Zitto Kabwe: Anayefikiri Tanzania itapata Katiba Mpya bila kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi hana ubongo

Zitto Kabwe: Anayefikiri Tanzania itapata Katiba Mpya bila kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi hana ubongo

Hivi hii mashine ya kukagua kama mtu ana ubongo au hana, iligunduliwa wapi kweli?
 
Katiba mpya ni blaaa blaaa za Wapinzani kutaka uchochoro wa kupata madaraka kwa njia ya Mkato

Huku Mtaani kwa wapigakura ushaskia kuna hizo mambo?
Kwamba Katiba Mpya hata wewe huoni UMUHIMU wake..??

Watu wako jela kwa Makosa ya Uongo , Mahakama haziko huru.. wanateswa ndani ya Taifa lao.

Watu wanauliwa na Hawa Polisi wetu na kunyang'anywa Mali zao.. hawana pakwenda kupata Haki.

NCHI hii kwa Karne hii BADO tunatumia Katiba ya Zamani 1977 ya kikoloni.. Wewe unaenjoy wenzio kuumizwa, kuuawa, ??

Ebu kua akili ... Unasema wanasiasa ndio wanaitaka (what)[emoji3][emoji3] Maoni ya Rasimu ya Jaji Warioba yalitolewa na Watanzania.. wewe haukuwepo??

Kwamba Rais sio Mwanasiasa [emoji3][emoji3]??
Nchi ina Mhimili mmoja tu .. wewe unafurahi tu.

Kila uchaguzi watu wanapigwa na kuuliwa hovyo wewe kwako sawa.. kuleta matozo ya Kijinga kwako sawa.. n. K

Kuwa Akili acha kutumika simamia Maoni Ya Rasimu ya Jaji Warioba.

Hii ni Nchi sio Kijiwe
 
Sasa ulikuwa unazunguka zunguka nini kujifanya wapinzani ndio wanakwamisha upatikanaji wa hiyo Katiba Mpya wewe Kalumekenge?
Si ungesema tu hutaki Katiba Mpya.
Jamaa hamna kitu kichwani huyoo
 
Inawezekana ni yeye ndiye asiye na Ubongo halafu anafikiri ni wenzake hawana ubongo.

Tatizo la Zitto, anafikiri kuwa tume huru itawawezesha kupata Wabunge wengi na hao wabunge ndiyo watakaosukuma kuleta Katiba mpya. That's wrong. Katiba ni ya wananchi. Kitendo cha CCM kukubali Tume huru bila katiba mpya wanajua ni wapi walipo na upper hand .... sasa Kijana anajichomeka tu ilimradi arudi mjengoni .... !!

Zanzibar waliunda Tume huru ..... na alichokifanya Jecha wote tunakijua. Labda Zitto ana Ubongo wa kuku amesahau .... maana kuku ukimfukuza hapa anarudi baada ya dakika. Kuku anafanya mambo kwa mazoea!!
Zitto na ubongo wa kuku kashasahau mambo ya Jecha ya tume huru Zanzibar.
Zitto hana habari kabisa na kila chaguzi watu wanaumizwa na wanakufa. Mjaalaa huyu. Anawaza kuwa kiongozi wa kambi Rasmi ya upinzani bungeni.
Wanachi tuwaonyeshe wanasiasa wasiojali uhai wa watu kwa vitendo.
Hizo chaguzi anazotaka zimrudishe Zitto bungeni ,?tusipige kura , wateuane tu.

Hakuna uchaguzi bila katiba mpya.
 
Kwamba Katiba Mpya hata wewe huoni UMUHIMU wake..??

Watu wako jela kwa Makosa ya Uongo , Mahakama haziko huru.. wanateswa ndani ya Taifa lao.

Watu wanauliwa na Hawa Polisi wetu na kunyang'anywa Mali zao.. hawana pakwenda kupata Haki.

NCHI hii kwa Karne hii BADO tunatumia Katiba ya Zamani 1977 ya kikoloni.. Wewe unaenjoy wenzio kuumizwa, kuuawa, ??

Ebu kua akili ... Unasema wanasiasa ndio wanaitaka (what)[emoji3][emoji3] Maoni ya Rasimu ya Jaji Warioba yalitolewa na Watanzania.. wewe haukuwepo??

Kwamba Rais sio Mwanasiasa [emoji3][emoji3]??
Nchi ina Mhimili mmoja tu .. wewe unafurahi tu.

Kila uchaguzi watu wanapigwa na kuuliwa hovyo wewe kwako sawa.. kuleta matozo ya Kijinga kwako sawa.. n. K

Kuwa Akili acha kutumika simamia Maoni Ya Rasimu ya Jaji Warioba.

Hii ni Nchi sio Kijiwe
Asipokuelewa atakuwa na matatizo......
 
Katiba ndio inatoa muongozo wa tume ya Uchaguzi, Huwezi kupata tume ya Uchaguzi bila kuwapo kwanza katiba hata ya mpito.Zitto kajipange.
 
Kuna anayeweza eleza kwa mifano tume inawezaje kuwa huru kwa mazingira ya katiba hii ya sasa?
 
Inawezekana ni yeye ndiye asiye na Ubongo halafu anafikiri ni wenzake hawana ubongo.

Tatizo la Zitto, anafikiri kuwa tume huru itawawezesha kupata Wabunge wengi na hao wabunge ndiyo watakaosukuma kuleta Katiba mpya. That's wrong. Katiba ni ya wananchi. Kitendo cha CCM kukubali Tume huru bila katiba mpya wanajua ni wapi walipo na upper hand .... sasa Kijana anajichomeka tu ilimradi arudi mjengoni .... !!

Zanzibar waliunda Tume huru ..... na alichokifanya Jecha wote tunakijua. Labda Zitto ana Ubongo wa kuku amesahau .... maana kuku ukimfukuza hapa anarudi baada ya dakika. Kuku anafanya mambo kwa mazoea!!
Tume huru ya zito ni lazima mwenyekiti wake atateuliwa na Rais wakati mwenyekiti wa katiba mpya atadhibitishwa na Rais baada ya kuchaguliwa na vyombo vingine.Kwa hiyo atakuwa huru kweli kweli kuliko huyo wa zito
 
Tukiacha siasa za vyama point ya zito ni nzuri, tunaweza enda na mchakato wa katiba mpya bila tume huru ya uchaguzi ila itakapofika wakati wa kupiga kura kuipitisha hio katiba jueni tutatumia tume hii hii ambayo itakuwa ni rahisi hata kwa watawala kuamua ipite au lah
So kama zikiundwa sheria mpya tukapata kwanza tume nzuri ya uchaguzi it will be helpful sanaaa
 
Lengo la Zitto ni kurudi bungeni at any cost,

Je, ana uhakika gani akipata tumehuru atashinda na chama chake kuwa na wabunge wengi watakaopitisha katiba mpya?
Wewe ndio maana Maisha yalikushinda ughaibuni, maana HUNA AKILI kabisa.
 
Achana na Mr Zero, Katiba mpya sio kwa ajili wapinzani, wanasiasia na wanachama tu, Katiba mpya ni kwa Watanzania wote milioni 60 ambao wengi wao hawajui hata kadi za vyama zikoje.
Kwamba watanzania Milioni 60 wawe wanahitaji Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi halafu wasipate?

Vijana wa Mbowe punguzeni bange Pombe Kali na UGORO.
 
Ukisema subset na mtu alikimbia hesabu unampa kazi sana. Subset ni zaidi ya english , tume huru haiwezi kuzaa katiba kwakuwa yenyewe nimtoto wa katiba
Kweli Zitto umefikia uwezo huu mdogo wa kufikiria? Hiyo tumehuru lazima iwe backed na sheria mama ambayo ni katiba, pasipo katiba mpya tume huru sahau.

Kumbuka katiba inasema rais akishatangazwa matokeo hayawezi kupingwa.

Sheria za uchaguzi zipo hovyo na hivyo kupelekea uundwaji wa tume kuwa hovyo.

Tume ni subset ya katiba na katiba sio subset ye tume. Hivyo katiba kwanza ndio tumehuru.
 
Kumbuka pia ile rasimu ya katiba ya warioba ilifinyangwa huko bungeni that means kuwepo bungeni kwanza ni muhimu pia !! Maana kama majority ya wabunge wangekuwa wanaikubali ile rasimu isingetupwa kapuni ! I stand to be corrected!
Una uhakiga gani atapata wabunge wengi.
 
Katiba mpya ni blaaa blaaa za Wapinzani kutaka uchochoro wa kupata madaraka kwa njia ya Mkato

Huku Mtaani kwa wapigakura ushaskia kuna hizo mambo?

..wapinzani na wanaharakati wakati mwingine inabidi wawe ahead of time kulinganisha na chama tawala na wananchi kwa ujumla ili kuleta MABADILIKO / MAMBO MAPYA.

..Wananchi wakiwatangulia wapinzani kuidai katiba mpya maana yake ni kwamba nchi imechelewa kushughulikia jambo hilo. Kwenye nchi nyingine hali hiyo huleta VURUGU.
 
Zitto mwnyw Sasa baada ya picha ya X-ray[emoji4]
IMG_20210929_172911.jpg
 
Zitto anajivua nguo sebuleni.Hivi hajui kwamba katiba ndiyo sheria-mama/sheria-msingi/sheria kuu?Unapataje tume huru bila sheria inayoitambua na kuiongoza?Afute kauli.

..Michakato ya kupata Tume Huru na Katiba mpya inatakiwa iende kwa pamoja.

..Hili suala linahitaji MARIDHIANO na sio upande mmoja kushambulia upande mwingine.

..CCM wanataka kutokee ugomvi kati ya Tume Huru vs Katiba mpya ili tufike 2024/25 tukiwa tumekosa vyote.
 
Jamani unaanza kuchamba Kisha unajisaidia haja kubwa au unajisaidia kwanza ndio ukimaliza uchambe?
You cannot put the cart infront of the horse and expect any work to be done.
Katiba mpya ni blaaa blaaa za Wapinzani kutaka uchochoro wa kupata madaraka kwa njia ya Mkato

Huku Mtaani kwa wapigakura ushaskia kuna hizo mambo?
Hivi katiba mpya inasaidiaje wapinzani kupata madaraka?!
 
Back
Top Bottom