Zitto: Msaidizi wa Maalim Seif alinipigia simu mara 4 kutaka kunijulisha msiba sikupokea ndipo akanipigia Rais Mwinyi nikapokea kwa mujibu wa sheria

Zitto: Msaidizi wa Maalim Seif alinipigia simu mara 4 kutaka kunijulisha msiba sikupokea ndipo akanipigia Rais Mwinyi nikapokea kwa mujibu wa sheria

Akizungumza katika kipindi cha Clouds 360 KC wa ACT wazalendo Zitto Kabwe amesema siku maalim Seif alipofariki yeye alikwenda hospitali asubuhi na kuelezwa maendeleo ya mgonjwa.

Anasema ilipofika saa 5 na ushee akiwa katika shughuli za chama alipigiwa simu na msaidizi wa maalim Seif aliyekuwa anashinda pale hospitali na hakuipokea.

Akapiga tena mara tatu zaidi lakini Zitto hakupokea kwa sababu alijawa na uwoga na hakuwa tayari kupokea habari mbaya kwa wakati huo, anaeleza Zitto.

Baadae kidogo nikapigiwa na mh Rais wa Zanzibar Dr Mwinyi ndipo kwa mujibu wa sheria ikanibidi nipokee na akanijulisha habari za msiba na tukakubaliana alitangazie taifa kisha nasi kama chama tukatangaza baada ya tangazo la serikali, amemalizia Zitto Kabwe.

Chanzo: Clouds TV

My take: Kiongozi anayeogopa taarifa ya msiba anaweza kuwa amiri jeshi mkuu kweli? Maana 2025 Zitto anatajwa kugombea urais.

Maendeleo hayana vyama!
Sasa wengine wanaogopa hata kutanganza maradhi sembuse kifo.........sijui kama ikitokea watatutangazia kwa mda ule ule
 
Back
Top Bottom