ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Jamaa(Jerry Nashon Dudumizi) alikuwa mtunzi kwelikweli wa nyimbo za mapenzi hasa akiwa na Bima Lee na Vijana Jazz...

Angalia kama kitu hiki kitamu hapa chini ambacho ni utunzi wake..

V.I.P-Jerry Nashon 'Dudumizi"


(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,

(Dudumizi): Si maji wala Soda vitakavyozima kiu yangu,ila ni wewe VIP,
Si maji wala Soda vitakavyozima kiu yanguuu,iila ni weweeeee,VIP
Baada ya kazi ngumu ya kutafuta pesa,na kisirani cha kufokewa na boss,
Nahitaji VIP wa kunibembeleza,nakutaka wewe mama,unibembeleze,
Si kwa maneno ila kunitomasatomasa,kwa mikono yako laini yenye bangili,
Unipe busu mwanana la kunipumbaza wee (VIP).

Baada ya kazi ngumu ya kutafuta pesa,na kisirani cha kufokewa na boss,
Nahitaji VIP wa kunibembeleza,nakutaka wewe mama,unibembeleze,
Si kwa maneno ila kunitomasatomasa,kwa mikono yako laini yenye bangili,
Unipe busu mwanana la kunipumbaza wee (VIP)

(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,
Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo.

Dudumizi: VIP sogea karibu,ubipe busu mwanana mama

(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,

Bridge

(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.
Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka


Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP,
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP
Natamani penzi live sio penzi la ndotoni,nakuomba uwe wangu VIP,
Tafadhali nakusihi, ili niondokane na ndoto za mapenzi.

(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.
Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka


Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP,
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP
Natamani penzi live sio penzi la ndotoni,nakuomba uwe wangu VIP,
Tafadhali nakusihi, maaa mamaa,maaa....maaa yoooo,maa mamamaaaaaaaaaaaaaaa,
Tafadhali nakusihi, ili niondokane na ndoto za mapenzi.


Dudumizi: Ukinikubali VIP,mimi niko tayari,kubadili dini,
Ukinikubaliii VIP mimi niko tayari,kubadili dini,
Hata kama wazazi wangu hawapendi,nitafanyafanya mipango niwe na wewe sambamba(sambamba)
nitafanyafanya mipango niwe nawee sambambaaa

(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.


Ukinikubalii VIP,mimi niko tayari kubadili dini,
Ukinikubalii VIP,nitatoa mahaliii ya mbuzi saba,
Hata kama sina VIP,nitafanyafanya mipango niwe na wewe sambamba(sambamba) nitafanyafanya mipango niwe na wewe
sambamba.

(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.



sasa hivi maproducer mavi watakopi haya maandishi na kuharibu kabisa kwenye fleva.
 
Vijana walikuwa juu sana katika muziki hata upigaji na mpangilio wao wa vyombo tofauti kabisa na hizi bendi zilizokuwa zinajiita wazee wa muziki Bongo. Nyimbo za Vijana zilikuwa tamu sana mpaka sasa na ndiyo bendi pekee iliyopitiwa na wapiga solo hatari sana hapa nchini, nani anabisha?
 
kabla ya mwaka 2000 vijana ilikua juu kuliko ottu ebu sikiliza vibao kama tereza, mvuvi kinda, mwisho wa mwezi, bujumbura, aza, shingo feni mfano ile albam ya top quine kunzia muziki wa kwanza mpaka wa mwisho huwezi kukaa isipokua mama wa kambo tu
 
jamani kama kuna mtu anavibao vya tereza na mvuvi kinda maana mjaruo jery nashon dudumizi alitisha RIP wekeni hapa jf tu download
 
jamani kama kuna mtu anavibao vya tereza na mvuvi kinda maana mjaruo jery nashon dudumizi alitisha RIP wekeni hapa jf tu download

Nenda youtube kuna jamaa anaitwa "eddie nassor" ana library nzima ya RTD, mwimbo wowote anakuwekea , kie kie kie
 
kuna wimbo wa mzee makassy siujui jina lake lakini ndani yake kuna mistari hii
"mtoto wa arusha mama mbona wanipa shidaa, mchana na usikuu nakuwaza wewe, warembo wengi nimewaona mamaa, lakini roho yangu imekupenda wewe.............
mapenzi ya pesa hayadumu mamaa, mapenzi ya kwelii ni ya maisha, nimekupenda na wewe umekubali, tukila kisamvu kaza roho mama, daresalam jiji umbea mwingi

Huo wimbo unaitwa Hanifa.
 
Mie kulikuwa na bendi nyingi sana ambazo zilikuwa zinanikuna sana baadhi tu ni Msondo, Ngide, Western Jazz, Marquiz, Dar Jazz, Vijana, Jazz na nyingi nyinginezo ambazo kwa kweli muziki wao ulikuwa ni moto wa kuotea mbali kulinganisha na huu muziki wa siku hizi "Bongo Flava" pamoja na kuwa kuna nyimbo chache nzuri lakini mie Mhhhhh! bado haujanigusa kihivyo ukilinganisha na muziki wetu kabla ya Bongo flava. Sikilizeni hawa jamaa wa kule Tanga walijiita Jamhuri Jazz vibao vyao vilikuwa vitamu sana

http://www.youtube.com/watch?v=Va2zVgFM80o

Simba Mwituni - YouTube

WOOOOOOTEE MME TAJA BENDI NYINGI LAKINI KIBOKO YA BENDI ZOTE ni moja tuu , WAZEE WA KAZI , TABORA JAZZY!!!!!, nani anabisha????????
Acha kabisa segere matata segua segua, iko vile bwana.
 
vifo vingi hutokea kwa kukosa misaada na kutomudu gharama za matibabu....................DDC MLIMAN PARK
 
Wanaofahamu naomba wanijuze kuna wimbo wa vijana jazz unaitwa Stella ni Stella yupi aliyeimbwa maana Hamza Kalala na Hemed Maneti wote wamezaa na wanawake tofauti wenye jina hilo.
 
Wanaofahamu naomba wanijuze kuna wimbo wa vijana jazz unaitwa Stella ni Stella yupi aliyeimbwa maana Hamza Kalala na Hemed Maneti wote wamezaa na wanawake tofauti wenye jina hilo.
Habari yako Chifu...

Ameimbwa Stella Cheyo, binti wa Mzee Mapesa John Cheyo ambaye sasa ni mke wa Komando Hamza Kalala....

Wimbo ni utunzi wa Komando Hamza Kalala na uliimbwa na Vijana Jazz chini ya Hemed Maneti Ulaya (R.I.P)...

Stella - Vijana Jazz

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu wewe ni wangu, Stella eeeh,
Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu wewe ni wangu, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio tumebaki tunaulizana ndugu kwa ndugu, mtoto wa Kisukuma ulivyolelewa,
Hata jirani zangu dirishani nimewasikia wakikusfu kwa ukarimu, Stella eeeh,
Kutokana na uwezo mwingi walionao wazazi wako wengi wao huwa wangeringa....

Hata jirani zangu dirishani nimewasikia wakikusfu kwa ukarimu, Stella eeeh,
Kutokana na uwezo mwingi walionao wazazi wako wengi wao huwa wangeringa....

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu ya sura nzuri, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio Kalala nabaki mi najiuliza hata Msai nitamueleza siku nitakayofika Mwanza,
Miezi mitatu ya majaribio hata mama yangu amekusifia hata Ilemela nitawaeleza siku nitakayofika huko,
Stella eeh, eeeh, Stella eeh, eeeh, Mwadilaa, Stella eeh, eeeh....

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu ya sura nzuri, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio Kalala nabaki mi najiuliza hata Msai nitamueleza siku nitakayofika Mwanza,
Miezi mitatu ya majaribio hata mama yangu amekusifia hata Ilamela nitawaeleza siku nitakayofika huko,
Stella eeh, eeeh, Stella eeh, eeeh, Mwadilaa, Stella eeh, eeeh....

Nikupe nini ee, nikupe nini ee, nikupe nini ee mayo wee,
Nikupe nini ee nasema cha kukupa sina iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee...

Nikupe nini ee, nikupe nini ee, nikupe nini ee mayo wee,
Nikupe nini ee nasema cha kukupa sina iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee...

Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....
Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....
Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....
 
Habari yako Chifu...

Ameimbwa Stella Cheyo, binti wa Mzee Mapesa John Cheyo ambaye sasa ni mke wa Komando Hamza Kalala....

Wimbo ni utunzi wa Komando Hamza Kalala na uliimbwa na Vijana Jazz chini ya Hemed Maneti Ulaya (R.I.P)...

Stella - Vijana Jazz

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu wewe ni wangu, Stella eeeh,
Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu wewe ni wangu, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio tumebaki tunaulizana ndugu kwa ndugu, mtoto wa Kisukuma ulivyolelewa,
Hata jirani zangu dirishani nimewasikia wakikusfu kwa ukarimu, Stella eeeh,
Kutokana na uwezo mwingi walionao wazazi wako wengi wao huwa wangeringa....

Hata jirani zangu dirishani nimewasikia wakikusfu kwa ukarimu, Stella eeeh,
Kutokana na uwezo mwingi walionao wazazi wako wengi wao huwa wangeringa....

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu ya sura nzuri, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio Kalala nabaki mi najiuliza hata Msai nitamueleza siku nitakayofika Mwanza,
Miezi mitatu ya majaribio hata mama yangu amekusifia hata Ilemela nitawaeleza siku nitakayofika huko,
Stella eeh, eeeh, Stella eeh, eeeh, Mwadilaa, Stella eeh, eeeh....

Sio kwamba ninakusifia eti kwa sababu ya sura nzuri, Stella eeeh,
Miezi mitatu ya majaribio Kalala nabaki mi najiuliza hata Msai nitamueleza siku nitakayofika Mwanza,
Miezi mitatu ya majaribio hata mama yangu amekusifia hata Ilamela nitawaeleza siku nitakayofika huko,
Stella eeh, eeeh, Stella eeh, eeeh, Mwadilaa, Stella eeh, eeeh....

Nikupe nini ee, nikupe nini ee, nikupe nini ee mayo wee,
Nikupe nini ee nasema cha kukupa sina iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee...

Nikupe nini ee, nikupe nini ee, nikupe nini ee mayo wee,
Nikupe nini ee nasema cha kukupa sina iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee...

Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....
Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....
Iliyobaki mimi na wewe tu tuoanee....


Mimi mzima sana mwanajangwani mwenzangu.

Nashukuru sana kwa kunijuza na kisha kuniwekea vionjo halisi, kwa kweli huu wimbo naupenda sana japo ni miongoni mwa nyimbo ngumu sana kuziiga uimbaji kwa jinsi mpangilio wake wa maneno ulivyo. Kuna wimbo umeimbwa na UDA jazz kwa lugha ya kimwera unaitwa 'Tulele tubone' sina uhakika kama nimetamka sawa naupenda mno lkn sijui maana ya ujumbe wake kama unaufahamu mwaga hapa pia kuna wimbo wa Dar International 'Siwema part 2' maarufu kama 'Sadiki' naomba mashahiri yake kama unao.
 
Angalia kibao kitamu kama hiki cha Tancut Almasi...

Ninakwendaa safari, safari yenyewe safari ya kikazi,

Ninajuaa mama utabakiii, watasema mengi,
Pia wabaya wetu mamaa watafurahii x 2

Ninakwendaa safari, safari yenyewe safari ya kikazi,

Ninajuaa mama utabakiii, watasema mengi,
Pia wabaya wetu mamaa watafurahii x 2

Ninakwendaa safari, safari yenyewe ya masafa marefu,

Ninajuaa mama utabakiii, watasema mengi,
Pia wabaya wetu mamaa watafurahii x 2

Ninakwendaa safari, safari yenyewe ya masafa marefu,

Ninajuaa mama utabakiii, watasema mengi,
Pia wabaya wetu mamaa watafurahii x 2

Lakini usisikie yaoo mama watoto oo,……………..,

Nakwenda kutafuta maisha ya watoto wetu…………….,

Chunga watoto wetu mamaa nitarudi, tutaonana kwa mapenzi ya Mungu,
Chunga watoto wetu mamaa nitarudi, tutaonana kwa mapenzi ya Mungu,

Safari sio kifoo o mama iyeye,
Subiri nitarudii o mama watoto,
Safari sio kifoo o mama iyeye,
Subiri nitarudii o mama watoto,

Nikirudi mamaa nitakuletea zawadi,
Nikirudi mama nipokee kwa mikono miwili

Iyeye, oo mama iyee,

Nikirudi mamaa nitakuletea zawadi,
Zawadii nono, mama watooto.


(a keba, keba, keba, keba, keba, keba, keba, kebaaa,)
(fimbo, fimbo, fimbo, fimbo, lugoda,lugoda, lugoda, lugoda - Mangalaa..



Asante mdau, kila nikisikia wimbo huu namkumbuka kipenzi changu Frank.
Tuliachana jioni, asubuhi akasafiri, njiani akapata ajali na kufariki dunia.
Huwa nikienda live band lazima niombe huu wimbo, huwa nausikiliza kwa hisia kali sana.
Asante Balantanda.....umenikumbusha mbali sanaaa.
Ohhhhh.....Frank, safari kwako imekuwa ni kifo.
Sijui lini utarudi....dahhh!!!!!, mdau, unaniliza ujue.
 
Last edited by a moderator:
ndugu nyimbo zote nimezikubali mno, PIA nia shida na nyimbo ya salum abdallah aliyoimba na cuban malimba band iitwayo "mkono wa eidd"
 
Halafu walikuwepo MK Groups watoto wa Maghorofani(New Afica hotel) wana Ngulupa tupatupa Dansi chini ya uongozi wake Kasongo Mpinda 'Clayton',hawa jamaa walikuwa wanatisha sana sikiliza nyimbo zao kama Nishike mkono,Mariam Mary,ama ule 'Kibela acha chuki,chuki yaleta ugomvi,Kibela acha chuki,chuki yaleta migonganoo,ooh ooh Kibela' na nyingine.

Bila kuwasahau MK Beats wana Tukunyema(mpaka chini mpaka chini) chini ya uongozi wake mzee Shem ibrahim Kalenga akiwa na vijana wake akina Malick Star na Sisco Lunanga(waliondoka MK Beats hawa wakaenda kuanzisha Lulu Band ya Kanda Bongo Man iliyokuwa na makazi yake pale La Prima Victoria chini ya uongozi wake Connie Karanja)..Enzi hizo ilikuwa ni mambo ya Tukunyema tu,wowowo...Tucheze wote ooh tuche wote tukunyema aah tukunyema wa Tabora ooh tucheze wote Tukunyema aah...Au Tukunyema tukunyema mpaka chini mpaka choniii,wowowoooo...Mambo ya Belaombwe..dah,si mchezo yaani...Mnayakumbuka mambo ya Mzee Kistuli na wowowo????


Idd Mubarak!
Daa! Nilikuwa sijafuatilia kona hii kwa umakini kama leo!
Mimi kuna wimbo wa MK GROUP ni kitendawili kwangu kama jina lake lilivyo! Unaitwa KITENDAWILI. Nafikiri ni akili ya hali ya juu ilitumika.
Hebu nipe shule!! Ni ushirikina kweli?
Nikitembea nasikia mwanangu ananiita
niligeuka hamijibu jamani, walimwengu siyo wemaa!
Yoo mama yo
 
jamani, huku ndani kuna audio ya hiba - bitchuka? maana nimeangalia sana sijaona
 
Enzi hizo...

10425184_900973249929166_8355511666834209320_n.jpg
 
Back
Top Bottom