Zitto Kabwe aunga Mkono Serikali 3 baada ya Hotuba ya Jaji Warioba Dodoma

Zitto Kabwe aunga Mkono Serikali 3 baada ya Hotuba ya Jaji Warioba Dodoma

Tanzania ni Nchi inayojitegemea kutokana na aina wa Muungano wetu, hatuna haja ya kuiga hiyo miundo mingine ya "nchi nyingine duniani"

muundo wa serikali 3 haufai, ni kujiongezea gharama kwa kutaka kujifurahisha, furaha ambayo haitadumu, hapa tunaanza safari ya kuua muungano, warioba pia amekiri challenge kubwa ni gharama, kwanini kuwatesa wananchi kwa matakwa ya wanasiasa wenye UCHU?? Tuboreshe tulichonacho kuliko kuongeza matatizo..
 
Muungano wa serikali 2 kwa miaka hamsini imeshindwa kuondoa kero. Mchakato wa kuelekea serikali moja ambao ilikuwa uanze mara tu ya Muungano miaka hamsini iliyopita, hata agenda haijawekwa mezani. Bado wengine wanaamini kitu ambacho kwa uchambuzi wa kina muungano wa serikali moja haiwezekani. Ni heri tujaribu serikali tatu. Na hii ikishindikana basi tutengane kimoja na tubaki na ujirani mwema. Tugange linalowezekana sio nadharia.

matatizo yapo kwa wanasiasa wanaotaka kuchukua nafasi hii kuona muungano unakufa, kwanini muungano huo haukuwa tatizo 40 yrs ago?? tumeanza kuwa na kizazi kisichojali misingi bora tuliyowekewa na babu zetu, tumepotoka na tunakoelekea ni kuiua hii nchi, historia itatuhukumu kwa kuwa waroho wa mambo madogo na kuacha kuangalia faida za kuwa na serikali moja imara yenye amani na maelewano, wakati ni sasa wa kuacha faida binafsi za muda mfupi na kuangalia vizazi vijavyo vyenye muungano bora,
 
katiba ya Jamhuri ya MUUNGANO WA TANZANIA, haijasema hivyo, hivyo amendment hiyo ni BATILI ON THE EYES OF THE CONSTITUTION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, 1977.

nibatili kivipi wakati tayari inatumika na katiba ya muungano inaifwata mfano kuchelewa kwa ukusanyaji maoni kulisubiri baraza la wawakilishi Zanzibar liizishe azimio toka bunge la jamhuri ubatili wake uko wapi Zanzibar sasa hivi ni sovereignty government ambayo haijazinishwa!!!!
 
muundo wa serikali 3 haufai, ni kujiongezea gharama kwa kutaka kujifurahisha, furaha ambayo haitadumu, hapa tunaanza safari ya kuua muungano, warioba pia amekiri challenge kubwa ni gharama, kwanini kuwatesa wananchi kwa matakwa ya wanasiasa wenye UCHU?? Tuboreshe tulichonacho kuliko kuongeza matatizo..

mkuu panua kichwa chako hata hizo gari za gharama zinaongezea wananchi mzingo tatizo la ccm wanapenda ccm iendele kuwa state party baadala ya political party legitimate hiyo haipo mkuu wajipange upya
 
Kwanini serikali 3?? kama si ulafi wa wanasiasa wachache, nini cha ziada? tuvunje Muungano tu - ndio suluhisho. Zanzibar waende kivyao na Tanganyika/Tanzania twende kivyetu na nina uhakika majority kutoka pande zote watakuwa happy tu
 
Hakuna Muungano wa nchi mbili duniani ulishawahi kuwa na serikali mbili,Tanzania ni ya Kwanza.Pia Tanzania inaweza kuwa ya kwanza kuwa na serikali TATU.Ni maamuzi ya sisi wananchi, na si kutazama wenzetu wakoje, ilimradi hatuvunji sheria yeyote.CCM mnalia tu serikali tatu hazitufai, ila hamsemi kwa nini mbili, na pia hizo kero zilizowashinda katika kipindi chote hicho, je!mtaziweza sasa?wapi paliwashinda?na kwa nini?Nini mwafaka baada ya kushindwa kutatua hizo kero ambazo leo mnatuambia kuwa mtazifanyia maboresho?Zanzibar ni nchi ama si nchi?Na kama ni nchi, Tanzania ni nini?Wapi Tanganyika?Muunganmo wa Kweli ni SERIKALI MOJA YA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ambapo Zanzibar na Tanganyika wanakubali ku surrender mamlaka zao na kuzikabidhi kwa Jamuhuri ya Muungani wa Tanzania.Ikishindakana, Tanganyika iwe na mamlaka, na zanzibar iwe na mamlaka na wote hawa waunde serikali itakayowaunganisha. Kinyume cha hapo, HAKUNA HAJA WALA FAIDA YA HUU MUUNGANO!NI BORA KILA MTU ABEBE CHA KWAKE.HATUTAKUWA WA KWANZA.USSR walifanya, SeneGambia Walifanya, nk.

hapo umenena mkuu.
 
matatizo yapo kwa wanasiasa wanaotaka kuchukua nafasi hii kuona muungano unakufa, kwanini muungano huo haukuwa tatizo 40 yrs ago?? tumeanza kuwa na kizazi kisichojali misingi bora tuliyowekewa na babu zetu, tumepotoka na tunakoelekea ni kuiua hii nchi, historia itatuhukumu kwa kuwa waroho wa mambo madogo na kuacha kuangalia faida za kuwa na serikali moja imara yenye amani na maelewano, wakati ni sasa wa kuacha faida binafsi za muda mfupi na kuangalia vizazi vijavyo vyenye muungano bora,
uko sahihi mkuu maana umepata stroke, stroke huwa ni tatizo baya sana kiafya, linaweza kuathiri hata uwezo wa kufikiri. Kwa kuwa Tanganyika haupendi irudi katika enzi yake , bali unataka serikali mbili na nchi mbili na sio nchi moja, unaonaje sasa uwashawishi Wazanzibari wakubali kuvunja serikali yao na nchi yao, maana wameendesha serikali yao kwa kipindi cha miaka 50, sasa iwe zamu ya Tanganyika, nasi tuendeshe serikali ya Jamhuri ya Tanganyika kwa miaka hamsini, yaaani iwe ni kupokezana, Jamhuri hii ikifikisha miaka 50, iwe zamu ya Zanzibar tena kuendesha serikali yao, si itapendeza!!!
Ili hilo wazo likubaliwe patachimbika kama unadhani natania kawagise Wazenj na wazo hilo, uone moto wake!!! kajaribu!!

Kama hilo haliwezekani, basi Jamhuri ya Tanganyika, Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba waridhie maoni ya Watanganyika na wengine yaliyowasilishwa kwao na Jaji Mkuu Mstaafu,Waziri Mkuu Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu, Jaji Warioba kwa niaba ya Wananchi wote
 
uko sahihi mkuu maana umepata stroke, stroke huwa ni tatizo baya sana kiafya, linaweza kuathiri hata uwezo wa kufikiri. Kwa kuwa Tanganyika haupendi irudi katika enzi yake , bali unataka serikali mbili na nchi mbili na sio nchi moja, unaonaje sasa uwashawishi Wazanzibari wakubali kuvunja serikali yao na nchi yao, maana wameendesha serikali yao kwa kipindi cha miaka 50, sasa iwe zamu ya Tanganyika, nasi tuendeshe serikali ya Jamhuri ya Tanganyika kwa miaka hamsini, yaaani iwe ni kupokezana, Jamhuri hii ikifikisha miaka 50, iwe zamu ya Zanzibar tena kuendesha serikali yao, si itapendeza!!!
Ili hilo wazo likubaliwe patachimbika kama unadhani natania kawagise Wazenj na wazo hilo, uone moto wake!!! kajaribu!!

Kama hilo haliwezekani, basi Jamhuri ya Tanganyika, Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba waridhie maoni ya Watanganyika na wengine yaliyowasilishwa kwao na Jaji Mkuu Mstaafu,Waziri Mkuu Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu, Jaji Warioba kwa niaba ya Wananchi wote

Na mimi napendekeza kuwa sasa ni ZAMU ya Zanzibar kuwa kama Tanganyika! Kivipi? Iwepo Serikali 2 yaani Serikali ya Jamhuri ya Zanzibar itakayoshughulikia mambo ya Zanzibar na ya Muungano, halafu kuwepo na. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ambayo ni huru,itakayoshughulikia mambo ya Tanganyika tu, kwani ni Zamu ya Watanganyika nao kupumua! Hiyo ni kama muungano uwe wa serikali2, la sivyo serikali 3 haziepukiki!
 
Na mimi napendekeza kuwa sasa ni ZAMU ya Zanzibar kuwa kama Tanganyika! Kivipi? Iwepo Serikali 2 yaani Serikali ya Jamhuri ya Zanzibar itakayoshughulikia mambo ya Zanzibar na ya Muungano, halafu kuwepo na. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ambayo ni huru,itakayoshughulikia mambo ya Tanganyika tu, kwani ni Zamu ya Watanganyika nao kupumua! Hiyo ni kama muungano uwe wa serikali2, la sivyo serikali 3 haziepukiki!
AhAAAAAAAHHHaaaahhh!!!! yaani unamaanisha nao watulipie mishahara kama sisi tunavyochangia bajeti yao kiaina, watulipie bill za umeme kama sisi tunavyofanya, te te te te h!!! watakimbia nchi mkuu
 
Zitto ameonekana Kufurahishwa na ufafanuzi wa Jaji Warioba na hata Kupelekea kuwashawishi Wajumbe wenzake kwamba, hawana budi kujadili namna ya Kuuboresha zaidi muundo huo wa Serikali tatu badala ya kujadili Serikali mbili ambazo yeye mwenyewe amekiri kwamba hazitakuwa Suluhisho la Kero za muungano kupitia ukurasa wake wa facebook.

Hii imemtokea baada ya jana Kuusikiliza kwa makini ufafanuzi wa Jaji Warioba kuhusu muundo huo wa Serikali tatu, pia Kwa mujibu wa Maelezo ya Julius S. Mtatiro Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge maalum la Katiba amesema Idadi kubwa ya Wajumbe wa CCM, jana baada ya kutoka ndani Ukumbi wa Bunge, walionekana kuridhishwa na ufafanuzi wa hotuba ya Warioba huku wengine wakitamka wazi kuwa Serikali tatu ndio mpango mzima.

Nawasilisha!

Chanzo: Zitto Kabwe's facebook page....

Mtanzania yeyote mwenye akili timamu hawezi kupingana na maelekezo muhimu ya Jaji Warioba... kwa maana nyingine watanzania wamefika katika hatua muhimu ya historia ya nchi yao....Jaji Warioba na tume yake wamefichua mambo yaliyofichika takribani miaka 30 nyuma... utashi wa Tume hiyo kwa watanzania unabaraka tele kwa wa Tanzania walio wengi... Mungu atawabariki wajumbe wote walioamua kufunguka na kuacha unafiki ambao umezoeleka miongoni mwa viongozi walio wengi... wanaopenda sana kujaza matumbo yao na kuangalia ubinafsi ... kusahau taifa linataka nini .. viongozi waliopata nafasi kuwa madarakani wanajisahau na kuwasahau waTZ ...

 
Kumbe watanzania wengi ni wavivu wa kufikili yaani kwa kero hz tuu ambazo zinazungumzika leo tunakata tamaa na kuona mfumo uliopo wa serikali ndio tatizo? Nadilikikusema tumepotea na hoja hii inapaswa kupingwa kwa nguvu zote, hv hii tume inajuwa afya ya serikali tatu na mbili ipi bora? Au wamekurupuka tuu?.
pinga hoja za warioba kwa hoja cyo kwa nguvu, miaka yote hiyo kero zinazidi kuongezeka, mmlikuwa wapi kuzizungumzia hadi zanziba ikavunja katiba?
 
Serikali 3! Ama suala la muundo wa kiutawala uweje, hiyo ndo inapaswa iwe kazi ya Bunge Maalum la Katiba kuboresha yale maoni ya Wananchi!

Bahati mbaya ni kwamba hao wajumbe wote hakuna nayefikiria kuhusu muundo wa Muungano, bali wanawaza Serikali 3. Serikali tatu maana yake si ni kwamba kila Seriklai iwe na mamlaka yake ?
 
huo ni mtazamo wake, hakuna nchi duniani yenye serikali tatu, labda sisi tuwe wa kwanza..3 hazina tija yoyote kufurahishana wakati tunaingia hasara, siungi mkono, suluhisho ni serikali moja tu

Jenga hoja kiongozi, kikubwa ni hoja kama zina mashiko husije ukatuletea ooo gharama za kuendesha serikali 3 ni kubwa wakati pesa zinazo ibiwa kwa kila mwaka ni nyingi mara 4 ya kuendesha hizo serikali 3.
 
Acheni Viroba bavicha Soma msimamo wa ZZK toka February.Tatizo mnakurupuka kama mmetoka usingizini.
Zitto Z Kabwe shared a link.

February 20


Muundo wa Muungano: Serikali Tatu, Moja, Mbili? Zote!

Zitto Kabwe

Mwalimu Azaveli Lwaitama ni mwalimu na mlezi wangu nje ya darasa. Alipokuwa Katibu wa Umoja wa Wanataaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mimi nilikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Idara ya Uchumi. Nilikuwa nashinda kwenye Ofisi ya UDASA tukijadiliana kuhusu Umajumui wa Afrika (Pan-Africanism), Ujamaa na harakati za kulinda haki za watu. Ilikuwa ni nadra kwa mwanafunzi wa uchumi kuwa karibu na mwalimu wa lugha na mnadharia mkubwa. Wanafunzi wa uchumi tulikuwa tunajidai na kujivuna. Tulikuwa tunajiona bora sana maana darasa letu halikuwa linazidi watu 40 na kwa kweli wote hawamalizi. Darasa langu tulimaliza wanafunzi 25 tu kati ya 40 tulioanza. Mwalimu Lwaitama ni mpenzi mkubwa wa Muungano kama nilivyo mimi. Tumeapa kuulinda kwa namna yeyote ile. Yeye alikuwa mhafidhina (conservative) sana akitaka Muungano wa muundo huu aliouacha Mwalimu Nyerere. Mimi nataka kuulinda kwa kuufanyia marekebisho makubwa sana ya kimuundo. Hatukuwa tunakubaliana.

Wiki iliyopita Mwalimu Lwaitama kaandika kuhusu muundo wa Muungano katika makala zake za kila wiki katika gazeti la kimombo la The Citizen. Amebadili msimamo. Ameona sasa muundo wa Muungano ulivyo sio endelevu. Ametoa mapendekezo niliyoyatoa siku za nyuma katika mazungumzo yetu ingawa yeye bado anayasema kwa shingo upande. Lwaitama sasa anataka Serikali mbili zilizonyumbuliwa. Anapendekeza Waziri Mkuu wa Muungano mwenye nguvu za za kitendaji. Nampongeza kwa kuboresha mawazo yake.

Hata hivyo bado Mwalimu wangu na Watanzania wengi wamejikita katika mjadala wa Serikali ngapi. Idadi ya Serikali inaonekana kama ndio dawa ya kero za Muungano. Ni kweli Wazanzibari wanataka uhuru zaidi na wengine hawataki kabisa Muungano. Unawalalia. Unawanyima uhuru wa kuamua baadhi ya mambo yao na japo halisemwi unawanyima wanasiasa wa Zanzibar mamlaka ya masuala mengine ambayo yangewafanya wajilimbikizie madaraka.

Huku bara napo kuna watu, tena wanaongezeka kwa kasi kweli kweli, wakitaka Tanganyika yao. Tena wengi vijana. Demografia zetu zinaonyesha kwamba Watanganyika waliozaliwa Tanganyika ni takribani asilimia 12 tu ya Watanzania. Asilimia 70 ya Watanzania wamezaliwa wakati Muungano umeshasherehekea miaka 15 ya kuzaliwa kwake. Lakini wanataka Tanganyika yao. Wamechoshwa na kelele za Wazanzibari. Hawawataki Wazanzibari kujaa kwenye Bunge la Muungano wakati wapo kiduchu sana. Wanasiasa nao, japo hawasemi waziwazi wanataka wawe na mamlaka zaidi bila kulazimika kushauriana na wanasiasa wa Zanzibar. Linapokuja suala la wagombea Urais ndio kabisa wanakereka kutafuta mgombea mwenza kutoka Zanzibar. Wachambuzi wa historia za kisiasa siku wakiamua kufanya tafiti watachoka na roho zao watakapoona aina za wagombea wenza ambao wagombea Urais huteua, hasa kutoka sisi vyama vya upinzani.

Kimsingi idadi ya wapinga Muungano inazidi kuongezeka siku hata siku. Ukiwauliza kwa nini hawataki Muungano wanasema aah, basi tu. Kama ni Mzanzibari atasema Tanganyika wanatutawala. Kama ni Mtanganyika atasema Wazanzibari wamezidi kelele, tunataka Tanganyika yetu. Sisi ‘Unionists’ (Wanamuungano) nao hatuna majibu ya kuridhisha sana na ya kukonga nyoyo. Isipokuwa tu, Muungano huu ni wa aina yake Afrika na Duniani. Ni alama pekee ya kuonyesha Mwafrika kupinga mipaka ya kikoloni. Sasa hili haliwaingii kichwani ‘secessionists’ (Wanautengano) na hatuna la kuwasaidia. Lakini ni lazima tuurekebishe Muungano huu. Ulivyo sasa utavunjika tu. Kuulinda Muungano ni kuufanyia marekebisho makubwa. Mwalimu Lwaitama kaliona hilo. Pendekezo lake liboreshwe sasa. Sio rahisi sana.

Sasa tufanyeje? Serikali moja itaimeza Zanzibar. Serikali Tatu ni gharama kuendesha na Serikali mbili zimeimeza Tanganyika na watu wanataka Tanganyika yao na zinainyima uhuru Zanzibar na watu wanataka wawe huru zaidi. Mfumo wa Serikali ngapi na kadhalika ni moja ya mikakati ya wanasiasa katika kusaka vyeo. Sisemi sio halali kujadili lakini kiukweli mfumo gani wa Muungano hautaongeza fungu la dagaa kwa mwananchi wa Kagongo au sinia la ubwabwa kwa mwananchi wa Mkanyageni. Waingereza wana msemo ‘unataka kula keki yako na kubaki nayo’, basi tuwe na Serikali zote.

Nimeanza na Mwalimu Azaveli Lwaitama. Naboresha hoja yake kwa kurudia niliyowahi kuyasema huko nyuma kuhusu muundo wa Muungano. Tuwe na Dola Moja tu. Ndio, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wala sio Shirikisho la Tanzania (kwanza litatuondoa kwenye kiti chetu kule Umoja wa Mataifa maana kwa jina letu sisi tunakaa katikati ya Uingereza na Marekani. Katikakati ya mabwana wakubwa, labda ndio maana wanatupa misaada sana, unajuaje?). Tuwe na Rais mmoja tu mwenye mamlaka kamili ya Asasi za Dola – Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Uhamiaji, Sera za Fedha na jukumu la jumla la kusimamia ustawi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Achaguliwe na Watanzania wote wa pande zote mbili za Muungano kwa kupata zaidi ya nusu ya kura za pande zote za Muungano. Tuachane na mambo ya Mgombea Mwenza. Tumejaribu tumeona hana maana zaidi ya kutembea na mikasi tu.

Zanzibar iwe na Waziri Mkuu Mtendaji kwa masuala yote ambayo sio ya Muungano. Tanganyika iwe na Waziri Mkuu Mtendaji kwa masuala yote ambayo sio ya Muungano. Hawa watateuliwa na Rais wa Muungano kutoka chama chenye Wawakilishi wengi katika Baraza la Wawakilishi Tanganyika na Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Wote watakuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa utaratibu kwamba iwapo Rais anatoka Zanzibar, basi Waziri Mkuu wa Tanganyika atakuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na wa Zanzibar atakuwa Makamu wa Pili wa Rais. Kule kule kwenye misingi haswa ya Muungano. Hawa wataongoza Mabaraza yao ya Mawaziri na watakuwa na nguvu ya kuteua na kufukuza Mawaziri wanavyotaka. Hawatakuwa Wabunge katika Bunge la Muungano.

Bunge la Muungano litakuwa dogo lenye Wajumbe wasiozidi 101 pamoja na Rais wa Bunge la Muungano. Wabunge wa Muungano watatoka kwenye mikoa (au Majimbo kama sera ya Majimbo itakubalika). Kwa utaratibu wa sasa kila mkoa utachagua wabunge 2 mmoja mwanamke mmoja mwanaume kwenda Bunge la Muungano. Wajumbe wa Ziada watatokana na uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata kwenye kura za Rais wa Muungano. Idadi hii yaweza kupunguzwa na hata kuwa na Wabunge 51 tu akiwemo Rais wa Bunge la Muungano ambapo kwa mikoa ya sasa kila mkoa utachagua Mbunge 1 na wengine watokane na uwiano. Rais wa masuala ya Muungano atakuwa Mkuu wa Shughuli za Serikali katika Bunge la Muungano na Rais kwa mwaka mara moja atahutubia Baraza la Taifa (Wabunge wa Bunge la Muungano na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka kila upande wa Muungano). Wazungu wanaita hotuba hii ‘State of the Union’ (Hali ya Taifa) na wengine huita ‘Queen’s Speech’ (Hotuba ya Malkia).

Mkuu wa nchi mmoja, Dola moja ya Jamhuri ya Muungano. Serikali mbili na kila upande una Serikali yake yenye mamlaka kamili ya maisha ya watu wao ya kila siku. Haya matatu pamoja na Serikali ndogo ya Muungano. Lakini tutakuwa tumepata kila kitu labda. Wenye kutaka Uhuru mpaka Zanzibar watapata. Wenye kutaka Tanganyika watapata na wenye kutaka Muungano kama Dola yenye nguvu watapata

Magamba jasho hadi ktk visigino.wamezowea vya kunyonga
 
Lazima utakua unasumbuliwa na Maradhi Zittophobia...kama hujui mchango wake katika Taifa Hili..
 
Back
Top Bottom