Pre GE2025 Zitto Kabwe ashauri vyama vya Upinzani kusimamisha Mgombea mmoja wa Urais katika uchaguzi ujao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
1,242
Reaction score
4,813
Your browser is not able to display this video.
Kiongozi mstaafu wa Chama cha ACT- Wazalendo Zitto Kabwe, akizungumza na Crown Fm ametoa rai yake kuhusu Upinzani kuungana na kuwa na mgombea mmoja. Akizungumzia jambo hilo Zitto amesema:

Ni wakati Vyama vya upinzani kuweka pembeni tofauti zao na kukaa pamoja kurekebisha makosa yaliyopita kuwa na mgombea urais mmoja katika uchaguzi ujao.
Soma Pia:
 
Naungana na zito katika hili. Hata hivo walichelewa. Vyama vya upinzan vikiungana ccm chali.
 
Huu ni mkenge wa enzi za UKAWA
 
Aache kuhadaa watu.
Je sheria inaruhusu vyama kuungana?

Na ana uwezo huo yeye kushawishi vyama mamluki wa Ccm kuungana na upinzani?
 
UKAWA
 
Kipigo kwa ccm kiko pale pale , hata chadema ikisimama kivyake , japo naunga mkono mashirikiano
 
Kuweni makini naye, anaweza kuja na mgombea wake mfukoni halafu dakika za mwisho anamwacha solemba ili kuwasafishia njia waleeeee!!!
 
Ccm ina vyama vyake kwenye kambi ya upinzani ambavyo hufanya kazi yake. Kuungana na vyama hivyo ni kujiandaa kucheza midundo ya mbogamboga
Bila wapinzani kuungana ccm haing'oki wala kutetereka, endeleeni kujifanya wapinzani kweli kuliko wenzenu muone mtaishia wapi
 
wizi wa kura na matumizi ya dola ni fasheni watafanyaje
 
Kwanza sijamskikia Kauli yake kuhusu Kutekana na Kuteswa na wasiojulikana.

Ameibuka tu na Mgombea mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…