Zipi ni alama za kuwa umefanikiwa kimaisha?

Zipi ni alama za kuwa umefanikiwa kimaisha?

Kwa Angle nyingi tu,

Mfano mtu akiweka malengo ya kuacha pombe na akafanikiwa kuacha hayo ni mafanikio kwake coz ametimiza lengo lake,
Mtu akiwa na lengo la kununua Baiskeli na akainunua hayo ni mafanikio yake,ndio maana nikasema kua mafanikio ni kutimiza malengo uliojiwekea coz binadamu tuna malengo tofauti tofauti,

Donald Trump ni tajiri ila alikua na lengo la kugombea urais wa US,baada ya kushinda ikawa ametimiza lengo lake,so hapo amefanikiwa,ni mafanikio kwake kwa kutimiza lengo lake.
Nilitaka uongee namna hiyo💪
 
Mafanikio ni ile level ambayo mtu humtegemei mtu mwingine kwenye basic need za kibinadam hapo tyr ushafanikiwa mana unaweza lea familia bila shida ss kama hata kula yako tu tabu hata kama una amani na upendo hujafanikiwa bado
 
Mafanikio ni ile level ambayo mtu humtegemei mtu mwingine kwenye basic need za kibinadam hapo tyr ushafanikiwa mana unaweza lea familia bila shida ss kama hata kula yako tu tabu hata kama una amani na upendo hujafanikiwa bado
Well,ndiyo mana nkasema nikiwa na kipato cha akiba cha kuweza kulisha familia mwaka mzima....

And binadamu kutegemeana ni jambo lisiloepukika,,,,
 
Kwangu mimi mafanikio ni kuwa na uwezo wa kufanya chochote unachotaka, na kuenda mahali popote unapotaka muda wowote unaotaka, ilimradi haumdhuru mtu wala hauvunji sheria za nchi
Nakubali, utajiitaje umefanikiwa ila hauna financial freedom..

Huwezi kula unachokitaka

Huwezi kuhimili medical bills kwenye hospitali zinazoeleweka

Huwezi kusafiri kwa usafiri unaoupenda

Savings zinawekwa ili ziliwe next month

Haya sio mafanikio Ila ni kupiga hatua tu kwenye maisha

Lakini pia kufanikiwa yaweza kumaanisha fullfillment inayotokana na mtu kufikia malengo aliyoyatamani. Maana kuna wengine wanapenda umaarufu, kusaidia watu au kuweza kuishi kutokana na vipaji vyao etc

Kwa hiyo wewe unaweza kumuona hajafanikiwa Ila amepata fullfillment aliyoitaka. So, hata hayo ni mafanikio
 
Maisha ni ubatili mtup
Only if it was Just a statement, but unfortunately it's not, that's the reality 🙂🙂
maisha ni ubatili mtupu- hii kauli huwa inaongelewa na WATU ambao hawajafika hatua inaitwa Self- actualization ambao hawajazigusa jamii zao kwa njia chanya


Ya duniani na mbinguni yote katoa Mungu hivyo every day is a gift from God. To say life is illusion inafikirisha.
 
Kufanikiwa hakuna maana inayojulikana moja kwa moja, hili swali litajibiwa Kutokana na mtazamo wa MTU binafsi.

Hii mada kuna watu watachanganya kati ya Kufanikiwa au mafanikio Success na kuwa na maendeleo development.

Mimi ntatoa mtazamo kuhusu kufanikiwa na sio Maendeleo.

Kuhusu Mimi kufanikiwa , huwa naangalia pale unapofika hatua ya kuwaathiri watu kwa njia chanya.

Mfano Una pesa au una kipawa fulani jinsi watu wanavyokuwa benefited kupitia ulichonacho tayari umefanikiwa.

Mfano, Diamond tunaona ametoa Sana Ajira kwa watu na hao watu wanaishi vizuri hayo sasa ndo mafanikio.

Hivyo yawezakana Mimi napesa Sana naishi vizuri Ila watu wakaribu yangu wakiwa hawaishi vizuri maana yake sijafanikiwa.

Huo ndo mtazamo wangu kuhusu mafanikio.

NB: Kujenga ghorofa, kuoa, kuolewa, kununua gari kuhamia kwako hayo ni maendeleo - development

Ila kusaidia ndugu aliyekwama Ada, kumuwezesha MTU kibiashara, kuwasapoti wazazi ndugu marafiki n.k hayo huitwa mafanikio. Success.
Hapo kwenye maendeleo na mafanikio nimekuelewa.
 
hili swali litajibiwa Kutokana na mtazamo wa MTU binafsi.
Na mazingira husika ya eneo

Kwa mfano mtu anayesema amefanikiwa kijijini ni wa tofauti na mjini

Mtu anayesema amefanikiwa Marekani ni tofauti na mafanikio ya mtu wa Tanzania

Mtazamo wa mtu binafsi na eneo analoishi vinaamua ikiwa mtu atajiona amefanikiwa au la
 
Kwangu mimi mafanikio ni kuwa na uwezo wa kufanya chochote unachotaka, na kuenda mahali popote unapotaka muda wowote unaotaka, ilimradi haumdhuru mtu wala hauvunji sheria za nchi
Kwa mantiki hii, rais wa Tz unaweza kusema amefanikiwa?
 
Nakubali, utajiitaje umefanikiwa ila hauna financial freedom..

Huwezi kula unachokitaka

Huwezi kuhimili medical bills kwenye hospitali zinazoeleweka

Huwezi kusafiri kwa usafiri unaoupenda

Savings zinawekwa ili ziliwe next month

Haya sio mafanikio Ila ni kupiga hatua tu kwenye maisha

Lakini pia kufanikiwa yaweza kumaanisha fullfillment inayotokana na mtu kufikia malengo aliyoyatamani. Maana kuna wengine wanapenda umaarufu, kusaidia watu au kuweza kuishi kutokana na vipaji vyao etc

Kwa hiyo wewe unaweza kumuona hajafanikiwa Ila amepata fullfillment aliyoitaka. So, hata hayo ni mafanikio
Yeah nakubaliana na wewe mkuu, ila kama nilivyosema huo ni mtazamo wangu binafsi na si maana ya moja kwa moja ya neno mafanikio, hili neno sidhani kama lina maana ya jumla kila mtu hutoa maana kulingana na mtazamo wake hivyo kubaki kuwa moja ya masuala mtambuka
 
Maisha ni ubatili mtup
maisha ni ubatili mtupu- hii kauli huwa inaongelewa na WATU ambao hawajafika hatua inaitwa Self- actualization ambao hawajazigusa jamii zao kwa njia chanya


Ya duniani na mbinguni yote katoa Mungu hivyo every day is a gift from God. To say life is illusion inafikirisha.
Mkuu kusema maisha ni ubatili haimaanishi watu hawatakiwi kutafuta mafanikio na kuyafurahia maisha, wewe pambana na furahia maisha yako wazungu wanasema "enjoy it while it lasts" ila hiyo haibadili ukweli kuwa maisha ni ubatili, Mfalme Suleiman alipewa vitu vingi vizuri na alifanya mambo mengi mazuri ila mwisho wa siku alikiri kwamba yote ni ubatili na kujilisha upepo tu
 
Back
Top Bottom