Uchaguzi 2020 Zitto mbona haongelei “Grand coalition” tena kama zamani?

Mkuu KUB anapatikana kwa idadi ya wabunge na idadi ya kura za urais.
 
Usisahau kura za urais.
 

Wabunge sio hoja, wanaweza kupata wabunge na mwisho wa siku wakaungana na wakamtimua Zitto bila soni. Usifanye mchezo na Wapemba kwa mahesabu, Prof. Limbumba alipambana kweli kweli kubakiza hata robo ya CUF
 
Zitto hakutaka kuunga mkono UKAWA 2015 leo aungane na nani?!

Kila team icheze mechi zake hakuna kuungana.

NCCR walijidai kwamba wao ndio waliibeba Chadema 2015, leo sijui wako wapi?!

CUF walisema wao ndio waliibeba Chadema 2015, leo hawana hata mgombea wa madrasa.

Dawa ya mamluki ni kuachwa wapambane kivyao, usaliti ni zaidi ya uhujumu, wakae huko huko hakuna cha Grand Coalition!.
 
Zitto amebaki kuduwaa tu. Seif akishirikiana na chadema wameshampora chama chake. Wameshatangaza kupitia TL kuwa wafuasi wa ACT walioko Tanzania bara kura zao watawapa wagombea ubunge wa chadema na mugombea urais wa chadema. Hivyo Membe na hata Zitto mwenyewe hawatapata kura kutoka kwa wafuasi wa chama chao. Yaani wamekatwa kitekniki.
 
Zitto hakutaka kuunga mkono UKAWA 2015 leo aungane na nani?!

Kila team icheze mechi zake hakuna kuungana.
Ni kweli lakini maeneo kma Dar na Kigoma tunaweza zipoteza kma kusipokua na muungano. Imagine Maalim,Zitto,Mbowe na Lissu jukwaa moja.

Inabidi tu washirikiane majimboni na Kata ni mara 10 lipumba ashinde jimbo kuliko lirudi CCM.

Ushirikiano ni muhimu mnoo wakati huu ukizingatia wagombea wengi wanaenguliwa.
 
Zitto alisema kigoma ni ngome yake, sasa ataipoteza vipi naye anachama cha ACT?!

Dar wanaipotezaje hao ACT na hawakubaliki?

Zitto hakutaka kuunga mkono UKAWA kwa madai ni kuifaidisha Chadema, akaenda kwa kina Lipumba na Mbatia kuwashawishi waiache Chadema peke yake.

Unakumbuka Mbatia aliomba aondolewe kwenye serikali kivuli ya upinzani bungeni baada ya kuanza mazungumzo na ccm?!

Unakumbuka CUF walichokifanya bungeni kwa Chadema wakati wa kugombea bunge la Afrika Mashariki?!

Unaunganaje na ACT, hawana chochote zaidi ya kutumika na CCM?!

Muungano mzuri lakini wenzetu vigeugeu sana, tuliachiana majimbo 2015 wakapoteza mengi baadaye wakasema Chadema iliwatumia kama daraja, wakaenda mbali zaidi kudai hata ruzuku igawanwe na wao ambao hawana idadi yoyote ya wabunge.

Tushindwe tusinde sawa lakini kila mmoja acheze mechi zake. Ushinde kivyako, ushindwe kivyako.
 
Unanzanje kuongea kuhusu coalition huku hujuhi wagombea kama wapo au wamekatwa? Tulia, muda bado.
 
Zitto ana stress maana hali ni mbaya.
 

Attachments

  • 2508706_65516dc9-4f6f-4565-aabf-2d87c35b06e5.jpg
    50.2 KB · Views: 1
Too late to calculate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…