Zitto afungua kesi ya kikatiba kupinga uteuzi wa CAG mpya

Zitto afungua kesi ya kikatiba kupinga uteuzi wa CAG mpya

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kiongozi wa ACT Wazalendo.,Zitto Kabwe, amefungua kesi ya Kikatiba dhidi ya mosi; Sheria ya Ukaguzi namba 11 ya mwaka 2008 kukiuka Katiba na pili Uteuzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) uliofanywa na Rais Magufuli kuwa kinyume na masharti ya Katiba.
EPIFBLXWAAAxXjv.jpg


Kesi hiyo ya Kikatiba namba 1 ya mwaka 2020 ambayo Ndugu Zitto anawakilishwa na Wakili Nyaronyo Kicheere, imefunguliwa Masjala Kuu ya Dar Es Salaam na imepangiwa Majaji Mlacha, Masoud na Masabo.

Zitto anaiomba Mahakama kutamka kuwa kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Ukaguzi No.11/2008 inaenda kinyume na Katiba kwa kukiuka Ibara ya 144(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia kupingana na kifungu 62(a) cha Sheria ya Ukaguzi ambacho kinaendana na Katiba.

Aidha Zitto anaiomba Mahakama kutamka pia kuwa uamuzi wa Rais Magufuli wa kumwondoa Ofisini Prof. Assad ulikuwa kinyume na Katiba kwani Prof. Assad hakuwa ametimiza miaka 65 ya kisheria wala miaka 60 ya Kikatiba. Pia uteuzi wa Bwana Kicheere hukufuata Katiba ufutwe.

Zitto Kabwe anasema baada ya kutafakari kwa kina ameonelea kuwa uvunjifu wa Katiba uliofanywa na Rais Magufuli haupaswi kukaliwa kimya. Kama Mtanzania, kwa miaka 8 aliyehudumu ktk Kamati za Bunge za Uwajibikaji, itakuwa dhambi kutotaka tafsiri ya Mahakama kuhusu uteuzi wa CAG.

"Nalifanya hili kulinda ma CAG wajao kwani tukiacha Katiba ikichezewa Ofisi ya CAG inayopaswa kuwa Huru KIKATIBA itakuwa dhaifu mno na kuhatarisha usimamizi bora wa Fedha za Umma. Kwa maoni yangu CAG akishateuliwa haondokeki mpaka afikie umri wa kustaafu kisheria." Zitto Kabwe.

Shauri hili la Zitto Kabwe litaitwa kwa mara ya kwanza Januari 28, 2020 saa 3 Asubuhi, ambapo Wajibu shauri ni Rais Magufuli kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, CAG Mussa Assad na Bw. Charles Kicheere.

Imetolewa na;
Suphian Juma, Afisa Habari, ACT Wazalendo.
Jan 25, 2020.
 
Mwaka wa mavurugu umewadia kipindi hiki hata ukifichwa ndani ya chupa jitahidi kitokeze hata kidole tu watu wakuone kuwa upo vinginevyo bungeni hurudi.

Wazee wa hoja kimyaaaaaaa au nazo zinahitaji mikutano ya hadhara?

Wazee wa kuzungusha mikono haya mabadiliko vepeeee mmeyaelewa eeeeeh hahahaaaaà 😆 kikubwa ruzuku inaflow na inaliwa.
 
Mwaka wa mavurugu umewadia kipindi hiki hata ukifichwa ndani ya chupa jitahidi kitokeze hata kidole tu watu wakuone kuwa upo vinginevyo bungeni hurudi.

Wazee wa hoja kimyaaaaaaa au nazo zinahitaji mikutano ya hadhara?

Wazee wa kuzungusha mikono haya mabadiliko vepeeee mmeyaelewa eeeeeh hahahaaaaà 😆 kikubwa ruzuku inaflow na inaliwa.


Hilo jina nakuambia mara kibao halikufai
 
Ungeaza kujiuliza wewe ulichoandika kwenye post yako hadi kikafutwa... Wewe kama umeandika vizuri kwa nini imefutwa... Acha kutafuta chokochoko na watu wasiokudis....itakusaidia nn


Mie sijaandika kibaya na hakijafitwa...nimeandika ndevu zimempendeza kila la heri zito..! Acha kuwa teja wa ccm ww !
 
Anamtishia nyau CAG mpya asifanye special audit ya matumizi ya pesa za ACT wazalendo

CAG mpya nenda kagua miaka ya nyuma upya ikiwezekana Rudi hata Saba nyuma .Tuma kikosi kazi.Hilo.ni tishio la kutaka umuogope ukae mbali na ulaji ruzuku wake
 
Mie sijaandika kibaya na hakijafitwa...nimeandika ndevu zimempendeza kila la heri zito..! Acha kuwa teja wa ccm ww !
Na umefutiwa zaidi ya moja... Kuna nyingine umeniqoute kabla sijajibu ikafutwa... Hii inaonyesha hujatulia hata... Kiufupi una mihemko ya kisiasa... Sijaona hoja uliyojenga hata moja... Yaani unafanya kama ninyi mnavyosutana... Achana na siasa,you are an adult but it seems you're still a kid in politics.
 
Asad kastaafu juzi tuu njaa imeanza kuuma na anatuma vijana wake ili wafanye jitihada wamrudishe kazini? umri!!! baba umri !!!baba

ALIIMBA MR.EBO
Njaa inauma...... chunga usichinje njau...........njaa inauma.........
 
Back
Top Bottom