Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Status
Not open for further replies.
Ila kuna watu wanafiki sana na zito ni mmoja wao... hivi JPM akipatwa na mabaya wewe utafaidikaje?

Nilipitia Kurasa zake katika hizo Siku za Uvumi nilisikita mno na nashangaa leo tena ameguka ghafla na kuonyesha huu Uugwana ambao hata sijui ameutoa wapi. Bahati nzuri Waha ni Watani zangu wakubwa tu ila kama kuna Tunu / Shani ambayo wamebarikiwa nayo na hata Yeye nae anayo ni ya ' Unafiki ' uliotukuka.
 
Nitashangaa kama ataendelea kurandaranda mtaani. Kwasababu kuna watu tunampemda rais hadi tunaumwa. Kasababisha tumepata heart [emoji813] attacks pasipo sababu.
Daah kwa kweli waliharibu jmapili yangu sana ! Mpaka rafiki zangu wa Kenya wamenipigia wakidai ufafanuzi.
 
GODBLESS Lema nae siasa uchwara na za hovyo sijapata kuona, kwenye issue ya bureau de change alishadadia nchi imeishiwa forex, kwahiyo inapora wafanya biashara. Mara hii nayo kaidakia juu kwa juu !
Kamanda Lema na mwenzie KC wa ACT wazalendo Zitto Kabwe siyo watu wa kuwatilia maanani kabisa watawapotezea muda wenu bure

Mungu ni mwema
Nawatakia Jumapili yenye furaha.

Maendeleo hayana vyama!
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Zitto, ulitoka chadema na ulipoteza imani kwa watu. Umepambana, watu wanaanza kurudisha imani kwako unakuja na upuuzi wa rais kafa na unasherehekea kuwa kuna hope.
Sidhani kama utapata imani ya watu tena zaidi genge lako. Ulichoandika hapa ni nafsi imekusuta na unafiki.
 
Ww utakuwa mwendawazimu, afike aanze kuwaambia wananchi kuhusu afya bila wao kumuuliza!? Utakuwa ni mkutano au ni siku ya chanjo na vipimo?
Kwa hiyo anasubili wananchi wamuulize juu ya afya yake, kama yeye anavyouliza afya ya rais? Yeye atueleze tu bossmaana ni siku nyingi. Tangu yule binti aliyetutoka!
 
VVU a.k.a Vyama Vya Upinzani sasa vimefirisika kabisa.
Hata kiongozi kubwa kabisa wa chama anacheza MDUNDIKO(anaogelea bwawa moja na wazushi mitandaoni)
Kwa hakika sikutarajia kabisa.
Mh. Ziro Zushi Kafiri unatakiwa kuomba radhi bila kukosa.

Kosa walilofanya viongozi wakuu wawili wa vyama vya upinzani 2015 waliofanya upinzani kutokuchukua madaraka NI LAANA ambayo itawatafuna pamoja na vizazi vyao kwa miaka mingi ijayo, mpaka generation tatu zipite!!!! Viongozi hao wanajulikana na wanajijua!! Ndiyo maana wanazushia Viongozi wengine vifo(the curse is really biting)!! Who will be in a position to break the curse or rather to have the leaders who played the major roll delivered? Allah(God/Jesus) knows better!!
 
Hakuna box la kura nchi hii, bali kuna tendo la kuwasimika wanaccm kupitia hadaa ya box la kura.
Hiii siielewi jomba..hivi mawakala was vyama huwa hawapo au wapi..kwa hiyo hizo hadaa zinatumia miundo gani
 
Kiutendaji, Rais wetu anafanya mambo mengi sana ambayo yangefanywa na wateule wake.
Wengi wa wateule wa Rais wamekuwa kama watazamaji tu wakimsubiri Rais au Waziri Mkuu afike maeneo yao na kutumbua watumishi na wakandarasi kutokana na ubadilifu wa mali za umma.
Waatalamu na Wanafalsafa wanasema " Design a system and system will work for you"
Rais wetu anamifumo mingi ya utendaji wa kazi na anafanya kazi kwa masaa mengi ambayo kiafya hairuhusiwi.
Inawezekana mifumo hii ya kazi inamtegemea yeye tu kuisimamia.
Wakuu wa Mikoa na Wilaya wako wapi mpaka ubadilifu mkubwa wa mali ya umma unatokea bila wao kujua na kuchukua hatua.
Tukisubiri kila kitu afanye Rais au Waziri mkuu tunawachosha hawa watu na wataadhirika kiafya.
Kama kila kitu tunasuburi Rais au Waziri mkuu atoe adhabu jukwaani wakati wateule wake wapo, utawala wa namna hii huitwa " management by crisis".
Utawala wa namna hii humfanya Kiongozi wa juu muda mwingi awe na hasira na maamuzi mengi yanayofanywa yanatokana na hasira.
Je hawa Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya ni watu wa maigizo tu na wanafanya mambo kama ya kuigiza ili kumfurahisha Rais na Waziri Mkuu wakati mambo mengi yanaenda hovyo na watu wanaonenewa mpaka Rais afike na kutoa msaada.
Tukumbuke yule Mama wa Sumbawanga aliyeibiwa ng'ombe 25, akampata mwizi wake, mwizi akawekwa ndani lakini baadaye akawekewa dhamana huko huko polisi na baadaye kutoroka.
Mama alipotoa malalamiko yake kwa Rais, OCD aliambiwa na Rais amlipe huyo mama shi milioni kumi na tano ndani ya siku tano.
Tujiulize, Huyu mama hakufika kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, RCO, RPC RSO na wengine wote kutoa malalamiko yake? Lazima alifika lakini hakusikilizwa.
Je Polisi wanaruhusiwa kutoa dhamana kwa jambazi ambalo hata kule mahakamani Sheria hairuhusu?
Hakika yule mwizi wa ng'ombe ni mshikaji wa hawa wakubwa na pengine amewasumbua watu wengi sana.
Watu walioonewa kama mama huyu Inchi hii ni wengi sana na viongozi wanawajua lakini hawawasaidii kwa kuogopa lawama au kunufaika na uonezi huu kwa kupewa kitu kidogo na wadhulumaji.
Tulinde afya ya Rais wetu kwa kutekeleza yale anayotaka kila siku na hatua kwa hatua.
 
Ukiona haya yanatokea kwenye nchi ambapo watu wake wanajinasibu kuwa na umoja ujue UFA ushaanza kujitokeza ya utengano na amani kupungua
 
Hiii siielewi jomba..hivi mawakala was vyama huwa hawapo au wapi..kwa hiyo hizo hadaa zinatumia miundo gani

Hao mawakala ndio wale wakurugenzi hukwepa kuwaapisha. Kwa macho yangu nilishuhudia kituo kimoja wakati wa uchaguzi wa marudio mawakala wa cdm wakipewa kipigo kikali na jeshi la polisi, ili kujaza fomu fake ya matokeo kuwa mgombea wa ccm ameshinda, na huo ndio utaratibu uliotumika nchi nzima. Kama ulikuwa hujui ama unajifanya hujui huo upuuzi, basi habari ndio hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom