Zitto hana chama, chama ni cha Wapemba na wafuasi wa Maalimu Seif

Zitto hana chama, chama ni cha Wapemba na wafuasi wa Maalimu Seif

Chama cha ACT kimeanzishwa na kina JK, Membe, Januari, Mwigulu nk kama Backup ya CCM baada ya kuzidiwa na CDM. Zito ndio alipewa jukumu hilo. Hao kina Limbu walitangulizwa tu baadae akataka kulazimisha kuwa kiongozi. Lakini wenye chama wakafanya yao na Zito akapewa nafasi yake. Rejea uchaguzi wa 2015 ACT ikiwa changa kabisa, ilisimamisha wagombea wa nafasi zote kuanzia urais, ubunge na udiwani nchi nzima, huku haifahamiki hela zao zilitoka wapi.

Magufuli 2015 ndio aliharibu mpango wa ACT kuwa chama kikuu cha upinzani, kwani alikuwa hampendi Zito, na pia hakuwa analipenda kundi la JK ambao ndio wafadhili wa ACT. Ni bahati mbaya wakati Maalim Seif anaporwa chama na Magufuli kwa kumtumia Lipumba, Maalim Seif akatafuta chama akaona ACT ndio hakina kiongozi wa muda mrefu na sio cha muda mrefu kama ilivyo CDM, NCCR, TLP nk. Alijua fika akiwa ACT atakuwa na maamuzi yote kama alivyokuwa CUF, na kweli ndio ilivyokuwa, ndio maana alishikilia kumuunga mkono Lisu kwenye urais, na sio Membe kama ambavyo Zito alitaka kwani Membe ndio wenye chama.

Zito ataendelea kuwa kiongozi wa chama cha ACT, kama ataendelea kuwafanya hao Wapemba wafanye Siasa zinazotakiwa na CCM. Hao Wapemba watavurugana na zito siasa za kweli za ushindani zitakapoanza na CDM kushika nafasi yake kama inavyotegemewa. Na zito anajakikisha anafanya siasa zinazotakiwa na CCM, kwa kuwahadaa ACT Wapemba kuwa hizo ni siasa za kistaarabu. Hili jengo la ACT lina fedha ya ufadhilii wa CCM, ndio maana huoni wakitaja thamani ya jengo, wala chanzo cha fedha hizo.
Zito ni pandakizi tangu akiwa CHADEMA.. na aliandaliwa na CCM ili aje kuidhoofisha kabisa kama ule mpando wa kuwa mwenyekiti ungefaulu
Hilo liliposhindikana ndio ukaundwa mpango wa usaliti chini ya viongozi watatu M1,M2 na M3.. M1 ilikuja kujulikana kwa wote ni Zito
Baada ya mtikisiko mdogo wa usaliti uliolenga kukigawa CHADEMA kuwa mapande mawili, kina Zito na kundi lake walipoteana na kusalitiana upya wenyewe kwa wenyewe

Wengine wakabaki na Zito ACT na wengine wakatimkia CCM kuunga juhudi na kupewa zawadi ya vyeo kina Shonza n the like.. Lakini picha halikuishia hapo.. Zito ndani ya ACT akapewa kazi ya kuhujumu kwa mlango wa nyuma juhudi na harakati zozote za upinzani (CHADEMA) kwa namna yoyote ile inayowezekana kufanya hivyo.. Na ndio anachokifanya mpaka wa leo

Zito hana mpango wowote wa kukipeleka ACT ikulu, hana mpango wowote wa kupigania mageuzi ya kweli, hana mpango wowote wa kuwakomboa watanzania kwenye shida yoyote... Yupo kwa ajili ya kutumika na kutumikia malipo ya ahadi
 
Hili andiko liko vizuri , na niliewa Sana, hakuna ACT bila CUF, ipo siku mbao zitagawanywa, mbao WAzanzibar sio wajinga , mfano tu ilo jengo halikutakiwa iwe agenda, ilitakiwa wakisha amia ndo wanaanza kutoa clip ndogo ndogo ,Sasa shida ya chama kile penda sifa
ACT - Wazalendo haina wanachama wala jengo la ofisi inalomiliki Bara. ACT inategemea nguvu ya wanachama kutoka Zanzibar wengi wakiwa ni wale waliokuwa wafuasi wa CUF- Maalimu Seif.

ACT -Wazalendo haina Jengo la Chama kwa maana ya umiliki, jengo walilopewa na Maalimu Seif Foundation ni lile walilokuwa wanatumia waliokuwa Wabunge watiifu wa Maalimu Seif, linamilikiwa na familia ya Seif.

ACT Wazalendo haina mtandao Bara mtandao wake uko Zanzibar. Kwa mtu makini ataelewa hapa mwenye nguvu ya chama ni nani kati ya Zitto, Wazanzibari na familia ya Seif.

Siku wenye chama chao wakiamua kuondoka na jengo lao chama kitakufa Zitto atabaki na makaratasi ya Msajili wa vyama vya siasa tu. Jifunze kutoka kwa Lipumba na CUF yake.

Najua wafuasi wa Zitto hawapendi kusikia haya lkn, Ukweli ndio huo.

Zitto and others, Keep this short Thread you will thank me later.
 
Chama cha ACT kimeanzishwa na kina JK, Membe, Januari, Mwigulu nk kama Backup ya CCM baada ya kuzidiwa na CDM. Zito ndio alipewa jukumu hilo. Hao kina Limbu walitangulizwa tu baadae akataka kulazimisha kuwa kiongozi. Lakini wenye chama wakafanya yao na Zito akapewa nafasi yake. Rejea uchaguzi wa 2015 ACT ikiwa changa kabisa, ilisimamisha wagombea wa nafasi zote kuanzia urais, ubunge na udiwani nchi nzima, huku haifahamiki hela zao zilitoka wapi.

Magufuli 2015 ndio aliharibu mpango wa ACT kuwa chama kikuu cha upinzani, kwani alikuwa hampendi Zito, na pia hakuwa analipenda kundi la JK ambao ndio wafadhili wa ACT. Ni bahati mbaya wakati Maalim Seif anaporwa chama na Magufuli kwa kumtumia Lipumba, Maalim Seif akatafuta chama akaona ACT ndio hakina kiongozi wa muda mrefu na sio cha muda mrefu kama ilivyo CDM, NCCR, TLP nk. Alijua fika akiwa ACT atakuwa na maamuzi yote kama alivyokuwa CUF, na kweli ndio ilivyokuwa, ndio maana alishikilia kumuunga mkono Lisu kwenye urais, na sio Membe kama ambavyo Zito alitaka kwani Membe ndio wenye chama.

Zito ataendelea kuwa kiongozi wa chama cha ACT, kama ataendelea kuwafanya hao Wapemba wafanye Siasa zinazotakiwa na CCM. Hao Wapemba watavurugana na zito siasa za kweli za ushindani zitakapoanza na CDM kushika nafasi yake kama inavyotegemewa. Na zito anajakikisha anafanya siasa zinazotakiwa na CCM, kwa kuwahadaa ACT Wapemba kuwa hizo ni siasa za kistaarabu. Hili jengo la ACT lina fedha ya ufadhilii wa CCM, ndio maana huoni wakitaja thamani ya jengo, wala chanzo cha fedha hizo.
Tusubilie ripoti ya CAG
 
Hili andiko liko vizuri , na niliewa Sana, hakuna ACT bila CUF, ipo siku mbao zitagawanywa, mbao WAzanzibar sio wajinga , mfano tu ilo jengo halikutakiwa iwe agenda, ilitakiwa wakisha amia ndo wanaanza kutoa clip ndogo ndogo ,Sasa shida ya chama kile penda sifa
Hakunaga Chama cha Siasa kisichopenda sifa
 
Zito hana mpango wowote wa kukipeleka ACT ikulu, hana mpango wowote wa kupigania mageuzi ya kweli, hana mpango wowote wa kuwakomboa watanzania kwenye shida yoyote... Yupo kwa ajili ya kutumika na kutumikia malipo ya ahadi
Siku Wapemba watakapogundua hilo Zitto ataliona jengo la Maalimu Seif alilozindua jana kituo cha polisi.
 
Hili andiko liko vizuri , na niliewa Sana, hakuna ACT bila CUF, ipo siku mbao zitagawanywa, mbao WAzanzibar sio wajinga , mfano tu ilo jengo halikutakiwa iwe agenda, ilitakiwa wakisha amia ndo wanaanza kutoa clip ndogo ndogo ,Sasa shida ya chama kile penda sifa
Uko sahihi, kulikuwa hakuna haja ya kutangaza uongo kuwa wamejenga na kuusambaza kwa vyombo vya habari, hawajui uongo kidogo tu unaweza kuondoa trust ya wanachama kwa chama.
 
ACT - Wazalendo haina wanachama wala jengo la ofisi inalomiliki Bara. ACT inategemea nguvu ya wanachama kutoka Zanzibar wengi wakiwa ni wale waliokuwa wafuasi wa CUF- Maalimu Seif.

ACT -Wazalendo haina Jengo la Chama kwa maana ya umiliki, jengo walilopewa na Maalimu Seif Foundation ni lile walilokuwa wanatumia waliokuwa Wabunge watiifu wa Maalimu Seif, linamilikiwa na familia ya Seif.

ACT Wazalendo haina mtandao Bara mtandao wake uko Zanzibar. Kwa mtu makini ataelewa hapa mwenye nguvu ya chama ni nani kati ya Zitto, Wazanzibari na familia ya Seif.

Siku wenye chama chao wakiamua kuondoka na jengo lao chama kitakufa Zitto atabaki na makaratasi ya Msajili wa vyama vya siasa tu. Jifunze kutoka kwa Lipumba na CUF yake.

Najua wafuasi wa Zitto hawapendi kusikia haya lkn, Ukweli ndio huo.

Zitto and others, Keep this short Thread you will thank me later.
Mag3 Retired Nguruvi3 Kalamu mnakubaliana na hili...?

Ila Zitto na wanachama wa Act bara wana nguvu na sauti kweli humo chamani ?
JokaKuu
 
Huwa ana bifu na Zitto mara nyingi nimeona nyuzi zake za kumsiginia kunguni Mwami.
Kwanza naona mleta mada na Baadhi ya wachangiaji kama wameanzisha huu uzi kutoa stress zao.

Ukiacha lugha za chuki kwa Zitto. Kilicho muhimu ni kujua namna ya kwenda na wazanzibari.

Hakuna chama chochote Tanzania hii ambacho hakitamani kupendwa na Wazanzibari. Si chama tawala wala Upinzani.

Mara ngapi CCM kinajaribu kutumia ushawishi wake ili kipendwe hiki ni chama Tawala.
Sikwambii Chadema na vyengine. Kule kuna malengo ya kisiasa na kuna ajenda za kudumu za kufanya siasa kuwa hai.

Nampongeza Zitto na Wenzake kwa kuona fursa cha msingi ni kujua namna za kuitumia ili kujenga mtandao wa chama mkubwa bara na visiwani. Unapozungumzia Wazanzibari (mnawaita wapemba) wameenea kote nchini na ni wafuasi wazuri wa kile wanachokiamini hawa ukiwachanganya na wanachama wengine wa huko Bara unapata ulezi na msingi mzuri wa mashina na ngome za chama. Hii ilikuwa siri ya CUF ambayo imekosa hio imani kwa sasa.

Kuna mtaji mwengine wa Elite walioko nje na wafanyabiasdhara . Wazanzibari wameeneo kila kona ya Dunia kutokana na historia yao ya visiwa.

Ushauri kwa akina Mh Zitto na wengine.

Tulizeni akili mjue vya kwenda na Wazanzibari ili mfikie malengo yenu. Kuna watu wanaitaka bahati hio hawajaipata kabisa. Zanzibar ndicho kitovu cha hamasa cha siasa za Tanzania na Mabadiliko kutokana na ajenda za kudumu za kimuungano na usawa, Uzalendo wa kiinchi na kujitawala, fursa za kiuchumi na ndoto za maendeleo ya ulimwengu ulivyo. Kule kuna kinyanganyiro (scramble) cha kuvutia mabwana wakubwa wa dunia kutokana na nafasi ya kijiografia ya Zanzibar. Zanzibar nafasi yake ipo kimkakati mno na ndio maana bila kuidhibiti Zanzibar unakosa utulivu wa kila kitu ki nchi. Sehemu kama hio ukawa na majority supporters inakuwa umeula kisiasa licha ya udogo wake na idadi ndogo ya watu.

Niishie hapo tu lakini Mh Zitto na wenzako jitahidinbi msikosee kama Lipumba. Kule wakishakosa imani nawe hutoboi. iulizeni CCM.


Nawasilisha
 
Back
Top Bottom