Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Anazikwa huko huko zinarudishwa nguo, viatu na vitu vingine alivyokuwa navyo mfungwahivi ikitokea mfungwa amefariki huko magereza....je anazikwa hukohuko au mwili wanapewa ndugu wakazike..?
Notorious thug ungetuambia nini sababu ya wewe kufungwa gerezani
ungemuacha tu ajibu mwenyewe.Sababu ya yeye kufungwa sioni kama ni critical hapa maana kila mmoja kule hufikishwa kwa sababu ambazo hazifanani na za yule, kila mmoja ana lake kule, cha msingi nikuomba Mungu akuepushe na huko na hata ikitokea uko kule basi walau hizi A b c alizotoa jamaa angalau zitakuongoza japo nahisi hata hizi ni sawa na bure, uhuru tulionao huku inje nimeona kumbe ni mkubwa mnoo, kama wafungwa huku uraiani wanapaita Ulaya [emoji23][emoji23][emoji23], basi tutembee kifua mbele.
Nitaelezea vitu viwili ambavyo vinapeleka watu wengi jela
9-- usipende vya watu.Gerezani ni sehemu ngumu sana na isiyoelezeka kwa mambo yaliyopo kule ili kupunguza makali ya gerezani unaweza fanya haya mambo.
1-Mfungwa hachagui gereza ni kweli ila unaeza kuchagua gereza wengi wanapohukumiwa huingia gerezani hapa unaeza kutambua gereza ulilopo ni la kilimo au vipi kama ni la kilimo fanya juu chini wewe na ndugu zako uhamishwe hapa ni wewe kusuka mipango na mabwana wakubwa toa fungu ndugu yangu utafia shambani. Bora ukae gereza la mjini huku kazi ni ndogo ndogo magereza ya kilimo ni mateso kazi ni ngumu vifaa butu askari wakali nyapara hawana huruma mbele bunduki nyuma fimbo.
2-Hela ya kula. Gerezani mlo ni mmoja saa nane achana na uji mlo wa gerezani ni kukufanya usife njaa ila sio mlo wa kula mwanadamu wakuu sasa hapa unaweza kuacha hela kwa mapai kwa mwez ukawa unapata msosi kutoka kwa wake za wadau wa pale ongea na ndugu zako angalau waache laki kwa mwezi kama inawezekana usijepata vidonda vya tumbo.
3-Nidhamu. Gerezani nidhamu unafundishwa kwa lazima ila watu sugu wapo pia epuka makundi gerezani utapata shida sana kuna wafugwa wao ni watata labda kuzaliwa au makabila kuna mfugwa alikua ni Mmasai kabila huyu alikua si mwelewa anaeza akaanza kkushambulia muda wowote kutokana na msongo wa mawazo na namba aliyokula kutoka ni 2035 watu kama hawa usijenge urafiki nao akili hua zinafyatuka.
4-Uongozi. Hapa namaanisha upate kitengo kizuri jikoni hua ni ngumu ila unaweza kupata uongozi wa kuongoza wenzako mnapokua kazini simaanishi uwe nyapara hapana unyapara unapewa kwa kuangalia muda uliokaa gerezani na nidhamu yako, hapa nazungumzia kusimamia genge mnapokua kazini kumbuka gerezani kazi ni nyingi na watu ni wengi muhimu ni wewe upatee nafasi ya kuwasimamia vinginevyo mikono itaota sugu na ngozi itapigwa jua kama la mbarali.
5- Marafiki. Anzisha urafiki na askari gereza ambaye labda ni kabila lako lafudhi hazipotei utaweza kumgundua huyu atakusaidia utakapokua mgonjwa au kwenye mambo mengine madogomadogo, askari mara nyingi hua wakali sana ila hamna mwanadamu anayekosa chembe chembe ya huruma atakusaidia kwa kujua huyu ni wa nyumbani. Pia kuna viongozi wa dini ambao ni wafugwa pia hawa watakusaidia kiroho na kukushauri ni watu muhimu pia.
6-Punguza mawazo. Hamna jambo gumu kama kuishi mbali na familia baba,mama,dada,kaka,mke na watoto utakua unawaza sana kuhusu maisha yao na pengo lako jipe moyo sana na jione bado wewe ni mtu kwenye jamiii. Unapokua na kifungo cha chini ya miaka30 ina maana bado una nafasi ya siku moja kutoka gerezani na kuendelea na maisha yako kma zamani usiangalie mwaka utakao toka utakata tamaa wewe amini tyu nitatoka siku si
7-Jifanyie usafi, linda afya yako. Ngozi yako epuka kushare share baadhi ya vitu unapokua kule ndani namaanisha sabuni na vitu vingine unavyokua navyo kwa siri. Jipende usijisuse ni hali ya muda soon utarudi ulaya(uraiani)
8- Usipende kudadisi wenzako mambo yao au kesi zao acha wao wakuambie vinginevyo wewe pambana na yako,wakili wako endelea kua na mawasiliano nae kupitia ndugu zako kuandaa mikakati ya rufaa na mambo mengine.
N:b. Ni haya machache wadau najua mna mengi karibuni tuendelee kupeana uzoefu na mbinu kwa waliokaa na ambao hawajakaa kila mtu ni mfugwa mtarajiwa tumekaa tumetokaa huenda tukarudi WHO KNOWS!!
Inaonekana unauzoefu na magereza ya tzMaweni naona ndio gereza gumu sana kutokana na location yake ilipo utapiga sana kokoto kwenye jua pale wafugwa wengi pale wametoka magereza ya karanga(kilimanjaro) na kisongo(arusha) hawa ni wa vifungo virefu na wale wa pale tanga kule shuruba ni nzito sana wafungwa wa kunyongwa wapo pia pale wengii tyu (condemn) maweni hata askari magereza ni wakali sana upekuzi ni kila muda na vipigo ukienda kule mwezi utapauka na kua mweusi tiii kutokana na joto,kazi,mrundikano wakuu gereza la maweni ndio gereza naloliogopa kuliko yote tanzania likifuatiwa na gereza la songwe na gereza lililopo ruvuma!
Ukihukumiwa miaka kadhaa jela na viboko mfano 12 wakat wa kuingia na 12 wakati wa kutoka kinacho fanyika kwanza hawakupigi Hadi uende kwa daktari upimwe afya athibitishe kuwa ni mzima wa afya na kwamba unaweza kumudu viboko baada ya hapo ndo unatembezewa kichapoMkuu embu naomba uniambie kuhusu adhabu ya mboko inayoambatana na kifungo kirefu.
Mfano mheshimiwa Sabaya amefungwa jela na kuhukumiwa kulambwa mboko kadhaa, sikumbuki idadi na wakati huo kakata rufaa.
Swali linakuja: je hizo mboko hutembea siku ya ngapi tangu uingie gerezani kuanza kutumikia kifungo?
Na je kwa mtu aliyekata rufaa hutembezewa mboko hata kabla ya rufaa yake kusikilizwa?
Ni hayo tu.
Jitahidi***** nilikaa siku 5 pale madale MAHABUSU
Sitaki shida na jamhuri
Labda itokee tu bahati mbaya Kama ilivyotokea.
Hahaha sana utapigwa runguNi bora ukutane na Simba ukurarue ufe uishe kuliko uwe mtovu wa nidhamu gerezani.
Yani kwakifupi gerezani chunga heshima babangu,ukijitoa akili maji utatamka"bhaji"kama una mafua hivi.
PoaNaomba unitag mkuu kama hutojalj
Sabaya kitakachomsumbua ni kua chini ya amri kufuata taratibu apa itamsumbua sana ila kifedha ataishi najua lazima atapewa cheo flanSidhan kama Sabaya ataweza kuyafuata haya
Jitahidi
Gerezani ni lazima ufanye kazi ukishakua mfugwa tena kwa nguvu hata wanaoumwa mara nyingine wanafanya kazi wanaambiwa wanasingizia kuumwa kupga kazi ni amriMkuu mimi nilifikiri ukifungwa unaondolewa uhuru wako na unatakiwa kupewa mahitaji yote ya msingi kama binadamu isipokuwa ule uhuru wako wa kuchangamana na watu wengine, je, ni sahihi wafungwa kufanya kazi wakiwa gerezani endapo hukumu zao hazikueleza kwamba wanapewa kifungo na kufanyishwa kazi, ziwe nyepesi au kazi ngumu. Mwenye uzoefu wa mataifa mengine anaweza kutupatia pia....
Ugopa kesi ya mauaji kwanza balaa linaanzia ukiwa kituo cha polisi pale ni msala utateswa hadi ufike mahabusu ya gerezani ushaivaMiaka mitatu iliyopita nilifahamiana na ndugu mmoja wa mwenye nyumba wangu kigamboni, jamaa alikua ana muonekano wa kihuni na kiteja. Nilikuja kufahamu kua jamaa alikaa gerezani kwa zaidi ya miaka 7 kwa kesi ya mauaji yeye pamoja na wenzake.
Jamaa alikua anatembea kama mlemavu, hyo ilitokea kipindi akiwa jela baada ya kuvunjwa mguu na askari magereza, anasema kisa cha kuvunjwa mguu ilikua ni fujo walizoanzisha gerezani. Jamaa anasema kama kuna kitu cha kuogopa sana kwa mfungwa ni fujo na utovu wa nidhamu gerezani.
Miezi mitatu kabla ya kufariki aliwahi kukutana na yule askari aliyemvunja mguu mitaa ya posta yalipokuepo makao makuu ya jeshi la magereza. Jamaa anasema alionana uso kwa uso na poti alishangaa kumuona jamaa yupo nje kwa msamaha wa Rais.
Alipomkumbusha kisa cha kumvunja mguu poti alijibu "nilikua kazini nikitimiza majukumu". Kuna msemo unasema 'ugali mtamu lakini sio wa jela.