Zipi ni alama za kuwa umefanikiwa kimaisha?

Zipi ni alama za kuwa umefanikiwa kimaisha?

"Mimi nimefanikiwa kung'oa pisi Moja matata hapa mtaani kwetu! Ilikuwa inanisumbua Kwa muda mrefu".

Tusipangiane maisha
 
"Mfalme Suleiman alipewa vitu vingi vizuri na alifanya mambo mengi mazuri ila mwisho wa siku alikiri kwamba yote ni ubatili na kujilisha upepo tu"
 
Mkuu kusema maisha ni ubatili haimaanishi watu hawatakiwi kutafuta mafanikio na kuyafurahia maisha, wewe pambana na furahia maisha yako wazungu wanasema "enjoy it while it lasts" ila hiyo haibadili ukweli kuwa maisha ni ubatili, Mfalme Suleiman alipewa vitu vingi vizuri na alifanya mambo mengi mazuri ila mwisho wa siku alikiri kwamba yote ni ubatili na kujilisha upepo tu

Philanthropist - ndo hatua nakuombea uifikie .

Ukiwa philanthropist utaweza kujiona vizuri
 
Mafanikio sio lazima pesa na mali.

Hata ukibadili mtazamo wako wa maisha tu nako ni kufanikiwa.
 
Kufanikiwa ni Kutimiza kusudi la Mungu aliloweka ndani Yangu, Na hatimaye baada ya kutimiza kusudi hilo niweze kufika kwake yeye aliyenileta.
 
Miaka miwili iliyopita huko Kigamboni,
Nilikuwa natoka kwangu na kwenda dukani kufuata mahitaji, wakati nipo njiani kuna vijana watano walikuwa kwenye mjadala juu ya kufanikiwa.

Ulikuwa mjadala wenye mabishano pia. Walitajwa watu maarufu wengi kama mfano wa watu wenye mafanikio.

Walitajwa : Diamond, Samatta, Dimpoz, Mwamposa, Kiba na wengineo wengi.

Nilisimama na kuwasikiliza ..
..nikachangia kwa kuuliza swali moja
"zipi ni alama kwamba mtu amefanikiwa kimaisha "

Nikawaambia mimi nitajiona nimefanikiwa kama :
  • Kipato changu kilichopo akiba kitaweza Kulisha familia yangu muda wa mwaka mzima bila kuterereka.
  • Nitakuwa na familia yenye amani na upendo.
Hata freemason na watoa kafara wenye vipato na matajiri wanalisha familia mwaka mzima bila kutetereka

Hata wanasiasa mafisadi na wezi wanafamilia zenye amani na upendo (kwa sababu ya pesa) mf. Nape
 
Mafanikio ni kua na Mara 3 au 4 zaidi ya kile ulichonacho hapa nazungumzia assets, mifano ni mingi let say unamiliki viwanda zaidi ya vitatu au vinne na kuendelea wewe tayari ni umeshafanikiwa

SIO eti unamiliki kigari kimoja na kijumba kimoja n still bank inakudai Pesa kibao za Mkopo wenye riba za kufa mtu na unakatwa kila mara eti unajiona umefanikiwa hell no ukiteteleka kidogo tu kigari chako na kijumba bank inapiga mnada hajafanikiwa bado
Watu wanamiliki viwanda vya kumwaga ila hawana uwezo wa kuzaa, wengine wana madonda yanayotoa funza, wengine wanafuga majoka n.k Nao wamefanikiwa kimaisha?
 
Watu wanamiliki viwanda vya kumwaga ila hawana uwezo wa kuzaa, wengine wana madonda yanayotoa funza, wengine wanafuga majoka n.k Nao wamefanikiwa kimaisha?
Wewe umesema nimesemaje ukiwa na Mara 3 au 4 ya kile ulichonacho km assets wewe tayari umefanikiwa mfano una mashamba Ekari 100 au Ekari 200 matatu au Manne na umepanda miti ya mbao ya kutosha wewe tayari umefanikiwa baada ya miaka Kumi unashika mabillion mkononi hapo tayari umeshafanikiwa
 
Kufanikiwa hakuna maana inayojulikana moja kwa moja, hili swali litajibiwa Kutokana na mtazamo wa MTU binafsi.

Hii mada kuna watu watachanganya kati ya Kufanikiwa au mafanikio Success na kuwa na maendeleo development.

Mimi ntatoa mtazamo kuhusu kufanikiwa na sio Maendeleo.

Kuhusu Mimi kufanikiwa , huwa naangalia pale unapofika hatua ya kuwaathiri watu kwa njia chanya.

Mfano Una pesa au una kipawa fulani jinsi watu wanavyokuwa benefited kupitia ulichonacho tayari umefanikiwa.

Mfano, Diamond tunaona ametoa Sana Ajira kwa watu na hao watu wanaishi vizuri hayo sasa ndo mafanikio.

Hivyo yawezakana Mimi napesa Sana naishi vizuri Ila watu wakaribu yangu wakiwa hawaishi vizuri maana yake sijafanikiwa.

Huo ndo mtazamo wangu kuhusu mafanikio.

NB: Kujenga ghorofa, kuoa, kuolewa, kununua gari kuhamia kwako hayo ni maendeleo - development

Ila kusaidia ndugu aliyekwama Ada, kumuwezesha MTU kibiashara, kuwasapoti wazazi ndugu marafiki n.k hayo huitwa mafanikio. Success.
Unaweza kufanya hayo yote lakini bado ukawa haujafanikiwa, Mfano Mobutu Seseseko Alikuwa na mali nyingi na alisaidia ndugu zake, Je na yeye alifanikiwa? Tujifunze kutambua mafanikio ya Kimwili, Nafsi na Roho.
 
Kwangu mimi mafanikio ni kuwa na uwezo wa kufanya chochote unachotaka, na kuenda mahali popote unapotaka muda wowote unaotaka, ilimradi haumdhuru mtu wala hauvunji sheria za nchi
Yote hayo yana maana gani kama hauna mguu mmoja, hauna uwezo wa kuzaa, una masharti ya kafara n.k? Ukipewa sharti la kuhasiwa haumdhuru mtu wala kuvunja sheria ila nafsi yako haijafanikiwa
 
Unaweza kufanya hayo yote lakini bado ukawa haujafanikiwa, Mfano Mobutu Seseseko Alikuwa na mali nyingi na alisaidia ndugu zake, Je na yeye alifanikiwa? Tujifunze kutambua mafanikio ya Kimwili, Nafsi na Roho.


Mafanikio hayana definition ndo maana hapa kila MTU anakuwa subjective anatoa mtazamo wake


Usi-question utaharibu mada.

Wenzako wamezungumzia kiuchumi wengine kijamii sasa umezungumzia kiroho

Na ukizungumzia kiroho unakuwa upo subjective
 
Mafanikio ni ile level ambayo mtu humtegemei mtu mwingine kwenye basic need za kibinadam hapo tyr ushafanikiwa mana unaweza lea familia bila shida ss kama hata kula yako tu tabu hata kama una amani na upendo hujafanikiwa bado
Kama simtegemei mtu ila namtegemea Jini nyoka a.k.a Ndumba kwa sharti la kidonda, hapo nimefanikiwa?
 
Back
Top Bottom