzangu ,alivyoona vile viazi akaanza shobo za kunitania oooh na we mwanaume mzima unakula chipsi?

Yule dogo hakuwahi niona nimekasirika ila siku hiyo alijuta kunishobokea, taratibu nilisogea pale walipokuwa wamekaa nikaanza kumpiga maneno ya karaha wale wanawake mwanzoni walikuwa wananishangaa coz hawakuwahi niona nikiwa kwenye mood ile, nilimpaka shombo sana yule dogo hadi wale madem ikafika hatua hawana mbavu ni mwendo wa kukenua meno tu,...tokea pale yule dogo mazoea na mm alikata tukikutana ni shikamoo bro imeisha.
 
Back
Top Bottom