Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Status
Not open for further replies.
Zitto brother umetuangusha sana. Bado unafanya siasa za kitoto! Jinsi ulivyo handle hizi tetesi binafsi zimenivunja moyo sana. Kama ni visasi basi nyie mtakuwa hatari mara mbili ...
 
Magari mrngine noma kweli
IMG-20191020-WA0005.jpeg
 
Nikikumbuka jinsi Tundu Lissu;
●Alivyopigwa risasi Bungeni
●Alivyonyimwa matibabu na Govt
●Alivyonyimwa mshahara
●Alivyoporwa ubunge
Kwa kweli sasa nimeamini malipo ya ubaya ni hapa hapa duniani.
Ukimtendea ubaya mwenzio nawe utalipwa kwa ubaya.
Endelea tu kukumbuka sisi Wala haitusaidii kitu kwenye maendeleo ya Taifa na isitoshe hata pesa ya matibabu hukuchangia japo hata kwa njia ya m.pesa ulituachia tu sisi watu wake wa karbu kushughulikia matibabu yake leo hii kapona ndo unakuja unajilizaliza kinafiki hapa jamii forum!! Yani wewe mtu cjui una matatizo gani tu..
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Ninapomuona Rais anasimama, nakudharau sana Zitto. Msifanye siasa kwenye mambo yasiyo na siasa
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Anaapisha watu Ikulu huko. Siasa za matukio ni shida
 
Zitto nakwambia live mbele ya wapambe wako hiyo tabia ya kuombea na kuzusha mabaya kwa Mwanaume mwenzio Tena anayependwa na familia yake anayoiongoza ya wanyonge kuliko unavyopendwa wewe ipo siku hizo chuki binafsi zitakurudia mwenyewe ...mungu Ni wetu sote baada ya kuombeana uzima wewe na kigogo wako mkaona mshike matako ya vabaraka wenzenu wa hii nchi kuiombea taasisi ya rais mabaya..haya mungu yupo na anayaona yote haya
 
Nipo hapa naangalia Upendo tv na Mungu ananibariki sana.

Kiukweli Zitto na waswahili wenzake akina Kigogo 2014 wamefeli vibaya sana.

Hakika taifa letu limesimama katika misingi ile ile aliyotuachia baba wa taifa mwalimu Nyerere.

Mungu endelea kumbariki Rais Magufuli.

Nawatakia dominika njema!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom