Tusubiri ubunge wa mahakama wa msaliti zzk kwa vyovyote cdm haiwezi kukubali utumwa wa mahakama na wakala ccm ambao masaa yote wanacheza na akili za wanachama wa cdm.tusubiri mwisho wa hili
 
Zitto mfamaji mwacheni atapetape maana hakuna jinsi lazima aje na mistari ya kutosha.Ahamie huko wanako msapport akajenge huko badala ya kuhangaika na kujichora,kiasi cha kupoteza ka umaarufu kadogo aliobakia nako.
 
 
cdm na ccm wot wezi tu,kz kuwafaidisha ndugu zenu na marafiki
 
Kweli Tindu Lissu ni kifaranga tu...haya mambo ya Mkono,Mbowe na Zitto wanayajua hawa watatu vizuri sana,kuyaingilia asiyoyajua ni kujidharirisha kama hivi....

Mkono anasema hajawahi kuwa na issue yoyote ya kuongea na Lissu zaidi ya mijadala ya kibunge sembuse hayo ya kumpa fedha Zitto aliyodai ameyapata kwa Mkono.Ndio tatizo la kifaranga kuingilia ugomvi wa mama yake.

http://mambomseto24.blogspot.com/2014/01/lissu-matatani-zitto-mkono-wampa.html
 
hakika mtu alie li engeneer hili sakata ni jasusi wa hatari....

WASIRA alisema mpaka 2015 na sasa hata muda huo haujafika_ni mpango wa M/mungu _wahun wa CDM (viongozi wazinifu) walitaka kutuaminisha wao ni wapigania Haki na tuwakabidhi nchi_nakwambia SLAA na MBOWE wana watoto wachanga wakat umri umekwenda_wangetuibia usiku na mchana kuwawekea akiba wachanga wao kudadadadedek
 
Wakati Mbowe anatolewa bungeni baada ya vurugu Huyu ZZK alikuwepo kweli bungeni?
unazani zitto ni zoba wakufanya ujinga wakati anafaham sheria na taratibu?
mazoba ndo walienda kumzingira zoba mwenzao
 
Mtumishi siasa waijua ha ha haa

Maalimu naona unafatilia hoja zangu kwa ukaribu sn!

Unajua umri nao ni dawa! Na ndio kuona mengi!

Haya mambo ni changamoto za kila siku! Kwahiyo ni rahisi kuyafahamu!

Kuna mada moja ulichungulia Mara moja ukaniambia nijipange then wew sikukuona tena!

Nafurahi sn kukutana na wewe!
 
Haha haha technically na yeye amechukua magari mawili haha big show ccm ni whatsup sana...huenda dogo naye kataka uenyekiti apige haha uzalendo ma s a bu ri yao!

Mungu wangu
Hata Mwenyekiti wetu Muheshimiwa Mbowe ni FISADI? Au anapokea Pesa za Mafisadi (Shetani wa Tanzania). Mimi sijui Watanzania sasa tukimbilie wapi?

Mimi ningeomba Mbowe Uwajibike kisiasa ili Usije kumpaka Rais wetu ajaye Dr. Slaa Matope ya ufisadi.

Dr. Slaa kaa mbali kabisa na Zito Kabwe na Mwenyekiti Mbowe kwani watakurushia Kinyesi cha Ufisadi.
 
Miaka mitatu iliyopita – Novemba 2009, gazeti la ----------- lilichapisha habari hii kwenye ukurasa wake wa kwanza kuhusu Zitto Kabwe.
Gazeti lilikuwa limefanya mahojiano na Mama Mzazi wa Zitto, Shida Salum. Katika mahojiano hayo, Mama Mzazi wa ZItto alikiri mwanawe kutumiwa na watu wasiokitakia mema chama.

Leo ni miaka mine tangu Mama Zitto kueleza hayo. Sasa wakati tukitafakari yanayompata Zitto ndani ya Chadema, tuyaangalia yale ambayo Mama Zitto alieleza wakati huo.



SHIDA Salum, mama mzazi wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema mwanaye anatumiwa kukivuruga chama chake.

Akizungumzia taarifa zinazoandikwa na baadhi ya magazeti kuhusu kinachoitwa mgogoro wa uongozi katika CHADEMA, kati ya Zitto na viongozi wenzake, Shida alisema, “hakuna mgogoro pale, kuna kikundi cha watu wanaotaka kumtumia mwanangu kufanikisha mambo yao.”

Akizungumza na gazeti hili juzi jijini Dar es Salaam, alidai kuna watu walio nje ya CHADEMA wanakula njama za kumgombanisha mwanawe na viongozi wenzake.

Alisisitiza, “kuna baadhi ya wanasiasa ndani ya CHADEMA wanaotumiwa na walio nje kugombanisha viongozi.”

Akaongeza, “Mambo ya uchaguzi yalikwisha kitambo na Zitto kwa moyo mmoja alikubali kumaliza tofauti zake na Mbowe (Freeman Mbowe) ndiyo maana akamuacha Mbowe kuwa mgombee pekee wa uenyekiti.”


Shida aliwatuhumu watu walio nje ya CHADEMA akisema ndio wanaopandikiza mbegu za chuki kwa lengo la kuwavuruga. Hata hivyo, hakuwataja.

Alisema kila mwenye akili timamu anajua kinachotafutwa, na nani mkweli na yupi anasingiziwa.

“Angalia wanaoandika haya. Kweli Zitto anaweza kutetewa na magazeti ya Habari Corporation yanayomilikiwa na Rostam Aziz halafu ukaamini kile kinachoandikwa?” alihoji.

Aliongeza, “Rostam yupi? Ni huyu tunayemjua au mwingine? Kwa wema upi alionao kwa chama chetu.”

Wiki iliyopita magazeti ya Rai na Mtanzania yalinukuu taarifa zikidai kuwa zimetolewa na Shida, kwamba anataka mwanawe aondoke kwenye chama hicho kwa kile ilichoeleza kuwa “kumwepuesha na yaliyomkuta Chacha Wangwe.”

Katika kujibu hilo, Shida anasema, “Mimi na Zitto tunajua katiba ya chama chetu. Tunafahamu taratibu za kuendesha chama. Yeye ni naibu katibu mkuu, mimi ni mjumbe wa Kamati Kuu. Tunajua nini maana ya uongozi, hivyo hatuwezi kukurupuka barabarani.

“Kwamba kama kuna malalamiko au tuhuma mathalani juu ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum, basi sote ni sehemu ya hicho kinacholalamikiwa. Kutokana na hali hiyo, hatuwezi kujifanya hatuhusiki na tukatuhumu kupitia vyombo vya habari, tena magazeti yanayomilikiwa na mwanachama wa CCM.”

Shida alisema anajua kwa mapana chanzo cha yote yanayoandikwa na jitihada za kutaka kumgombanisha Zitto na viongozi wenzake, hasa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe.

“Yote haya tunafahamu chazo chake. Si uchaguzi wa ndani ya chama. Uchaguzi ulishakwisha na Zitto kwa moyo mmoja alikubali kumuachia Mbowe uenyekiti ili kulinda maslahi ya chama,” alisema.

Alisema kuwa yeye kama mlezi, hawezi kuruhusu hali hiyo, hivyo atatumia nafasi yake ya mjumbe wa CC kuhakikisha kwamba tabia hiyo ya kugombanisha viongozi inakoma.

“Nikiwa mzazi, mlezi na mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA, siwezi kuruhusu Zitto kutumika kuingiza chama katika mgogoro. Nitasimama imara kuhakikisha kwamba CHADEMA inakuwa salama,” alisema.

Wiki iliyopita, Dk. Slaa aliwaondoa katika nafasi za utendaji David Kafulila aliyekuwa Afisa Habari na Danda Juju aliyekuwa Afisa anayeshughulika na Halmashauri na Bunge kwa kile kinachoelezwa kuwa utovu wa nidhamu kwa chama na viongozi wake.

Kafulila alinukuliwa na baadhi ya magazeti kuwa alibeza kikao cha viongozi wa juu wa chama hicho kilichofanyika Dodoma ambapo Mbowe na Dk. Slaa walikutana katika kikao cha kawaida na wabunge wa chama hicho na baadhi ya wakurugenzi.

Kafulila alisema mkutano huo wa viongozi haukuwa na maana; na alifika mbali zaidi kwa kuufananisha na vikao vya geto. Ni matamshi hayo na mengine yaliyomfanya Dk. Slaa kutumia mamlaka yake ya kikatiba kumuondoa Kafulila katika wadhifa huo.

Taarifa zinasema hoja ya kumuondoa Kafulila katika kikao ilitolewa na Msafiri Mtemelwa, mmoja wa viongozi wake na ambaye alikuwa meneja wa kampeni za Zitto wakati wa kuwania uenyekiti wa CHADEMA
 
Hata wenyewe chadema walikuwa wapi Sikh zote kuyasema hayo? Au kwasababu wamemuona anaweza kupata uongozi?
walikuwa wapi kuyasema yapi?kwani umesikia wapi cdm walipo kiri hizi allegations? these are mere allegations mpaka hapo,unless uniambie cdm wamekiri madai hayo its only then when your comment can be valid.
 
Zitto hajajibu mashtaka kwake kuhusu magari aliyopewa na Mkono. Two wrongs do not make a right.

Kabla ya ku deflect mashtaka kwa kuibua uozo wa mpinzani wako, jibu mashtaka kukuhusu wewe.
Ajibu wapi? Humu JF?
Zitto ana haki ya kujibu tuhuma kupitia njia zile zile maadui zake wanazotumia. Wanatumia JF, Facebook, na blogs mbalimbali bila ya kusubiri jibu rasmi kwenye kikao.
Wana behave kihuni na ana respond kihuni, binafsi sipendi aina hiyo ya malumbano maana yanakidhoofisha chama, lakini ni vigumu kunyamaza tu ukirushiwa kila aina ya matusi, kebehi, kejeli na uzushi!
Sasa ni wakati wa kuingia ndani, kuzungumza bila ya kumpa faida adui kwani maadui wa CHADEMA wanarukaruka kwa furaha kila wanapotuona tukivuana nguo hadharani!
Msimamo wangu mimi ni kwamba inawezekana ndugu hao walikosea, lakini chama kime over react katika suala hili ambalo lingeweza malizwa kistaarabu na bila ya kukijeruhi chama. Nauliza tena hivi ni nani huyu aliyeturoga hadi tunahangaikia issue ya watu watatu, wanne na kusahau mambo muhimu kabisa kwa nchi kama Katiba, madawa ya kulevya yaliyotamalaki na utoroshwaji wa kutisha wa nyara za taifa na manyang'au hawa CCM?
 

HIVI UNATAKA AKANUSHE NINI WAKATI AMEHOJIWA NA KUELEZA KUWA HAKUNA KOSA KUPOKEA HELA KWA MTU YEYOTE. Maana yake amekubali kuwa ni kweli alipokea na ni kweli alikidanganya chama kuwa anakikopesha wakati waliotoa walitoa kwa ajili ya chama na sa kwa ajili ya mbowe. CHADEMA NAWASHANGAA SANA WANAMWITAJE ZZK MSALITI WAKATI HATA WAO WENYEWE WAMEPEWA HELA NA MATAJIRI WA CCM? Kunya anye kuku, akinya bata kaharisha. Wangemtuhumu zzk kwa kuvunja katiba ningewaunga mkono 100% lakini kumuita msaliti kisa kapewa gari mbili hapo siwaungi mkono hata siku moja.
 
unazani zitto ni zoba wakufanya ujinga wakati anafaham sheria na taratibu?
mazoba ndo walienda kumzingira zoba mwenzao

Ulikua unajinasibu kua wewe ni mfuatiliaji Wa Siasa za Tz na kimataifa! Lkn kwa Jibu lako hili wewe ni mshabiki Wa mtu binafsi! Kwasababu wapinzani wote bungeni walitoka nje kupinga kuburuzwa ktk kujadili swala la katiba mpya kwa uchache wao kasoro Mh Mlema!

Sasa hapo ukimsifu Huyo ZZK wakati hajaonesha kupigania ata swala la katiba mpya sikuelewi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…