Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Asante kwa jibu. Lakini unajua watu wengi wanamalalamiko kama hayo lakini hawana uwezo au hawajui JamiiForums na kuleta shida zao hapa? Sehemu wanayoweza kwenda ni ofisi za tanesco maeneo yao na huko ndo kwenye shida hasa. Hivi kweli tanesco hamna nguzo kweli? Mfano mkoa wa mwanza maeneo ya kisesa ilo ndo limekua jibu lao kila siku na ukienda au ukipita ofisini kwao hapo kijereshi nguzo zipo za kutosha zinapigwa jua tu. Hivyo ombi la tulio wengi ni changamoto za kwenye ofisi na wafanyakazi zishugulikiwe tu.
Tafadhali tambua kuwa zipo taarifa za mtu binafsi hizi zinatolewa na mteja mwenye kutaka huduma fulani kwenye makazi yake au taarifa za wengi pale ambapo kuna ombi au tatizo la eneo kubwa. Hivyo ikiwa taarifa inakuhusu wewe mwenyewe toa kwetu huku ukionyesha taarifa kamili kwa kuwa taarifa za kila mteja zipo kwenye mfumo wetu
 
Tafadhali tambua kuwa zipo taarifa za mtu binafsi hizi zinatolewa na mteja mwenye kutaka huduma fulani kwenye makazi yake au taarifa za wengi pale ambapo kuna ombi au tatizo la eneo kubwa. Hivyo ikiwa taarifa inakuhusu wewe mwenyewe toa kwetu huku ukionyesha taarifa kamili kwa kuwa taarifa za kila mteja zipo kwenye mfumo wetu
Nimekuelewa mkuu. Hongera kwa kazi nzuri
 
Upumbavu mtupu. Mmejaza taratibu kwenye karatasi ila utendaji wenu ni kila mtu anavyojisikia.

Nasema hivi, kama hamtaki kunipa surveyor basi bakini na umeme wenu uwalipukie mkakufee..

Mtu unafatilia utafikiri unapewa umeme buree..!!! Halafu chakushangaza ananifata dogo mmoja yupo kwenye planning ananiambia ukitaka tukufanyie haraka kuna malipo.

Hivi swala la surveyor linahitaji siku ngapi? Maana naingia wiki ya nne sasa, na site kwangu mpaka tanesco ni mwendo wa dk 6-9.

Narudia tena, kama hamtaki kunipa surveyor basiii.... nimefunga solar na sipungukiwi kitu, siku mkijisikia kuja mtanipigia simu. Siwezi kumnyenyekea mtu maana hamnifanyii bure.

TANESCO DODOMA.
Jina lako, Wilaya na namba ya simu tafadhali
 
Habari..hapo kwenye hatua ya TANO ya kufanya Malipo ndio tumekwama ni Wiki ya pili ka sio ya tatu kila tukieenda ofisn kwenu tunaambiwa Mtandao unasumbua yaani tatizo ni kutoa account namba yenu ya CRDB ili tuweze kufanya malipo kila tukienda mtandao unasumbua hii ni kweli au wanataka tutoe Rushwa, Nyumba iko Tabata Kisukuru .
HATUA YA KWANZA

MAOMBI YA MWANZO

Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?


Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)

JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?

Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.

VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU

1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.

2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.

3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)

4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.


5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.

6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.

7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu

HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU

Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo

1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)

2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.

3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme

4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)

HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)

Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.

HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME

Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

MAELEZO

Muda wa makadirio

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 7 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)

Ndani ya siku 10 za kazi

Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)

Ndani ya siku 14 za kazi

HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO

Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.

HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME

Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.

MAELEZO

Muda wa kufungiwa

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 30 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika

(mita 30- 100)

Ndani ya siku 60 za kazi

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

Ndani ya siku 90 za kazi

KWA MAULIZO WASILIANA NASI

Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400

Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz

Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu

Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu

Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
 
Meter ikishafungwa sehemu hata ukitaka kuhama huwezi kuihamisha labda iwe within the sama plot (yaani mfano mita ipo chumbani unataka kuihamishia barazani au kuna nyumba nyingine kwenye the same plot)

Kama unahamia kwingine hapo meter hurudi Tanesco na wewe huko unapohamia utafanya maombi yakupata meter mpya
Sio kweli, meter inahamishika ila iwe within same district
 
Nimesikia kuwa katika mkoa wa kilimanjaro wilaya ya moshi vijijini, marangu, samanga kuna ofa ya kuunganishiwa umeme kwa Tshs. 27000/= ikiwa nguzo iko ndani ya mita 30. Je ni kweli kuna ofa hiyo?

Pili naomba maelekezo ya kurudishwa tarif 1 maana nimeshajaza fomu na ni miezi 3 sasa hawajaja kukagua luku ili kujiridhisha.
 
HATUA YA KWANZA

MAOMBI YA MWANZO

Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?


Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)

JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?

Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.

VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU

1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.

2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.

3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)

4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.


5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.

6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.

7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu

HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU

Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo

1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)

2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.

3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme

4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)

HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)

Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.

HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME

Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

MAELEZO

Muda wa makadirio

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 7 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)

Ndani ya siku 10 za kazi

Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)

Ndani ya siku 14 za kazi

HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO

Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.

HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME

Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.

MAELEZO

Muda wa kufungiwa

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 30 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika

(mita 30- 100)

Ndani ya siku 60 za kazi

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

Ndani ya siku 90 za kazi

KWA MAULIZO WASILIANA NASI

Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400

Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz

Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu

Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu

Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
Maeneo gani hua mnapanga kwamba hapa itapita phase I au III, kigezo ni kipi ili upate phase III?
 
Unaomba jina la wilaya unadhani,utasaidia chochote,acheni porojo zenu za kutesa watu,yaani kuwasha umeme ndani ya mita 20( nguzo tayari) ndiyo ichukue miezi 3, kwendeni uko ,tumewachoka sana.
Tupo tayari kukusikiliza na kukuhumia mpendwa mteja wetu
 
Muda mnaochukua kufungia wateja umeme ni mrefu sana mimi nina miezi miwili tangu nilipie lakini hakuna dalili ya kuja kufungiwa ndio wanasema wamewafikia wateja wa mwezi wa 11/2018 sasa tuliolipia mwaka 2019 tutafikiwa 2021au
 
Wapuuzi kabisa mkuu, wamepitisha main line eneo yalipo makazi yangu leo mwaka wa tano hawataki kutandaza nyaya ndogo lakini badala wameenda kutandaza eneo la mbele.

Yaan assume starting point ni A then unaenda B, C, D etc sasa wao wameenda kutandaza point D na kuruka B na C. Hapa utawaelewa?
Inaelezwa kuwa kuna UTATU MTSKATIFU wa kuingiza majumbani umeme wa REA:
1. REA, mlipiaji wa gharama za miradi ya usambazaji wa umeme vijijini,
2. WAKANDARASI, watandaza nyanya, na
3. TANESCO, wasimamiji wa miradi sehemu husika.
Nguzo za nyaya za umeme usiopoozwa zimepitishwa uwanjani kwangu. Miti yangu mingi ilikatwa ili kuwezesha nguzo kujengewa. Nilikubali hiyo gharama nikiamini ningeneemeka kwa kupata huduma ya umeme.
Mkandarasi ameruka kitongoji changu kwenye kutandaza nguzo za nyaya za kuingiza umeme kwenye nyumba zetu.
* TANESCO wanatuambia hakuna cha mradi mwingine wa REA; II wala III.
* Wananchi wa kijiji cha Bisarwi, Manga, Tarime, hali zetu ni duni. Hatuna uwezo wa kulipia gharama ya mamilioni za maombi ya mradi wa kuwezesha kupata umeme:
(a) dhana ya umeme wa gharama nafuu iko wapi?
(b) kwanini tumekuwa wahanga wakati kama shirika, ofisi yenu ya wilaya haikusimamia ipasavyo utelekezaji wa mradi wa REA? Ushaidi:
- transfoma zilizowekwa ama ni ndogo, mbovu, au zilikuwa chache ikilinganishwa na mahitaji.
- ndiyo maana mkalazimika kibadikisha baadhi baada ya kulipuka, na
- kazi chini ya kiwango. Nimeshuhudia TANESCO wakirekebisha baadhi ya dosari kama kufunga earthwire.
Najiuliza: hapakuwepo na kipengele cha muda wa matazamio ya mradi kama Sheria ya Manunuzi ya Umma inavyotaka?
Sijapata muda wa kutosha kufuatilia suala hili.
 
Changamoto ni kitengo cha kupima, surveyor ni wachache mno kulinganisha na waitaji wa huduma hiyo. Waweza kaa hadi miezi miwili hujapimiwa. All in all asanteni kwa elimu
 
Dah Huo ujasiri wa tanesco nimeukubali..hii ni roho ya kisomali kabisa, umepata ujasiri wa kujibu kero za Tanesco, Tanesco mnakera sana nyie watu nahisi hata wafanyakazi hampati neema sababu ya laana za wananchi...Mimi kuna nguzo ipo pembeni ya duka langu...nimeomba mita mwezi wa pili sasa...duka lenyewe vyumba viwili tu..watu wakufanya survey ndio kila siku wanakuja j3...yaani j3 usipopitiwa imekula kwako....sasa najiuliza, inamaana hawa jamaa wanafanya kazi jumatatu tu? (kama una meter ya magendo sema nikupe hela uje unifungie tu..bila hivyo mwaka utaisha)
 
Jamaa anavyojibu kiutaratibu humu ni kama ndiyo walivyo field?watu wa hovyo sana hawa
 
Tangu tarehe 12 watu wanauliza maswali hawajibiwi, leo tarehe 21 mko kimya tu.

Watu wameuliza maswali wanahitaji msaada ila hamtaki kujibu mko kimya tu.
 
Back
Top Bottom