Zitto: "Majibu ya Sumari ni 'ovyo ovyo'"; atakiwa kufuta kauli!

Zitto: "Majibu ya Sumari ni 'ovyo ovyo'"; atakiwa kufuta kauli!

Hawa ndio wa hatari kuliko hata hao wanaoonyesha sura zao kamili. Hawa ndio wanafiki na ndumilakuwili wanaofoka na kutoa povu leo, lakini mwisho wa siku wanaungana na wenzao kupitisha miswada na bajeti za wizi na ya kitapeli. Toka lini maji na mafuta yakachanganyikana kilaini hivyo ?
Selelii, Kilango, na Ole Sendeka,
Mporogomyi, Kimaro na Mwakyembe
Mwambalaswa, Mpendazoe na Shibuda
Shelukindo, Chegeni na Zambi
hivi tuwaeleweje ?
Acheni kelele zenu za kinafiki
wote mwaogelea kwenye uchafu.
Hivyo wote ni wachafu

Mag3, Nakuunga mkono. Wabunge wa CCM ni wanafki sana kelele nyingi bungeni lakini linapokuja swala la kupitisha Budget ndio hao hao wanakuwa wa kwanza.
 
hongera sana kwanza kwa zitto kabwe kwa kutetea maslahi ya nchi.inaonesha mwenyekiti ni ovyo nae pia pamoja na wabunge wa ccm wengine ambao wanafikiri wako bungeni kwa maslahi ya chama na sio nchi (wananchi).mimi naona tuchapishe karatasi zinazoelezea kazi ya mbunge nini na tukawape wabunge bure hili wajue manake naona kuna wabunge wengine hawajui kazi yao nini.
Tetea kauli yako mkuu.
Tuwekee mfano mmoja au miwili ili tuweze kwenda sambamba.
 
Hawa wabunge wetu inabidi tuwachomoe humo bungeni. kwani kuna utata gani au maudhi gani kuambiwa kuwa umejibu ovyo! kama majibu hayaridhishi na hayana substance nafikiri mheshimiwa kabwe angetumia neno kali zaidi ya 'ovyo ovyo'. Inaudhi sana hawa watu wanatumia kodi yetu na badala ya kutoa michango yenye maana wanakuwa wa kwanza kutaka miongozo, hii ni kutaka kujipendekeza tu! People we have to make these people accountable otherwise let us use ballot box power to throw them out.
 
Sumari hakujibu ovyo ovyo, bali alijibu kijinga. Ni vyema Zitto, akasimama imara maana watanzania wengi tuko nyuma yake. Alichosema ni kwele mtupu. Tulimshuhudia Sumari kwenye Runinga akijibu kijinga!

Mimi ningekuwa Zitto, nigesema alijibu kijinga. Kule kumwambia Slaa, atafute maswali mengine ni ujinga mtupu. Kwani ya Mereremeta yamejibiwa? Inashangaza sana jinsi Mawiri wanavyokuwa na kiburi cha kijinga. Tulishuhudia yale ya Karamagi. Alijibu kijinga na mwishowe za Mwizi zikafika - sasa yuko wapi na kiburi chake?

Ni lazima tupambane kwa nguvu zote kuondoa ujinga kama wa Zumari. Tunakuwa wajinga pia tukikubali kuongozwa na wajinga!

Hongera sana Zitto, songa mbele bila kuongopa. Hongera sana Slaa, kaza kamba watanzania wengi tuko nyuma yako. Tutashinda! Aluta Kontinua!
 
Piganieni SERIKALI isiundwe na WABUNGE. Vinginevyo msitarajie majibu zaidi ya hayo ya akina Mh Sumari!
 
Wamebadilika baada ya wabunge wa Upinzani kuonenyesha kuwa wapo makini na sisi kama wananchi tupo nyuma yao na hivyo kufanya kuwa lazima nao wabadilike, Hivyo Kilango na wengine wamebadilka baada ya Buzwagi tu
 
Ukweli siku zote unauma sana. Alafu hao wabunge wa CCM ni wabaguzi sana, mbona Mudhihiri, Selelii au Mhagama hawakuambiwa wafute kauli?
 
Duh kweli hili ni Bunge tukufu na wabunge wetu wanatuwakilisha vema. Wanaacha kujadili hoja za maana na kushabikia visivyo na kichwa wala miguu. Kwani hovyo hovyo kiswahili ni tusi? Maana yake ni jambo lisiloeleweka, lisilokuwa na mwelekeo maalumu sasa hapo kwa nini wahisi wametukanwa?. Hata bunge lenyewe ovyo ovyo tu!
 
Mh. Zitto anastahili pongezi kwa msimamo thabiti kwani majibu ya hovyo yanabaki kuwa hovyo hata kama hawpendi kusikia maneno hayo.
 
Tumewekewa hansard record ya Mh. Zitto.

Wengine tungeomba, tafadhali, record ya maneno Waziri Sumari, sentensi au paragraph nzima, neno kwa neno.




Vizuri Zitto ametuwekea Hansard ametuelimisha zaidi lakini sisi tulikuwa tunamjibu aliyeanzisha thread na tulivyosikia Sumari akimjibu Dr Slaa kwa namna ya ovyo kabisa
 
Kwa keli Zitto amesema mambo mazito sana. Yafaa bunge na serikali kuafanyia kazi.

Hekooooooooo Zitto Kabweeeeeee
 
Ukweli siku zote unauma sana. Alafu hao wabunge wa CCM ni wabaguzi sana, mbona Mudhihiri, Selelii au Mhagama hawakuambiwa wafute kauli?


Ongezea na Juma Kilimba wa Iramba magharibi aliyewafananisha Mawaziri na mbwa,lipi gumu ovyo ovyo au Mawaziri kufananishwa na mbwa CCM lazima watambue wapinzani ni watanzania na wanawakilisha watanzania bungeni
 
kama majibu hayaridhishi na hayana substance nafikiri mheshimiwa kabwe angetumia neno kali zaidi ya 'ovyo ovyo'.
Tena kuna wakati hata Sitta mwenyewe aliwaonya mawaziri kuacha kutoa majibu ya hovyo na kuwatishia kuwa atawarudisha wakatafute majibu mapya pale itakapobainika kuwa hawakujibu swali ipasavyo. Ajabu kuwa hajawahi kufanya hivyo na busara za watu wengi zinaona kwua majibu mengi ya serikali hayatoshelezi. labda busara za spika Sitta zinamwonyesha kuwa majibu hayo ni muruwa
 
Aaaaaa Zitto, mshkaji wangu ile move niliiona kwenye TV usiku.. nimekukubali nilishindwa kujizuia ilibidi nisimame toka kilipokaa na kupiga makofi Bravo Zitto.. mtoto wa mjusi uzi uwe huo huo.. hivi hitu vinatakiwa kama kumamtu anaiweka hiyo hapa lika mtu anawatch hata wenzetu walioko nje waone,..inagusa sana Heko Zitto!!!
 
Zitto hongera na jua kwamba msimamo wao ni wa wengi, mimi nilishtusha sana na conclusion ile ya Mh Sumari kumuambia slaa eti na wewe sasa leta hoja nyingine...hii ni zaidi ya hovyohovyo...jamani hata kama suala lilikuwa ni la usalama wa Taifa, taifa linapaswa kujua, it should account for it...na unapomuambia mtu abadilishe hoja, Je hizo alizoleta mmezijibu??? halafu pia mawaziri wanasahau kwamba hawamjibu mbunge tu ila wanalijibu taifa...tunawaona, tunawasikia...na mambo mengi ambayo yanatokea sasa kutoka kwa wabunge wa CCM na upinzani ni serious issues...na waziri napoteleza sio tu analidanganya taifa bali pia anaiweka serikali yake pabaya..
waziri anaposema kitu bungeni lazima awe makini, hatakiwi kuwakilisha hisia zake, kila anachosema kinaingia kwenye records kama majibu ya serikali...sasa huku CAG anakubali kutakiwa achunguze makampuni tena kwa kuandikiwa na katibu wa bunge...spika anasema hayatachunguzwa maana kamati ya uongozi ya bunge imekubaliana masuala yale yanahusu usalama wa taifa...hii barua ya CAG inatoka kwa nani???

hoja hazitarudiwa kama zinajibiwa....acheni majibu ya hovyohovyo...
 
Ongezea na Juma Kilimba wa Iramba magharibi aliyewafananisha Mawaziri na mbwa,lipi gumu ovyo ovyo au Mawaziri kufananishwa na mbwa CCM lazima watambue wapinzani ni watanzania na wanawakilisha watanzania bungeni
Na bado, moto utawawakia mwaka huu... nadhani hawakumwelewa Mwakyembe alipowaambia kuwa Watanzania si mabwege tena. na wakiacha kusema wabunge, wananchi nao wataanza kupiga kelele, sijui watamkemea nani na kumtaka afute kauli
 
Ukweli ni kwamba Waziri Sumari aliongea ovyo. Mimi namuunga mkono Zitto Kabwe.

Zitto endelea na msimamo wako huo huo.

Wakati sumari anajibu ovyoovyo na kumnyooshea kidole Slaa, Mwenyekiti aliona ni sawa; Hakumkemea; leo kidole amegeuziwa waziri Mwenyekiti anaona ni kero. Ama kweli mkuki kwa nguruwe.
Wabunge wa CCM acheni kutumia wingi wenu vibaya. Mnayoyafanya yanaoneka live kwenye TV. Hamuwezi kuja majimboni kutudanganya; angalia msije kuzomewa!
 
alishakimbia kule tena nikamwomba hata tumpigie simu kamishina wa madini niweke loudspeaker ateter hoja zake akakimbia toka siku hiyo basi nikasema huyu mzugaji kuna watu wanamtumia na wameshamchoka sasa hata ubunge hautaki tena hata uzalendo hana tena anaamua kufanya anachojisikia yeye yaani kuharibu nchi na wananchi wake

UTAKUWA NA MTINDIO WA UBONGO LAZIMA(Zitto ktk report kasema out of 10 Tz; 2 wana mtindio wa ubongo) now inawezekana anabishana na yule ambaye ana utafiti wake tayari;
 
Back
Top Bottom