Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

WILAYA

ENEO

NAMBA YA SIMU TAFADHALI
 
Wilaya

Eneo

Namba ya simu


Tafadhali
 
Ipo siku Tanesco itakua inahangaika kuwatafuta wateja kama ilivyo TTCL leo. Wafanyakazi wa TTCL miaka ya 90 ulikua ukienda kuomba form ya kuwekewa simu, unaulizwa " Simu unataka we ya nini" but leo, mmh.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]eti we unataka simu ya nini?Kama ni Mimi ningewajibu na nyie mnauza simu za nini?
 
Aisee napoishi mita namba nikinunua umeme napewa mchache sana
Na matumizi yangu ni chini ya unit 2 kwa siku
Mfano 2000/= 5.7 unit
While nnachojua 2000/=14.... Unit

Sasa apo ni hasaraa
 
Mbona inaelekea kuna mgomo baridi,TANESCO wamekuwa wagumu sana kufungia watu umeme kwa hii rate mpya ya Sh.27,000.Nasema hivyo kwa kuwa upo ulalamishi wa wazi kutoka kwa watumishi wa TANESCO kwamba rate hiyo haina maslahi.And then mbona kiuhalisia bei ya kufungiwa umeme sio 27,000 ni 57,000,kwa kuwa ipo Sh.30,000 ambayo inabidi ulipe kwa mtu anayeitwa Contractor,wakati kazi ya huyo contractor haionekani kazi zote wanafanya TANESCO wenyewe?Huu si upigaji jamani.
 
Leo Sichangi Sana Nawasubiri Bado Siku Kazaa Hapo Mbele Umeme Walete Malipo Nimeshamaliza Na Rist Ya Benk Ninayo
 
WILAYA

ENEO

NAMBA YA SIMU TAFADHALI
Nilitegemea jibu kama hili maana huu takribani mwaka wa 3 kila nikijaribu kuelezea na kuleta maombi humu mimi huwa naambiwa kauli kama hii, ok namba nakupatia tena ni, 0684542853
 
Nilitegemea jibu kama hili maana huu takribani mwaka wa 3 kila nikijaribu kuelezea na kuleta maombi humu mimi huwa naambiwa kauli kama hii, ok namba nakupatia tena ni, 0684542853
Ndugu mpendwa mteja wetu tumekupigia simu yako haipokelewi,Je ni kijiji gani na wilaya tafadhali
 
Nashukuru sana ni kweli nimepigiwa sim sikuweza kuipokea nilikuwa kusali. Ni miaka mingi sana nilileta ombi langu la kuomba kusaidiwa suala la kupatiwa umeme wa REA kwenye kitongoji cha KIJUKA Kijiji Mabuye Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera. Kitongoji cha KIJUKA kiko Kaskazini Mashariki mwa Wilaya ya Missenyi ni mwendo wa km Kilometa mbili tu kutoka yalipo makao makuu ya wilaya ya Missenyi na ni kitongoji cha kwanza kutoka yalipo makao makuu ya Wilaya ya ya Missenyi ukiwa unaelekea kwenye kijiji cha Mabuye. Hiki kitongoji cha KIJUKA kimebaki kama kisiwa kimerukwa na hakijapewa umeme wa REA japo kina kila sifa ya kupewa Umeme wa REA. Tumejaribu kufuatilia lakini mpaka sekunde ya leo hakuna majibu ya kuridhisha Kibaya zaidi hata viongozi hawatupi ushirikiano ni sisi wananchi tunahangaika wenyewe. Tumeenda mbali tukapanga vijana tuunganishe nguvu tujivutie umeme lakini imeshindikana kumbe hatuwezi kutokana na gharama kuwa juu. Sasa tunaomba msaada tafadhali sana hiki kitongoji kipatiwe huduma ya REA. Aidha hata mimi nashukuru nimepigiwa sim kwa bahati mbaya nilikuwa kanisani ila nimepiga tena sikupokelewa nitafurahi kesho nikipigiea tena nitatoa ushirikiano.
0684542853
 
Tumewahi kukupatia maelezo mara kadhaa zidi ya eneo hili tutakupatia tena maelezo ya ziada
 
Biharamulo niliomba umeme tangu mwezi 02/2019 Hadi leo nimeishia kufanyiwa tathimini tu! Kila nikienda nazungushwa mara fomu haionekani, mara hakuna mtandao wa kutolea control number huu ni mwezi wa sita namba sipewi ili nikafanye malipo. Japo Kuna mtumishiwa wao sliniambia bila kutoa chochote nitasikia tu kwa majirani na Mimi hela ya kuwapa nje na malipo halali Sina. Sijui hata la kufanya.
 
Waziri wa nishati kasema ni marufuku kununua nguzo,kwa nn mlikuwa mnatuuzia nguzo?
 
Hawa Tanesco wa jamii forum hawana msaada kabisa ni simba aliyechorwa tu
 
Kwa nn Tanesco wanaweka matumiz makubwa kwa walioingiza Umeme three phase ikiwa matumiz ya mteja hayazidi unit 70 kwa mwezi????
 
Kiongoz, hili linafikishwa kwa Rais moja kwa moja, hawa watumishi wa tanesco haiwezekani watuchezee akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…