KERO Zoezi la uhakiki wa taarifa NMB

KERO Zoezi la uhakiki wa taarifa NMB

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Mwezi uliopita nilidhamilia 100%nihakiki,kwa unynyekevu nikasogea tawini,panga foleni nafika tu naambiwa NIDA mtandao unasumbua,zoezi likaishia hapo,naeudi nyumbani niko kwenye harakati nyingine nikaangusha kitambulisho cha NIDA,na hawataki namba wanataka kitambulisho kabisa.

Kwa sababu shida ni yao,nasubiri wafunge hiyo acc nihamishe bank ya kupokelea mshahara maana naona tunasumbuana tu.
Kwamba hawakubali kupokea namba ya NIDA hadi uwe na kitambulisho chenyewe kabisa?
 
Vijana wa siku hizi hamna ubunifu enzi zetu tulikuwa tunaweka mawe kama foleni kusubiri unga wa Yanga national milling na kwenye kusubiri sukari utafikiri unapewa bure then unaenda kupiga mishe jiwe linakuwa linasogezwa tu no kupoteza muda ukirudi unakuta jiwe lipo namba 2 unakaa dk 2 unahudumiwa unaenda sasa ninyi mnashinda Nyerere square
Nani atakuwa anakusogezea ukiwa wewe haupo?
 
Huwezi kubali kuwa wa Tanzania wengi hivi ni wateja wa NMB, tuliowahi walau hatukuteseka sana,

Tatizo la kuongojea tarehe za mwisho mwisho ndilo limewakumba wengi.

Jana mmama mmoja kapewa namba 370, just imagine.
Nina account mbili huko,nifungue nisipohuisha nini kitatokea?
 
nadhani ndo itakuwa hivyo, ila suala la kuhakiki litakuwa pale pale...
nitasubiri watu wakipungua ifikapo mwezi wa 9 ndo nitaenda
Hakuna closure yoyote ya akaunti inayotumika. Ila wanapenda kuwasumbua watanzania tu.
 
Mmeenda wote /wengi siku z mwisho.mnategemea.kisiwe na foleni...Jana nimeona NMB Mkoa Fulani kundi la watu kama 300,Sasa hapo utalaumu Nini
Unajua wewe unachokitetea hata hakijulikani?

Umeambiwa hata kama watu ni wengi bado wameendelea kuweka dawati moja kwa ajili kufanya kile kile walichokuwa wakikifanya kipindi wateja ni wachache so shida inakuja kwanini wasiongeze watoa huduma kipindi wateja wamekuwa wengi?Umeelewa Sasa???
 
Nimepita Leo nilikuwa nataka nione km acc yangu Bado Iko hai😄
Aisee watu Wana moyo siwezi mi foleni ile🙌

Mi nilienda direct Kwa mdada 1 nikamwambia shida yangu ,akataka kadi ,nikampa akacheki...km dkk5 nimemaliza

Wakati nataka kuondoka nikamuuliza ni nn hii foleni ,ndo akaniambia😄 wanahakiki...
Akasema ila ni Kwa watu waliotumiwa ujumbe tu!
So sio wote wanaohakiki
 
hama , toka kwenye usumbufu huo
Nyie mbona hamuhami nchi kila siku mnapiga kelele.
Tunachotaka wajipange na kuboresha huduma.
Mie nipo kalambo huku unataka niende bank gani kwa mfano?

Unadhani kila mtu yupo mjini kwenye utitiri wa benki?
 
Mashine zao zote zina FP Option ama watabadili walete mpya?

Whatever it will be, FP tayari ziko Nida, wanataka nikachukuliwe nyingine za nini?

Lakini pia PIN is the easiest way, FP zina usumbufu sababu ya mitandao yetu. Ngoja tusubiri.
Mara nyingi unaweza kutumia mojawapo kati ya hizo.
Mfano rahisi ni kwenye simu tu. PIN ama biometric sign.
 
Zoezi la uhakiki wa taarifa bank ya NMB ni kero kwakweli, foleni ni ndefu kila branch, watendaji hawajipanga, inchukua hadi dk 20 kwa mtu mmoja kuhudumiwa na wahudumu kwa kila branch ni mmoja.

Mara waseme mtandao unasumbua kwahyo mshine inachelewa.

Nimezunguka NMB branch zote Dodoma, msururu wa foleni ni mrefu, uwe umekula umeshiba n uwe n nguvu za kusimama ili kusibiri foleni yako ifike.

Wajipange upya na waongeze muda wa zoezi.
Wanahakiki nini kwani? Mbona wao tu miaka nenda miaka rudi?
 
Huwezi kubali kuwa wa Tanzania wengi hivi ni wateja wa NMB, tuliowahi walau hatukuteseka sana,

Tatizo la kuongojea tarehe za mwisho mwisho ndilo limewakumba wengi.

Jana mmama mmoja kapewa namba 370, just imagine.
Duh! huu Usumbufu ni kwa garama za Nani?
 
Nimepita Leo nilikuwa nataka nione km acc yangu Bado Iko hai😄
Aisee watu Wana moyo siwezi mi foleni ile🙌

Mi nilienda direct Kwa mdada 1 nikamwambia shida yangu ,akataka kadi ,nikampa akacheki...km dkk5 nimemaliza

Wakati nataka kuondoka nikamuuliza ni nn hii foleni ,ndo akaniambia😄 wanahakiki...
Akasema ila ni Kwa watu waliotumiwa ujumbe tu!
So sio wote wanaohakiki
Kwani kufungua Akaunti mpya wakati nahitaji Akaunti ya NMB itagharimu nini?
 
Back
Top Bottom