Wakati wa ukuaji wangu nilikuwa nasikia matendo mabaya sana kuhusu aliyekuwa Rais wa Uganda, Id Amini Dada, moja ya matendo hayo ni pamoja na ulaji wa nyama za watu hasa waliokuwa wapinzani wake wakubwa. Rejea Idi Amin Dada : The Ugandan Butcher & Murderous Cannibal
Uvumi ulienea kwamba aliweka vichwa vya wanadamu kwenye jokofu lake. Na alikiri kula nyama mara kadhaa. Kuna mahali nimeona amenukuliwa mwaka wa 1976 akisema "Nimekula nyama ya binadamu, ina chumvi nyingi, hata zaidi ya chumvi kuliko nyama ya chui."
Kuna wanaosema kuwa suala la Idi Amini ni propaganda zilizozushwa na maadui zake, pia kuna waliosema ni kweli alikuwa mtumiaji mzuri wa nyama za binadamu.
Aliyekuwa Rais wa Venezuela, Hugo Chavez aliwahi kunukuliwa haya...