Zimbabwe: Wakamatwa kwa kuuza tiketi za kwenda mbinguni

Zimbabwe: Wakamatwa kwa kuuza tiketi za kwenda mbinguni

macho_mdiliko

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2008
Posts
25,191
Reaction score
48,765
image3.jpg


Tito and Amanda Watts mtu na mkewe, walikamatwa mwishoni mwa wiki kwa kuuza ''ticket za dhahabu za kwenda mbinguni'' kwa mamia ya watu. Wanandani hawa, waliokuwa wanauza tiketi hizo kwa dola za kimarekani 99.99 kwa kila tiketi, huku wakiwaambia wanunuaji kuwa zilikuwa zimetengenezwa kwa dhahabu halisi na kila tiketi ilikuwa na uwezo wa kumpeleka mtu mbinguni-- mara ukionyesha hii tiketi kwenye lango la mbinguni unakuwa umefika, walidai.

Polisi wazungumza:
''Hatukatazi watu kuuza tiketi za kwenda mbinguni'' msemaji wa polisi wa eneo la Jacksonville alisema

''lakini hawa ndugu walifanya ulaghai '' Tiketi zilikuwa ni miti iliyopuliziwa rangi inayofanana na dhahabu huku zikiwa zimeandikwa ''Tiketi ya kwenda mbinguni- jinyakulie moja''. Huwezi kuuza kitu unachosema ni dhahabu kumbe sio. Hapa ndipo hawa wanandani walipovuka mpaka''

Tito kwenye maelezo yake kwa polisi aliandika:

"Sibabaishwi na wanachokisema polisi. Hizi tiketi ni dhahabu halisi na sio kweli kuwa nimepulizia rangi. Ni Yesu mwenyewe aliyenipa pale nyuma ya mgahawa wa KFC huku akiniambia nikauze ili nipate fedha za kwenda anga za juu.

"Kwanza nilikutana na kiumbe wa sayari nyingine anayeitwa Stevie ambaye aliniambia kuwa kama nikiwa na fedha ataninyakuwa mimi na mke wangu kwenye ungo wake unaopaa mpaka kwenye sayari yake ambayo imeumbwa kwa cocaine tupu. Nitaweza kuvuta unga wa cocaine kadiri nipendavyo... tena bila malipo.

Jaribuni kumpeleka mtu asiye na hatia jela ndio mtakiona cha mtema kuni. Kama ni kukamata basi akamatwe Yesu kwasababu ndio yeye aliyenipatia hizi tiketi na kuniambia nikauze. Niko tayari kumrikodi kwa kificho ili ukweli ujulikane"

Mke naye alijitetea:

"Nia yetu ni kuondokana na dunia hii tuende zetu anga za juu tukavute unga wa cocaine.

Sijafanya chochote. Mume wangu ndio alikuwa anauza hizo tiketi za dhahabu za kwenda mbinguni. Mimi nilikuwa mwangaliaji."


Polisi wanasema waliwakamata na zaidi ya dola za kimarekani 10,000 taslimu, mabomba matano ya kuvutia unga na mamba mdogo.

Couple Arrested for Selling "Tickets to Heaven" | CelebTriCity
 
jamaa kweli ni mtata,....hebu mwachen amrekodi huyo Yesu kwa kificho ili angalau tumsikie hata sauti yake tu
 
Hahahaaaaa hahahaaaaaaa Hahhaahahahaha dunia ya Mola hii basi tu! Unawauzia watu tiketi za kwenda mbinguni ili upate pesa Za kwenda anga za juu ukavute cocaine bure

Hawa ni wagonjwa na wakiachwa wanaweza kusababisha maafa makubwa kwakuwa nyuma yao kuna kundi kubwa linawaamini!imagine wamekutwa na cash dola elfu10 tasilim
 
Kumbe hata wazungu wenyewe wanatesana imekaaa poa sana hiyo
 
Nilisoma habari za hawa jamaa, nikasikitika sana sana.
 
Kila nikizitafakali akili za hao waliokuwa wakinunua tiketi hizo nashindwa kuelewa kuwa walikuwa wanatumia kiungo gani cha mwili kufikiria hadi kufanya maamuzi ya kununua tiketi....
KWELI DUNIA MSONGAMANO...
 
Hivi ni mazingaombwe au kweli?Ama kweli huo ni upumbavu uliotukuka;Mwanadamu mwenzako anakuuzia ticket ya kwenda mbinguni,na unanunua?Mbinguni utakwenda kwa imani yako tu,imani itakayotokana na dini unayoabudu,au imani za wapagani nao wana utaratibu wa kuabudu.Leo uuziwe ticket ya kwenda mbinguni,UPUUZI WA HALI YA JUU.Kununua tickets hizo
 
Kila nikizitafakali akili za hao waliokuwa wakinunua tiketi hizo nashindwa kuelewa kuwa walikuwa wanatumia kiungo gani cha mwili kufikiria hadi kufanya maamuzi ya kununua tiketi....
KWELI DUNIA MSONGAMANO...

Nadhani vichwani kwao kuna vinyesi;tuwaombee kipindi hiki cha pasaka,walikuwa wanafanya mambo bila wao kujua wanafanya nini.Pengine ilikuwa ni mazingaombwe watu wakaingia kichwakichwa kununua.Maana hata hata mateja huwa yanaogopa kufa.Iweje mtu na akili zako binafsi ununue ticket ya kwenda mbingun?Labda ilikuwa fools day sawa.
 
Back
Top Bottom