Zitto Kabwe apendekeza TANESCO wauze hisa(20%) fedha itakayopatikana ilipe madeni, Waziri Makamba atoa maagizo

Baada ya mikataba mibovu sasa wataka kulichukua shirika zima
 
Hivi tanesco inapataje hasara, wajuvi tunaomba mtupe majibu. Ni vipi hili shirika linapata hasara?
 
Wanataka kuibinafsisha TANESCO haki ya Mungu familiya za JK na Makamba zitakuwa na mwisho mbaya sana, Tamaa na ubinafsi itawaangamiza
Hizi ni mbinu za kujiuzia hili shirika..zito na jk na makamba ni timu Moja..kama magufuli aliweza kutumia mabilioni kuliokoa shirika la ndege ni kwa nini wasifanye hivyo kWa tanesco
 
Shirika linadaiwa zaidi ya bil 300...alafu uniambie niiweke fedha zangu hapo..ila unakumbuka swala la tozo lilivyoanza? Waliongea hivi kimasihara mwisho wa siku ikawa hivyo..na hii nakueleza kuna kina kinasukwa na kina jk ...kumtoa Ruge na week hiyo hiyo kumteua january
 
Wewe hauoni labda hawa 20% watatufunulia kujua kwanini kila mwaka ni Loss? kwasababu 20% watahitaji more transparency and accountability!
Haiwezekani...labda kama wangeuza 51 wajiondoe kwenye uongozi ..tatizo la mashirika ya imma mengi ni matumizi makubwa kuliko kinachoingizwa..na mbaya zaidi sera wanatungiwa na wanasiasa..ila hili shirika libaki kuwa la serikali ..huwezi kubinafsisha tanesco kwenye nchi masikini kama tanzania
 
Tanesco sio independent entity..wala sio corporation...
Tanesco ni sawa na Halmashauri..
Kila kitu wanapokea maagizo kutoka juu
Makusanyo yote wanapeleka hazina
Halafu wanaomba pesa za matumizi

Sasa haya yana fit vipi kwenye set up hiyo?
Umeandika point ya msingi Sana.
Kwa uzoefu mdogo, yawezekana mteja wa hizo hisa yupo around.
Anyway! Na reli walipewaga wahindi sijui hata stori zake
 
Lazima ukose akili na maarifa ndiyo ukanunue hisa za TANESCO. Shirika halijawahi kupata faida hata mwaka mmoja tangu lianzishwe, ukanunue hisa, kwaajili ya nini?
Bwawa likianza kuzalisha je??hakutakuwa na faida bado??
 
Kwa vitabu 2018. Tanesco total assets ni trilioni 8.7?!!!!!!
That’s the number, halafu mtu anakwambia (based on book value) 20% izalishe over 6 trillion ya kulipa madeni na kufanya investment zingine.

How is that possible bila ya kufanya market value ya biashara ujue hisa uuze kiasi na ngapi kufanya hiyo mipango yako; wazimu wanao ongeaga kule Twitter unawatosha wao wenyewe.
 
Wawekezaji wengi Tanzania kwenye umeme wanataka wawe kwenye hpande wa uzalishaji halafu waiuzie Tanesco, kwa nini wasizalishe na kusambaza wenyewe? Jibu ni moja, watanzania hawana tabia ya kulipa madeni hivyo hakuna ambae yuko tayari kubeba hasara.

Ndio maana wao wanawekeza kwenye kuzalisha halafu wanailazimisha tanesco inunue kwao iuze, watu walipe bill wasilipe haiwahusu wao wanamkaba koo tanesco.

Tukiacha siasa, taneeco itafika mbali.
 
Eleweni January ndio mwanya wake wa kupata pesa za kutafuta uraisi in future.Tegemeeni sanaaa Mambo ya Richmond, dowans etc
Zitto kabwe kwanini kafungua kinywa katika hili..mnaounganisha dot mtaelewa chain ya zitto na January.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwani DSE ni kama soko la Kariakoo?
Nijuavyo, kuna vigezo rundo mpaka kampuni isajiliwe, ikiwemo KUTENGENEZA FAIDA KWA MIAKA 3 MFULULIZO.
Urafiki Textiles walitaka kutumia hii janjajanja ya Zitto kupiga hela, DSE wakawagomea.
Je kuna shirika la umma lililosajiliwa DSE?
 
Naihifadhi hii comment
 
Relax Brother, hebu soma nilipoanzia 20% haiwezi kuwa na impact yoyote katika maamuzi maana hata board hawataweza kuiunda, angalia juu kabisa hizi ni assumptions zangu ambazo ni kama guessing tuu.

Again can you buy shares without being full informed on management accounts?
 
Ni
Kweli lakini ili watu waweze kununua shares si lazima wawe well informed au ndio wanaenda kutupa capitals zao, kwa namna yoyote hata kama ni ndogo itabadilisha operational style whether postive or in negative way.
 
Well sina uhakika na sheria za Tanzania on the regulation of issuing IPO (kwa nchi zingine faida sio swala la msingi).

Lakini kumbuka ‘Swala Oil’ (kampuni ya oil and gas exploration ya Mengi) ilikuwa aina ata operations na ikasajiliwa so I don’t know exactly ni nini kilichozuia urafiki.

But the issue hapa how does one justify 20% ya TANESCO shares is enough to pay for their long term debts and leave enough to do other investments (from what evaluation) zaidi ya kujiropokea tu.

Besides TANESCO tatizo lake sio madeni pekee, CoS ni kubwa kushinda revenue; sasa badala ya kuangilia nini shida hapo wanakimbilia solution za baadae tena bila ya hata kujua thamani ya hisa.

Anyway wacha niachie hii mada hapa, just wanted to highlight the thought nonsense in all of this.
 
Nani anunue hisa za shirika mfu kama TANESCO
Shida ya wana siasa wetu wengi wanataka kutengeneza fursa za kuchukua bure mali za umma. Kubinafshisha Tanesco kwa weledi itasaidia. Nakumbuka TRC nayo ilibinafishwa. Ikaishia kutegemea tena aliyeibinafisha.
National interest ziwe sehemu ya agena zetu na sio kutaka utajiri ambaop ipo siku watanzania watataka kujua mahesabu yake
 
Wawekezaji wapo tayari kuzalisha na kusambaza umeme, kikwazo ni sheria iliyotungwa na wanasiasa, kwa sababu wanazojua wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…