Sio sahihi dada, na walipokuwa wanavuta huo waya wewe haukuona?Mtoa mada naomba unisaidie. Kuna jirani yangu kaunganishiwa umeme. Lakini huo waya unaoenda kwa jirani yangu, nikisimama kwenye varanda maeneo ya jikoni, nakuwa na uwezo wa kuushika waya huo maana mimi niko kwenye mwinuko na huyo jirani yangu yuko bondeni. Hivi karibuni nilimkuta msichana wa kazi kaanika nguo juu ya waya huo wa umeme unaoelekea kwa jirani yangu. Je, hii ni sahihi? Maana naona kama inatishia usalama wangu.
Kama unahitaji mita ya ziada (meter separation) utaratibu ni huo huo kama wa maombi ya awali kama uzi ulivyoeleza.Naomba unipe utaratibu na vianavyohitajika katika mita za ziada.
Mkuu ili kufungiwa umeme kuna vifaa vinahitajika hivyo kukiwa na upungufu wa hata material ya aina moja huwezi kufungiwa mpaka yakamilike hivyo Tanesco nao wanapenda kupata wateja wapya ili shirika lipate mapato na sio kwamba wanachelewesha makusuditanesco mda mwingine mnasema uongo, sijui kama mmebadilika au la!!!
mwaka jana, eneo langu ilikua karibu na nguzo mita 15 ila imechukua hadi siku 60 baada ya kufanya malipo,
ni kwamba mmejirekebisha au ni kuridhisha umati,
asante
Fika ofisi ya Tanesco katika eneo unaloishi kisha utapewa utaratibu wa kufuata, gharama utajua surveyor akishafika site na kupima kisha kufanya estimatesGharama za kuvuta umeme umbali wa mita 350 ni kiasi gani?
Sio kweli mkuu.. Ma surveyor sio wala rushwaTanesco kuna viumbe wanaitwa surveya ni wala rushwa pasipo mfano..
HATUA YA KWANZA-:- MAOMBI YA MWANZO
Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?
Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)
JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?
Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.
VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU
1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.
2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.
3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)
4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.
5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.
6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.
7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu
HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU
Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo
1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)
2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.
3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme
4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)
HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)
Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.
HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME
Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:
MAELEZO
Muda wa makadirio
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 7 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)
Ndani ya siku 10 za kazi
Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)
Ndani ya siku 14 za kazi
HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO
Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.
HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME
Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.
MAELEZO
Muda wa kufungiwa
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 30 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika
(mita 30- 100)
Ndani ya siku 60 za kazi
KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)
Ndani ya siku 90 za kazi
KWA MAULIZO WASILIANA NASI
Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400
Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz
Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu
Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu
Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
Anaomba nyaya hizo kuhamishwa ndiye anayewajibika kulipia gharama za kuhamisha nyaya hizo.Swali kama mtu amejenga chini ya nyaya za sevis line nani anawajibika hapo
Ndio inawezekana ila kwenye mchoro huyo contractor awe registered na anayetambulika na shirika.Asanteni kwa ufafanuzi mzuri, naombeni mnisaidie swali hili hapa chini,
Kwasasa mimi nipo dodoma, ila nina nyumba ipo dar nimeshafanya wire-ring tayari ila process za mchoro bado, je kama process za kuomba umeme nikizifanyia uku dodoma, na mambo ya mchoro nikayafanyia uku uku itawezekana?
Gharama za ku separate meter ni sawa na gharama za s/l mpya. Bei yake inategemea ni meter ya aina gani (single phase au three phase) na upo sehemu gani (kijijini au mjini)Gharama ya separeti mita za chumba kimoja zipo, na kama zipo ni kiasi gani mteja anatakiwa kulipa ila afanye matumizi ya kiwango cha chini cha nyumbani?
1. Kuhusu meter ngapi hapo huwezi kusema mpaka surveyor afike site na kuangalia mazingira yalivyokaa na namna gani ata design ili uweze kupata huo umemeNaomba usikimbie. Tujibu baadhi ya maswali japo machache:
1. Ni meter angapi maximum mtu atahitaji nguzo? (Yaani nguzo iliyopo hadi kufika ktk nyumba). Naomba maelezo hapa, kwani hapa ndio mafundi wa TANESCO hutupigia hela. mf ni 30m -70m au 30m to 100m? au 30-70m ni kile chuma tu bila nguzo kati ya 30m -100m?
2. Je ni sahihi ktk mfumo wa leo mtu kufunga/kuweka Cut-Out ktk meter kabla ya umeme kuingia ndani? (Japo ndani kutafungwa Circuit Breaker)
3. Naskia sijui Two Phases au Single Phase. Je ni mfumo upi ni mzr kwa matumizi ya nyumba ya makazi?
Note: Umesema Jedwali, lipo wapi sasa?
Ahsante sn mkuu.1. Kuhusu meter ngapi hapo huwezi kusema mpaka surveyor afike site na kuangalia mazingira yalivyokaa na namna gani ata design ili uweze kupata huo umeme
2. Cut out inafungwa baada ya meter kabla ya umeme kuingia kwenye main switch ambayo itakuwa na Circuit Breaker. Kuweka Cut Out sio lazima ila ukiweka ni sawa.
3. Kuhusu umeme wa single phase au three phase inatagemea na load yako. Load inamaanisha mahitaji yako ya umeme. Mfano unatumia taa ngapi, fridge ngapi, labda una pump ya maji, una cooker, una tv ngapi, una ac ngapi.
Hapo contractor wako wa umeme anataefanya wiring ya nyumba yako ndio ata calculate load yako na akipata total KW unazohitaji ndio ita determine unahitaji single au three phase..
Hivyo hakuna kusema eti umeme wa single au wa three phase ndio mzuri hapana. Aina ya phase unayowekewa inatokana na load yako. Mara nyingi ukiwa na load kuanzia 14kW kwenda juu hiyo ni three phase ina maana kushuka chini ni single phase.
Na huwezi kuwekewa three phase ukiwa na load ndogo kwakuwa umeme wa three phase una Volts kuanzia 400 wakati single phase ni 220- 200 Volts.
Hivyo basi ukiwekewa umeme wa Volts 400 wakati una load ndogo inaweza kupelekea vitu vyako kua overloaded na kuungua na ukiwekewe umeme wa volts 210 wakati load yako ni kubwa basi usishangae ukiwasha ac haziwaki mara cooker haliwaki maana umeme unakuwa mdogo. Asante
hongera kwa kulisaidia shirika.1. Kuhusu meter ngapi hapo huwezi kusema mpaka surveyor afike site na kuangalia mazingira yalivyokaa na namna gani ata design ili uweze kupata huo umeme
2. Cut out inafungwa baada ya meter kabla ya umeme kuingia kwenye main switch ambayo itakuwa na Circuit Breaker. Kuweka Cut Out sio lazima ila ukiweka ni sawa.
3. Kuhusu umeme wa single phase au three phase inatagemea na load yako. Load inamaanisha mahitaji yako ya umeme. Mfano unatumia taa ngapi, fridge ngapi, labda una pump ya maji, una cooker, una tv ngapi, una ac ngapi.
Hapo contractor wako wa umeme anataefanya wiring ya nyumba yako ndio ata calculate load yako na akipata total KW unazohitaji ndio ita determine unahitaji single au three phase..
Hivyo hakuna kusema eti umeme wa single au wa three phase ndio mzuri hapana. Aina ya phase unayowekewa inatokana na load yako. Mara nyingi ukiwa na load kuanzia 14kW kwenda juu hiyo ni three phase ina maana kushuka chini ni single phase.
Na huwezi kuwekewa three phase ukiwa na load ndogo kwakuwa umeme wa three phase una Volts kuanzia 400 wakati single phase ni 220- 200 Volts.
Hivyo basi ukiwekewa umeme wa Volts 400 wakati una load ndogo inaweza kupelekea vitu vyako kua overloaded na kuungua na ukiwekewe umeme wa volts 210 wakati load yako ni kubwa basi usishangae ukiwasha ac haziwaki mara cooker haliwaki maana umeme unakuwa mdogo. Asante
Karibuhongera kwa kulisaidia shirika.
Cut-out ni kifaa cha umeme ambacho kina unganisha cable ya umeme ya tanesco na wiring ya mteja. Yaani hapa ndipo pale umeme wa tanesco unakutana na wiring system ya mteja inapoanzia.Ahsante sn mkuu.
Eti matumizi ya Cut-Out ni yapi ndg?
Meter ikishafungwa sehemu hata ukitaka kuhama huwezi kuihamisha labda iwe within the sama plot (yaani mfano mita ipo chumbani unataka kuihamishia barazani au kuna nyumba nyingine kwenye the same plot)Asante sana TANESCO kwa maelezo na majibu mujarabu kabisa.
Labda nami nikuulize kitu kimoja.
Iwapo nimekodi eneo la biashara mfano ofisi na nikalazimika kufunga mita yangu ya umeme ili kuepusha usumbufu na watumiaji wengine. Na iwapo mita hiyo ipo kwa jina langu kwa malipo niliyofanya mwenyewe baada ya kukubaliana na mwenye jengo au eneo kwa utaratibu ulioueleza kwenye uzi wakohapo juu. Je pindi nikitaka kuama eneo au ofisi, ninaruhusiwa kumtafuta fundi wenu aweze kuniamishia mita yangu kwenda kunifungia mahali pengine ninapotaka kuhamia? Au ukishaifunga mita basi haihamishiki tena. Maelezo tafadhali