Zimebaki siku nne tu kwa mujibu wa katiba kumtangaza, kuthibitishwa na bunge na kuapishwa kwa Makamu wa Rais

Zimebaki siku nne tu kwa mujibu wa katiba kumtangaza, kuthibitishwa na bunge na kuapishwa kwa Makamu wa Rais

Naona lukuvi akiwa ana ulinzi wa kificho sijajua atakua na post ipi.
 
Wakuu

Kuanzia tarehe 17/3/2021 mpaka leo ni siku kumi. Kwakuwa katiba inatamka ndani ya siku 14 makamu awe amepatikana, basi sasa rais na chama wamebakiwa na siku 4 kutuletea makamu.

Niwatakie kila la heri na watuletee mtu mwenye uwezo.
Katiba inamtaka Rais aliye apishwa kuteua makamu wake ndani ya siku 14 tangu alipo apishwa
 
🤣🤣 Nimecheka sana!!, Wizara ya afya inakoelekea kama hazitachukuliwa jitihada za haraka kuinusuru tunaenda kuipoteza. Gwajima+Mollel,, sijui jiwe alifikiriaga nini au ndio kutokushauriwa
Combination ya hovyo kupata kutokea.
Wapigwe chini mapema sana.
 
Mpaka kufikia jana kuna mahali niliweza kusikia tetesi halisi za majina pendekezwa, mpaka sasa ni majina mawili tu kwa uhakika yaliyokuwa yanafanyiwa vetting, na niliposikia hayo majina nilistaajabu, maana hakuna hata mmoja miongoni mwao anatokea kwenye kundi la watu wanaotajwa sasa au kuwahi kusikika kwenye majukwaa ya kisiasa hapa Tanzania.

Nimesita kuandika hayo majina hapa kwa sababu ya kulinda bahati zao. Nahisi kusemwa semwa mitandaoni kunaweza kuwaharibia, na mmoja kati yao ni mtu niliyewahi kufahamiana naye kwa karibu siku za nyuma.
Ni kweli kabisa,hawapo kabisa kwenye ubashiri wa watu(kutajwa tajwa)
 
Binafsi nilikuwa namuona January kwenye hiyo nafasi ila tangu wadau wanitolee macho kuwa jamaa haitawezekana kutokana na dini, basi karata yangu nairusha kwa Nchimbi, hata nikititazama utendaji wake alipokuwa kiongozi wa UVCCM na jinsi anavyokijua chama, hapo naona kabisa anaweza kupata nafasi.
Hatutafut kiongoz wa chama tunatafuta kiongoz wa nchi izo cv za ccm hatuzitak
 
Binafsi nilikuwa namuona January kwenye hiyo nafasi ila tangu wadau wanitolee macho kuwa jamaa haitawezekana kutokana na dini, basi karata yangu nairusha kwa Nchimbi, hata nikititazama utendaji wake alipokuwa kiongozi wa UVCCM na jinsi anavyokijua chama, hapo naona kabisa anaweza kupata nafasi.
Kigezo cha dini kimefanyaje? Tangu lini Tanzania kukawa na kigezo cha dini kwenye teuzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anaitwa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, alizaliwa Kilimatinde, Manyoni, Singida. Baba yake (Mchungaji na Mwalimu) ni Mgogo na mama yake (Mwalimu) ni Mkaguru wa Kilosa.

Baadae wazazi wake walihamia Mvumi Makulu, Chamwino, Dodoma.
Mtashuhudia vituko..
 
Back
Top Bottom