ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Sasa huwezi kuamini juzi nimeenda South Africa nikakuta audio CD orijino ya vijana jazz ya 1975 wakitumia style ya koka koka.
imerekodiwa ujerumani na ina nyimbo 12 ukiwemo ule wa Niliruka ukuta.


Wanaiuza bei gani?
 
Milima ya Kwetu 1 - Super Rainbow Band (Utunzi wake Eddy Sheggy, waimbaji Eddy Sheggy na Emma Mkelo 'Lady Champion')

Nikitazama milima ya kwetu ee,
machozi yanitoka kwa uchungu na mawazo,
tulitoka wawili ninarudi peke yangu,
baba na mama wataniuliza bibi yako yuko wapi ee,
Ndugu jamaa wataniuliza bibi yako yuko wapi eee,

japokuwa ninakaribia kufika nyumbani ee,
Ninatamani gari isifikie upeesi,
kwa ile aibu nitakayopata mbele ya wazazi ii,
kwa vile ni miezi michache imepita nilitoka na bibi yangu,

(Eddy)
Nitasema nini kwa baba mimi najuta aa,
kwa pesa zake nyiingi alizopotezaa,
harusi ilifanyika kwa gharama kubwa sana,
watu walikula na kunywa na kusaza mamaa,

Nikaenda kuishi na bibi yule mjini,
kazi yake ilikuwa ni vituko,
nikaenda kuishi na bibi yule mjini kazi yake ilikuwa ni vitiimbwi,

Alianza kuweka sukari kwenye mboga,
nikaonja haviliki tukalala na njaa,

kafuatia na kuweka chumvi kwenye chai,
nilikuwa na wageni wakatoka bila kuaga,

kafuatia kuchelewa akienda sokoni,
nikimuuliza anitukana hadharani aibu,

kuna gari imekuja hadi mlangoni,
kujitetea akasema mjomba wake kaja,

hivi juzi kavunja kioo cha dirisha,
apate kuchungulia wapitao njiani,

hatimaye kunibeza na kunidharau,
shikamoo ikaisha ikabaki
Vipi babu, mambo zakoo ee x2

Nilishindwa kumuuliza ee sikutaka kumuudhi,
sababu nilikuwa nampenda nampenda saana x 2

chorus:

walisemaa dalili ya mvua ni mawingu,
niliyempenda kanitoroka mama,

(Eddy Sheggy)
Nilinyang'anywa tonge mdomoni,
nilinyang'anywa tonge kinywani,
niliyempenda kanikimbia mama yoyo,
niliempenda kanikimbia masikini nifanye nini mama,

(chorus)

Vituko ee, vituko vya bibi huyoo,
sitaweza kusahau mimi oo mama ee,
sitaweza kusahau mimi oo sheggy ee,
alikuwa kama helikopta, ndege isiyochagua mahali pa kutua ee,
kila mtaa hapa mjini jamani tazameni oo,
ana bwana mmoja ama wawili mama mama oo,
nifanye nini mama oo,

(chorus)
Yani kipande hiki cha hapa nilikuwa na wageni wakatoka bila kuagaaaa! kinanikumbusha siku naangalia final euro 2008 Spain vs Germn final,mimi pekee nilikuwa nasapoti Spain wote wenzangu walikuwa German sasa Torres akawafunga halafu karibia mpira unaisha huu wimbo ukapigwa basi na wengi wao wakaanza kuondoka mmoja mmoja bila kuagaaaaa! samahani lakini nimeingiza mada ya soka.:heh:
 
Oh baba mapenzi ya pesa kaka ni ya shida kwelimkwa mbele ya wandugu dada nakuambia yote lakini mapenzi ya pesa si ya kweli dada aa dada aa,waniumiza roho oh Tabu Ley na Mbilia Bel intro hiyo anaejua vizuri amalizie
 
Official Vijana Jazz Orchestre known as Sagarumba Air Pamba Moto distributed by Viva Conscious arts Presenting ..Its Tanzanian music Gerned Rhumba .enjoy and rate it ..
+255712845804
+255756694227
Its Official Number of VIJANA JAZZ BAND source: Joseph viva Stephen wa Youtube- Vijana Jazz Orchestre (Sagarumba Air Pamba Moto)-
 
Last edited by a moderator:
Salama wakuu?,ni jumapili nyingine tulivu....

Leo naomba tujikumbushe bendi zetu zilizotamba sana miaka ya 80 na 90,bendi ambazo ama zimekufa ama zinaendelea kusuasua na ambazo ukisikiliza muziki wake leo hii unatamani ungerudisha wakati nyuma.......

Kwa kuanzia tuanze na hawa Orchestra Vijana Jazz,bendi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Umoja wa vijana wa CCM,bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo ya Sindimba,Hekaheka,Heka koka,Watoto wa nyumbani,Air Pambamoto(awamu ya kwanza na ya pili) na baadae mtindo wa Saga Rhumba.....

Kwangu mimi bendi hii ndiyo ilikuwa chaguo langu hasa......Ukitaka kuujua ukali wa bendi hii sikiliza nyimbo kama Chiku,Mary Maria,Penzi lamea penye penzi,Shemeji,Bujumbura,Ilikuwa lifti,Tambiko la Pambamoto,Adza(Aza),Ngapulila,Ogopa Tapeli,Mwisho wa Mwezi,Penzi haligawanyiki,Wivu,Malaine,Nyongise,Shoga,Theresa,V.I.P,Mama Chichi na nyingine nyingi tu tamu....

Bendi hii imewahi kuundwa na wanamuziki kama Hemed Maneti 'Chiriku',Hamza Kalala 'Komando',Manitu Mussa,Issa Chikupele,Hassan Dalali,Hassan Shaw,Ally Jamwaka,Abuu Semhando,Bakari 'Baker' Semhando,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya zege',Eddy Sheggy,Shaban Yohana 'Wanted',Rashid Pembe 'Profesa',Kida Waziri,Beno Villa Anthony,Rahma Shally,Jerry Nashon 'Dudumizi',Suleiman Mbwembwe,Shaban Dogodogo,Aggrey Ndumbalo,John Kitime,Abdallah Mgonahazelu,Freddy Benjamin,Mohammed Gotagota,Said Hamis 'Misukosuko',Athumani Momba na wengine kibao...
Kaka unatisha enzi hizo ni noma
 
Mark Africa Band - MATUKIO source: markafricaband wa youtube
 
Last edited by a moderator:
Super Kamanyola Band wakiendeleza ''Sendema ya Moto' muziki wa dansi ya iliyokuwa Maquiz Orignal, wakiwa ndani ya ukumbi wa Villa Park Resort, Jijini Mwanza wakifanya vitu vyao chini ya Parashi, Roy Mukuna na wengineo: source: 00051 Avondje stappen Anne Kuijs wa youtube : Live music in Villa Park, Mwanza Jarmo wa youtube
 
Last edited by a moderator:
Da, vijana Jazz usipime wandugu. Ule uliluwa muziki hasa wa Ki-Tanzania. Bantu Group nayo ilikuwa hatari. MCA International,Bimalee, Washirika Tanzania Stars, DDC, Juwata/OTTU, ZAITA Musica, Police kutaja chache.
 
Balantanda, thank for this great thread, angalau nimepata nafasi ya kukumbuka nyimbo zetu za ujanani. Hivi kuna mtu anaweza kuwa na lyrics ya wimbo: Mazoea yananikondesha? Nimeona mtu mmoja humu amejaribu kuuandika lakini ameishia njiani. I would real like to get it. Thanks wakuu!

Sory kwa kuchelewa kujibu mkuu wangu sana Mnyalu..........

Huu hapa wimbo wa Mazoea yananikondesha kutoka kwa Mzinga Troupe utunzi wake Issa Mrisho amb aye pia ndiye aliimba wimbo huu....


Mazoea yananikondeshaaaa eeeeee,
Nimpendae kachukuliwa eeeh mamaaa,
Wala sina la kutamka, wenye nguvu wamerudia eeeh!,
Wala sina pa kushitaki, wenye nguvu wamerudia eeh eeh...

Tuliishi bila matatizoo, nyumbani vitu teletele wallahi oooh,
Kama mimi nina kasoro wandugu natakanijulishweeee,
Aaaah, kwa ninimumezoea kunichukulia nimpendaeee.....

Daima hakutenda ovu wala sikutenda ovu lililoacha makovu ya kutokusahau mileleeee....

Aaah, sikutenda ovu la kuweza kulipwa kisasi, wala hakutenda ovu la kutokusahau milele,
Oooh, tuliishi kwa mapendo mamaaaa aaah aaah....

Mazoea, mazoea yananikondeshaa.....

Kinachonifanya nisemee, sio sifa ya uzuri wake tuuu,
Ama sitopata zaidi yake aaah aaah,
Ama nimeshakula kizizi labda lakini siamni,
Alijua matatizooo, kweli nasema mtoto kalelewaa....

Kinachonifanya nimuwazee, sio sifa ya upole wake tuu,
Ama sifa zake nyingine aaah, hapana alijua matatizoo,
Kwa haki nasema Mungu amjalieeee,
Walimwengu mama eeeh eeeh, walitaka niteterekeee....

Mbona mjusi ama Kinyonga, anapata riziki yake,
Tena hula vijidudu hai, hasa vyenye kurukaruka,
Mbona yeye hana mbawaa, hana makucha wala vikumboo,
Hashiki panga wala bundukii, masikini eeeh, unamtosha ulimi wakee,
Sembuse mimi mwanadamuuuu.....Mazoea yananikondesha eeeh eeeh.....

Mbona mjusi ama Kinyonga, anapata riziki yake,
Tena hula vijidudu hai, hasa vyenye kurukaruka,
Mbona yeye hana mbawaa, hana makucha wala vikumboo,
Hashiki panga wala bundukii, masikini eeeh, unamtosha ulimi wakee,
Anakula kwa ulimi wakee, anashiba kwa ulimi wakee,
Anapata riziki kwa ulimi wakee,sembuse mimi mwanadamuuuu.....

 
Laah, aisee kali kweli balantanda umetukumbusha mbali.
 
Sory kwa kuchelewa kujibu mkuu wangu sana Mnyalu..........

Huu hapa wimbo wa Mazoea yananikondesha kutoka kwa Mzinga Troupe utunzi wake Issa Mrisho amb aye pia ndiye aliimba wimbo huu....


Mazoea yananikondeshaaaa eeeeee,
Nimpendae kachukuliwa eeeh mamaaa,
Wala sina la kutamka, wenye nguvu wamerudia eeeh!,
Wala sina pa kushitaki, wenye nguvu wamerudia eeh eeh...

Tuliishi bila matatizoo, nyumbani vitu teletele wallahi oooh,
Kama mimi nina kasoro wandugu natakanijulishweeee,
Aaaah, kwa ninimumezoea kunichukulia nimpendaeee.....

Daima hakutenda ovu wala sikutenda ovu lililoacha makovu ya kutokusahau mileleeee....

Aaah, sikutenda ovu la kuweza kulipwa kisasi, wala hakutenda ovu la kutokusahau milele,
Oooh, tuliishi kwa mapendo mamaaaa aaah aaah....

Mazoea, mazoea yananikondeshaa.....

Kinachonifanya nisemee, sio sifa ya uzuri wake tuuu,
Ama sitopata zaidi yake aaah aaah,
Ama nimeshakula kizizi labda lakini siamni,
Alijua matatizooo, kweli nasema mtoto kalelewaa....

Kinachonifanya nimuwazee, sio sifa ya upole wake tuu,
Ama sifa zake nyingine aaah, hapana alijua matatizoo,
Kwa haki nasema Mungu amjalieeee,
Walimwengu mama eeeh eeeh, walitaka niteterekeee....

Mbona mjusi ama Kinyonga, anapata riziki yake,
Tena hula vijidudu hai, hasa vyenye kurukaruka,
Mbona yeye hana mbawaa, hana makucha wala vikumboo,
Hashiki panga wala bundukii, masikini eeeh, unamtosha ulimi wakee,
Sembuse mimi mwanadamuuuu.....Mazoea yananikondesha eeeh eeeh.....

Mbona mjusi ama Kinyonga, anapata riziki yake,
Tena hula vijidudu hai, hasa vyenye kurukaruka,
Mbona yeye hana mbawaa, hana makucha wala vikumboo,
Hashiki panga wala bundukii, masikini eeeh, unamtosha ulimi wakee,
Anakula kwa ulimi wakee, anashiba kwa ulimi wakee,
Anapata riziki kwa ulimi wakee,sembuse mimi mwanadamuuuu.....

Thanks a lot mkuu. Kwa hakika huu wimbo huwa unaniburudisha sana, kwa namna ulivyoimbwa na ujumbe. Good composition. Sijui tutawapata wapi akina Mrisho wengine miaka hii ya leo.
 
Odama Band ikitoa burudani ya muziki wa dansi jijini Dar-es-Salaam, Aug 10, 2013 kwa cover wimbo original 'AFRO' wa Simba Wanyika Source: Ahmad Michuzi wa youtube.
 
Last edited by a moderator:
Halafu walikuwepo MK Groups watoto wa Maghorofani(New Afica hotel) wana Ngulupa tupatupa Dansi chini ya uongozi wake Kasongo Mpinda 'Clayton',hawa jamaa walikuwa wanatisha sana sikiliza nyimbo zao kama Nishike mkono,Mariam Mary,ama ule 'Kibela acha chuki,chuki yaleta ugomvi,Kibela acha chuki,chuki yaleta migonganoo,ooh ooh Kibela' na nyingine.

Bila kuwasahau MK Beats wana Tukunyema(mpaka chini mpaka chini) chini ya uongozi wake mzee Shem ibrahim Kalenga akiwa na vijana wake akina Malick Star na Sisco Lunanga(waliondoka MK Beats hawa wakaenda kuanzisha Lulu Band ya Kanda Bongo Man iliyokuwa na makazi yake pale La Prima Victoria chini ya uongozi wake Connie Karanja)..Enzi hizo ilikuwa ni mambo ya Tukunyema tu,wowowo...Tucheze wote ooh tuche wote tukunyema aah tukunyema wa Tabora ooh tucheze wote Tukunyema aah...Au Tukunyema tukunyema mpaka chini mpaka choniii,wowowoooo...Mambo ya Belaombwe..dah,si mchezo yaani...Mnayakumbuka mambo ya Mzee Kistuli na wowowo????

Hapa naona umemsahau mzee King Kiki....🙂
 


Yaani hiki kitu kimekaa sawa mno, hawa so-called producer wa Bongo fleva wanatakiwa wawe wanasikiliza hizi rare gems....:A S-fire1:
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Umeona eeh! Msondo ngoma hao banaaa!!! Kitu kimepangika na kimetulia mnooo, siyo hizi Bongo Fleva.



Yaani hiki kitu kimekaa sawa mno, hawa so-called producer wa Bongo fleva wanatakiwa wawe wanasikiliza hizi rare gems....:A S-fire1:
 
Last edited by a moderator:
Umeona eeh! Msondo ngoma hao banaaa!!! Kitu kimepangika na kimetulia mnooo, siyo hizi Bongo Fleva.




Mkuu
Ngoma hii nayo imetulia, yaani hapa unaweza tengenezea hawa vijana wa b-fleva beat moja kali sana, unafanya loop/sample ya hilo pini kuanzia hapo 0:08 min (tan tan tatanh tan tan tantaah tan tan tataaah), unacombine na rythm guitar inayoanzia 1:03 weka hi-hat na drums tulivu na vichombwezo viwili vitatu basi umemaliza....kijiwe cha BET nominations hicho lol...

Sijui huwa wanasilikiliza nini hawa vijana...:tape:
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Msondo ngoma ni kama Zaiko Langa langa ya Congo.mziki umetulia
 
Mshenzi mkubwa wee, nyinyi ndio mnaoua wenzenu kwa wizi wenu. Unaziuza umeziimba wewe?

Na wewe unayetafuta nyimbo, nenda dukani. Hizo nyimbo sio ZILIPENDWA, bado zipo madukani.

Zilipendwa ni enzi hizo za kina Muba, Salum Abdallah, Daudi Kabaka na wakongwe wengine.

Quban Marimba, Tabora Jazz, Moro Jazz, Mwenge Jazz n.k

Nakuacha na kipande hii moja ya Muba.....Dr. Kleruu

''Oooh Dr. Kleruuu, ukalale pema kiongozi wetu shujaa.......''
''Mwanamapinduzi, kalale pema kyongozi weetu shujaa...
Kifo chake dokta, kimetusikitisha sisi wakulima wote woye......


Mkuu hizo Nyimbo hazina mwenyewe zipo free sababu zamani hatukuwa na sheria kali na wanamuziki wa zamani walikuwa wakiimba kama sehemu ya starehe tu na sio Biashara sana RTD ndio waliwaingiza mkenge wakiwaambia kama wanataka sawa kama hawataki wasepe wengi walikubali ili wasikike tu.... pesa walikuwa wakizipata kwenye live tu so hadi sasa huyo anayesimamia atakuwa ni mwizi tu.... unaposema aende dukani akanunue hizo pesa zitaenda kwa nani?
 
kuna wimbo unasema:-

Naikumbuka siku ileeee ulipokuja asubuhi na mapema,
ukifoka kwa ukali , kwamba ni mimi niliyetaka vunja ndoa yako.

Namshukuru baba mwenye nyumba,
aliyelizua panga lako,
lisishuke maungoni na kunipa kilema cha maisha.

Chorus:-

ukweli ulikuja kwa hasira sana (ehhh bwana ehhh)
bila kufahamu undani wa mambo yenyewe.


wimbo huo nautafuta sana, sikumbuki jina lake wala walioupiga

Haya kazi kwako mkuu Bujibuji
 

Attachments

Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom