Wakuu,
Akiwa kwenye mkutano na wananchi Kigoma, leo Novemba 29, 2024 Zitto amesema;
Nataka nimwambie mwenyekiti wa CCM Rais Samia, kama kuna kosa ambalo CCM wanafanya ni kusurrender siasa kwa vyombo vya ulinzi na usalama. Vyombo vya Usalama vikishaonja madaraka ya kisiasa kama hivyo unavyofanya watakaofata kushughulikiwa ni CCM wenyewe, hivyo vyombo vitawaondoa CCM Madarakani.
Tunayoyaona ayantokea Angola, Mozambiki ni makosa ya FLELIMO na MPLA kusarenda kisiasa kwa vyombo vya dola ndio maana muda wote wangu wote nilivyokuwa mbunge katika jambo nililokuwa nalipigania kwa nguvu zangu zote ni kuiondoa Idara ya Usalama wa Taifa katika makucha ya CCM, nikawapigania mageuzi ya TISS kwasababu ni kosa kubwa sana kuiondoa nchi kwenye democracy na kuipeleka kwenye nchi inayoongozwa na vyombo vya dola.