tanga kwetu
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 2,193
- 1,437
Kazi za mbunge zimeanishwa wazi kabisa hiyo ya kuwasiliana na benki ya dunia kwa kutumia Ofisi ya bunge na karatasi yenye nembo ya bunge haimo kwenye kazi za mbunge.
Ikiwa umehukumiwa kifo, kimakosa, na Zitto anakutetea kwa kusimamisha msaada wa nchi mpaka upewe hukumu ya haki.
Halafu anakuja mtu na kusema kwamba, Zitto asisimamishe msaada, kwa sababu wewe anayekutetea ni mtu mmoja tu, akuache uuawe, ingawa umehukumiwa kimakosa.
Utakubaliana na hoja hiyo na kukubali kuuawa kimakosa?
Sent using Jamii Forums mobile app
Sielewi... naomba unielimishe TafadhaliKuruhusu mabinti waendelee na masomo si kukubali kwamba mabinti kupata mimba ni sawa.
Unaelewa hilo?
Unaelewa kwamba kuna mabinti wanapata mimba kabla ya kupata majority age na hivyo hawatakiwi hata kuwajibishwa kwa kupata mimba ambazo basically zinatokana na statutory rape?
Unaelewa statutory rape ni nini?
Unaelewa majority age ni nini?
Unaelewa kwamba mkono ukishika mavi haukatwi, unaoshwa?
Sent using Jamii Forums mobile app
Huelewi nini?Sielewi... naomba unielimishe Tafadhali
Ni sawa, unachosema, vyovyote vile anatambulika na WB. Hata wewe hapo ulipo, WB wanakutambua aidha kama raia wa Tanzania au kwa cheo kingine uchochte lichonacho, hata kama hakina uhusiano na malaka za Serikali. Na kwa swala hili basi, alitakiwa aandike barua aidha kama mtu binafsi, au Kiongozi wa ACT Wazalendo, na si kama Mbunge kwa sababu Bunge halikuwa na hoja hiyo. Hapa kinachogomba ni kuwa ameandika barua kama Mbunge, kulisingizia Bunge hoja ambayo halikuwa nayo, ni hoja ya chama chake au ya kwake binafsi. Amefanya vizuri lakini kwa sababu amejiingiza kwenye target ya Bunge pasipo mwenyewe kujuaUnapokuwa mbunge kwenye Bunge la Tanzania ujue kuwa ubunge wako unatambuliwa na Jumuia ya Madola kwa sababu Bunge la Tanzania ni mwanachama wa mabunge ya Jumuia ya Madola.
1) amejua kujenga na kutetea hoja wakamuelewa
2) Zitto kawakilisha tu kundi kubwa la watetezi wa haki elimu kwa wasichana wa Tanzania
3) Ndugai, bunge lako limekuwa part ya serikali.....limekuwa hovyo kabisa na dawa ni kuli-bypass
4) afuate urasimu wa kuwasilisha mabadiliko ya sera wakati document linasogea mbele?
5) hata angeleta hoja bungeni, jibu tunalijua kwamba mngekataa
Mkuu Ni muda gani zitto anakuwa si mbunge? Huko shuleni mnaenda kusomea niniNi sawa, unachosema, vyovyote vile anatambulika na WB. Hata wewe hapo ulipo, WB wanakutambua aidha kama raia wa Tanzania au kwa cheo kingine uchochte lichonacho, hata kama hakina uhusiano na malaka za Serikali. Na kwa swala hili basi, alitakiwa aandike barua aidha kama mtu binafsi, au Kiongozi wa ACT Wazalendo, na si kama Mbunge kwa sababu Bunge halikuwa na hoja hiyo. Hapa kinachogomba ni kuwa ameandika barua kama Mbunge, kulisingizia Bunge hoja ambayo halikuwa nayo, ni hoja ya chama chake au ya kwake binafsi. Amefanya vizuri lakini kwa sababu amejiingiza kwenye target ya Bunge pasipo mwenyewe kujua
Kwenye mkopo sio mabeberuTukubaliane kwanza wale WB ni mabeberu au sio mabeberu...?
Kwa kutoa maoni yake? Hill bunge litakuwa limekosa kazi ya kufanya.bunge limebaki kubariki kila uchafu unaofanywa Na serikaliBunge liazimie Zitto azuiwe Vikao vya Bunge mpaka 2025, kwa maana hata akishinda Uchaguzi ujao abaki kwenye kifungo
Sent using Jamii Forums mobile app
kumbe sindano imewakolea?Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai amesema kama kulikuwa na tatizo la kisera, ni mambo ya kujadiliwa bungeni. Sio mara ya kwanza kutokea sera zikawa na udhaifu au zinahitaji maboresho.
Anasema Zitto alipaswa awasilishe maoni yake na mapendekezo kuhusu ubovu wa sera ya elimu kisha litazamwe. Ndio kazi za bunge. Sasa yeye anaenda kupiga kelele nje ya nchi kwa sababu hakubaliani na sera kweli?
Awajibishwe.
=========
Leo Ijumaa Januari 31, 2020 bungeni jijini Dodoma, Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema wanamsubiri Zitto awaeleze kwa nini aliandika barua hiyo.
“Mtu unaweza kuwa na tofauti na sera au mtazamo kati ya wewe mbunge au upande wa Serikali na kadhalika, lakini kufikia mahali pa ‘kublock’ Tanzania isipate fursa fulani nadhani ni kwenda mbali mno.”
“Kwa sababu watoto watakaokosa fursa hiyo ni watoto wa Tanzania ni walimu wa Tanzania ni miundombinu ya elimu ya Tanzania, sijui katika hilo kama mbunge unanufaika nini maana kama ni suala la utofauti la kisera haya ni mambo ya kujadiliana tu,” amesema Spika Ndugai.
Katika kusisitiza hilo, Spika Ndugai amesema, “ningependa kutoa ushauri wa ujumla tu kwamba ni vema kutumia fursa yetu kama wawakilishi wa wananchi tukaelimishana tukaelezana kuliko kuwakosesha Watanzania fursa wakati baadhi yetu watoto wetu wapo Feza Boys, wapo Marian Girls halafu unablock msaada kwa watoto walio wengi wa wapiga kura wetu jambo ambalo halifai kabisa.”
Hata hivyo hapo jana Waziri wa zamani wa Viwanda na Biashara nchini Tanzania, Joseph Kakunda alisema kitendo cha Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kuandika barua ya kutaka kuzuia mkopo wa elimu unaotolewa na Benki ya Dunia (WB) ni kituko nani aibu.
Kakunda aliyasema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akichangia taarifa za kamati za Bunge za bajeti na Uwekezaji na Mitaji ya Umma.
“Naomba nizungumze masikitiko yangu dhidi ya barua moja ambayo mwenzetu mmoja (Zitto) ameiandika kutaka kuzuia fedha za miradi ya elimu ni kituko na ni aibu sana kwetu sisi wabunge kuona mwenzetu ameandika barua,” alisema Kakunda ambaye pia ni Mbunge wa Sikonge (CCM) mkoani Tabora
Alisema barua hiyo wangekuwa wameandika watu wa mashirika yasiyo ya kiserikali yeye asingestuka sana lakini kuandikwa na mbunge mwenzao wakati Serikali imepeleka Sh1 bilioni kwa ajili ya kukarabati Sekondari ya Kigoma iliyoko kwenye jimbo lake ni jambo la kusikitisha.
“Sasa hivi Sekondari ya Kigoma ni kama mpya. Na vilevile Serikali imepeleka zaidi ya Sh4 bilioni kwa ajili ya kuboresha elimu. Sasa anazuia zisije kwa haraka kwa ajili ya kuwasaidia watoto wa kitanzania nieleze masikitiko makubwa sana,”amesema.
“Nilitamani nipaze sauti huko aliko anisikie lakini kwa sababu yuko mbali naachia hapo lakini atasikia kutoka kwenye Hansard (kumbukumbu Rasmi za Bunge)" alisema Mh. Kakunda
Hats wewe pia