GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
1. Walikuona unakula dagaa, watasema umefilisikaKwenye maisha, usihangaike wala kuzingatia sana walimwengu, hawana jema.
Watu wana asili ya roho mbaya, hata yule anaeonekana anakuchekea, usishangae hali haiko hivyo moyoni, si kila mtu anafurahia mafanikio yako.
2. Wakiona unakula vyuku, watasema unaringa
3. Ukiwa na tabia ya kuwatembelea majirani zako, watasema umekosea kazi
4. Ukiwa unatoka saa kumi na Moja Asubuhi na kurudi saa tano Usiku, watakutuhumu hujumuiki na majirani
5. Ukinunua IST used, wataaita mkweche
6. Ukinunua V8, watasema la "bosi" wako
7. Ukijenga ghorofa, watasema umeiba
8. Usipowakopesha, watasema una roho mbaya
9. Ukifanikiwa katika mambo yako, watakuambia walikuwa wakikuombea
10. Mambo yako yakiharibika, watajitapa kuwa walijua tu kuwa hutafika mbali.
Vyo yote iwavyo kwako hawatakosa cha kusema!
Ili wasikuseme, ukubali kutokuwa chochote wala kufanya chochote!