Zitto akiwa mwenyekiti; naahidi kuipa CHADEMA kura zangu zote!

Zitto akiwa mwenyekiti; naahidi kuipa CHADEMA kura zangu zote!

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,149
Reaction score
3,825
WanaJF!

Binafsi nina amini katika 'uongozi' na sio hali ya taasisi, hii ni kwa kumaanisha kuwa endapo akipatikana kiongozi bora, basi hata taasisi iwe hoi namna gani itanyooka tu na kuwa yenye tija na yenye manufaa makubwa kwa umma.

Nina yasema haya kwa kutambua kuwa hivi karibuni una tarajiwa kufanyika uchaguzi wa ndani ya CHADEMA ambao umekuwa ukifanyika kwa kila baada ya miaka mitano, hivyo mimi kama mwananchi mpenda amani, haki na usawa, nimeona nitoe yaliyo moyoni kuhusu uchaguzi huo.

Zitto ni kijana ambae amehusika kwa kiasi kikubwa katika haya mabadiliko tunayo yaona hivi sasa kwa CHADEMA na taifa kwa ujumla wake, ni kijana ambae amejitoa kuhakikisha haki ina tolewa, usawa una kuwepo na sheria zinafuatwa, na hayo amekuwa akihakikisha yanafanywa na kuonekana kufanyika.

Zitto ndiye amekuwa tanuru la vuguvugu lenye kutoa hamasa na ujasili kwa vijana kuamka na kuhoji juu ya mambo mbalimbali yanayogusa mstakabali wa taifa letu, kwani itakumbukwa vijana wengi walijiunga na CHADEMA kwa kuvutiwa na ushawishi wa Zitto, uwezo wa kujenga hoja na uzalendo wake.

Aidha, itakumbukwa kuwa Zitto ndiye aliye ifyeka njia na kuwaandalia mazingira ya kuaminiwa na wananchi hawa wabunge wapya wa CHADEMA, kwani ni Zitto ndiye aliyekuwa akiibua mambo mbalimbali ya kifisadi serikalini, hii ilijenga imani kuwa ya wananchi kwa kijana huyu na kupelekea CHADEMA kujulikana nchini.

CHADEMA (nikiwa na maana ya wanachama) kama itajivika ujasiri na kukataa hali ya kuendeshwa na kikundi cha watu wachache na ikathubutu kumpa ridhaa ndugu Zitto nafasi ya uenyekiti wa chama hicho, binafsi nitatoa kura zangu kuanzia ya urais, ubunge mpaka udiwani kwa CHADEMA bila kujali ni nani aliye simamishwa kugombea nafasi hizo (soma aya ya kwanza).

ANGALIZO: USHABIKI WA ITIKADI ZA KISIASA NI KIKWAZO KWA MAENDELEO YA NCHI.
 
Last edited by a moderator:
Utakuwa umetumwa asubuhi hii? kumekucha wewe ndo unaota!! Huyo siku hizi ni Afisa habari wa wanamziki sio tena mwanasiasa ndg yangu HAMY-D,
 
WanaJF!

Binafsi nina amini katika 'uongozi' na sio hali ya taasisi, hii ni kwa kumaanisha kuwa endapo akipatikana kiongozi bora, basi hata taasisi iwe hoi namna gani itanyooka tu na kuwa yenye tija na yenye manufaa makubwa kwa umma.

Nina yasema haya kwa kutambua kuwa hivi karibuni ina tarajiwa kuwa na uchaguzi wa ndani ya CHADEMA ambao umekuwa ukifanyika kwa kila baada ya miaka mitano, hivyo mimi kama mwananchi mpenda amani, haki na usawa, nimeona nitoe yaliyo moyoni kuhusu uchaguzi huo.

Zitto ni kijana ambae amehusika kwa kiasi kikubwa katika haya mabadiliko tunayo yaona hivi sasa kwa CHADEMA na taifa kwa ujumla wake, ni kijana ambae amejitoa kuhakikisha haki ina tolewa, usawa una kuwepo na sheria zinafuatwa, na hayo amekuwa akihakikisha yanafanywa na kuonekana kufanyika.

Zitto ndiye amekuwa tanuru la vuguvugu lenye kutoa hamasa na ujasili kwa vijana kuamka na kuhoji juu ya mambo mbalimbali yanayogusa mstakabali wa taifa letu, kwani itakumbukwa vijana wengi walijiunga na CHADEMA kwa kuvutiwa na ushawishi wa Zitto, uwezo wa kujenga hoja na uzalendo wake.

Aidha, itakumbukwa kuwa Zitto ndiye aliye ifyeka njia na kuwaandalia mazingira ya kuaminiwa na wananchi hawa wabunge wapya wa CHADEMA, kwani ni Zitto ndiye aliyekuwa akiibua mambo mbalimbali ya kifisadi serikalini, hii ilijenga imani kuwa ya wananchi kwa kijana huyu na kupelekea CHADEMA kujulikana nchini.

CHADEMA (nikiwa na maana ya wanachama) kama itajivika ujasiri na kukataa hali ya kuendeshwa na kikundi cha watu wachache na ikathubutu kumpa ridhaa ndugu Zitto nafasi ya uenyekiti wa chama hicho, binafsi nitatoa kura zangu kuanzia ya urais, ubunge mpaka udiwani kwa CHADEMA bila kujali ni nani aliye simamishwa kugombea nafasi hizo (soma aya ya kwanza).

ANGALIZO: USHABIKI WA ITIKADI ZA KISIASA NI KIKWAZO KWA MAENDELEO YA NCHI.

Kwani una kura ngapi unavyosema zote, si ajabu hata haujajiandikisha
 
Kwani una kura ngapi unavyosema zote, si ajabu hata haujajiandikisha

Mkuu, nina ushawishi kwenye jamii, hivyo sio tu mimi ambae nitapigania CHADEMA ishinde (endapo Zitto akiwa mwenyekiti), bali hata vijana na wazee watajumuika na mimi kuhakikisha hilo linafanikiwa.
 
Wee msemaji wa Zito au wa Chadema??????
Ya ngoswe mwachie Ngoswe, au ndio adui mwombee njaa?
 
CDM inafanya maamuzi chini ya vikao halali vya chama. Hatuongozwi kwa hisia ( kama wale wa pigeni tuu tena nasema muwapige).

CDM kama taasisi inasheria na taratibu. Wanachama wa CDM wataamua nani anafaa kuwa mwenyekiti. By the way, tupo na ishu ya Ponda kwa sasa ndio habari ya mjini.
 
CDM inafanya maamuzi chini ya vikao halali vya chama. Hatuongozwi kwa hisia ( kama wale wa pigeni tuu tena nasema muwapige).

CDM kama taasisi inasheria na taratibu. Wanachama wa CDM wataamua nani anafaa kuwa mwenyekiti. By the way, tupo na ishu ya Ponda kwa sasa ndio habari ya mjini.

Hiki kichekesho kweli na udikteta wote wa CHADEMA unapata wapi ujasiri wa kuyasema haya.
 
CDM inafanya maamuzi chini ya vikao halali vya chama. Hatuongozwi kwa hisia ( kama wale wa pigeni tuu tena nasema muwapige).

CDM kama taasisi inasheria na taratibu. Wanachama wa CDM wataamua nani anafaa kuwa mwenyekiti. By the way, tupo na ishu ya Ponda kwa sasa ndio habari ya mjini.

Hivi ilikuwaje mpaka Zitto akawekewa kizuizi ili asigombee uenyekiti, nikumbushe ni kikao gani kilifanyika kumkataa Zitto asiwe mwenyekiti wa CHADEMA!
 
Wee msemaji wa Zito au wa Chadema??????
Ya ngoswe mwachie Ngoswe, au ndio adui mwombee njaa?

HAMY-D anachokoza tu anajua kitu kama hicho hakiwezekani ndani ya chama cha wana wa Kaskazini. Ni heri NASSARY akapata hiki cheo kuliko huyu kijana mwenye uwezomkubwa wa kukwepa kuwekewa sumu. Wakimshindwa watamuondoaje?
 
Hivi ilikuwaje mpaka Zitto akawekewa kizuizi ili asigombee uenyekiti, nikumbushe ni kikao gani kilifanyika kumkataa Zitto asiwe mwenyekiti wa CHADEMA!

HAMY-D ndugu yangu unajisumbua bure, hapa leo umeamua kufanya siku nzima gumzo liwe kwa mada yako japo umesema ukweli mtupu. Kati ya watu wanaowanyima usingizi hawa CHADEMA mmojawapo ni ZITTO.
 
Back
Top Bottom