Zitto afungua kesi ya kikatiba kupinga uteuzi wa CAG mpya

Zitto afungua kesi ya kikatiba kupinga uteuzi wa CAG mpya

Mimi ningefurahi sna ningeona amefungua kesi ya kudai tume huru ya uchaguzi ili CCM isitawale milele.
 
Mleta mada kajichanganya muda mrefu alikuwa hayuko mtandaoni baada ya chadema kumpiga chini kwenye chaguzi zao za ndani naona kapost mbio.mbio.akiwa na hang over ya frustration kichwani za kupigwa chini na chadema chaguzi zao za ndani

Hizi post anaonyesha wazi kahamia ACT wazalendo hayuko Tena chadema.Kaandika Akiwa na misongo ya mawazo msamehe bure

Kwani ana ulazima wa kuwa mwanachama wa cdm? Ana haki ya kuhamia chama chochote akitakacho na hajavunja sheria yoyote ya nchi.
 
Tujiandae kwa maajabu mengine ya vyombo vyetu vya kutoa haki na kutafsiri sheria.
Zitto aachane na hilo linaloweza kupoteza muda muhimu tulip nao. Akili yote iwe kuibana serikali kupeleka muswada wa dharula kuhusu tume huru ya uchaguzi huku akishirikiana na wenzake katika mpambano huo na kuachana na personal kiki.
Ni bora hata uchaguzi uahirishwe hadi mwakani mpaka tume iundwe kuliko kufurahia kufanyika hivyohivyo na litume lililopo.
Kukubali kuwahisha ndio mwisho wa vyama vingine vyote ukiacha ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zito ili kulinda heshima yako inabidi ujifunze kuwa sniper na sio machine Gunner wa matukio the more unashambulia aimlessly serikali hii inakushushia credibility yako kwenye siasa.

Zitto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa zina ujinga mwingi sana, basi tu kwa vile imebidi siasa zitulishe na kutuongoza.
 
He is fighting a losing battle. Wastage of time and resources.
You are most definetly layman in constitutional law, let me give you enlightment before you futher go astray.

Zitto Kabwe is not litigating for himself or in his personal capacity rather the case has the status of 'public interest litigation' he is literally, suing for public good and judgement entered will be 'judgement in rem' binding to all us in our jurisdiction as opposed to 'judgement in persona' If he would have sued for himself.

We all have stake in Zitto's case, either loosing or winning.
 
Anachokifanya Zito ni sahihi sana. Hata kama hukumu wengi wanaona inajulikana lakini ni vema mashauri kama haya yakiwepo maana yanatunza kumbukumbu sahihi za historia ya Taifa letu.

Matukio haya yataeleza jinsi uvunjifu wa katiba ulovyoweza kufanyika wakati fulabu, jinsi watu walivyopinga kwa njia mbalimbali, na jinsi mfumo wa mahakama ulivyoshindwa kutimiza wajibu wake.

Hongera sana Zito. Kesi za namna hii zilistahili kuwa nyingi. Kila tukio ambalo watu wanasema katiba ilivunjwa, na hasa na viongozi, ni vema kufungua kesi, hata kama mahakama isiposimamia ukweli, kumbukumbu itakuwa imewekwa.
 
He is fighting a losing battle. Wastage of time and resources.

Angesema tu bila ya kuchukua hatua kama hii bado unge mlaumu na kumkosoa ktk ayakayo yasema ,hapa kachukua hatua bado unabeza.Tatizo lako hapo ni nini !?
 
Mkuu nadhani kweli Zitto asikatishwe tamaa Bali ashauriwe asishike mengi kwa wakati mmoja, apeleke nguvu zote kwenye kutaka Tume huru ya uchaguzi.
Kwanza bila tume huru hata akishinda uchaguzi wowote hawezi kutangazwa, sasa wa nini huo uchaguzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa nini yeye ndiye afanye kila jambo?
Viongozi wengine kwako wapi na wanafanya nini kuhakikisha kuwa inakuwepo tume huru ya uchaguzi?
Viongozi wote Wa upinzani wameshindwa kupeleka hili jambo mahakamani kazi ni kusema tuu kwenye vyombo vya habari... eti tunataka tume huru!! Kweli!! Kirahisi namna hiyo??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom